Kwa Rais Magufuli tu - Must Read 2017

Kwa Rais Magufuli tu - Must Read 2017

Hayo ni maoni yako ila kundi linalompenda nikubwa sana kuliko uzaniavyo, usije ukawa unashinda hapa jf na ikawa ndio tathimin yako kuwa Bw Pombe hapendwi.Kwa sisi wafanyakazi tunampenda sana mfano tu mdogo wakubwa wengi wa Idara zama zilee walikuwa ni kama miungu watu ila sasa wamekuwa wa kaida sana tuu.na wamekuwa hata ushauri wakiomba kwa wafanyakazi wa chini, Kikubwa usijidanganye wala kudanganywa na story za vijiweni.
Piga kazi mkuu kila kitu utakiona sawa tu.


Kwa hiyo Watanzania wote 45m ni wafanyakazi na wana wakuu wa idara? Naona hata yeye mwenyewe JPM anafikiri kuwa kila mtu ni mfanyakazi na anapiga dili tu. Thinking while living in a cubicle!
 
Achana nae afie mbali yeye si bingwa ? Let him rott in hell.
 
Ni sababu hii tu mkuu au kuna zingine?
Mkuu, sababu aliyotoa NI MTAZAMO TU, ni kubwa sana, labda kama wewe si mtumishi wa uma au ni kigogo ama una mahusiano makubwa na vigogo.

Wafanyakazi wa chini walinyanyasika sana, uhamisho wa ovyo, kunyimwa safari, seminars, ovetime nk.
Kulikuwa na watu maalumu waliokuwa wakisafiri, wengine hawafai. Kulikuwa na watu maalumu wanoenda semina, wanapewa vitengo maalum vya ulaji, ukihoji unapata uhamisho. Lakini tangu zama hii imeingia hakuna safari za hovyo, na ikitokea anaenda mtu wa kitengo husika tena aliye mpetent. Maana kwanza lazima ruhusa inayoombwa ieleze kwanini mtumishi asafiri, itagharimu shilingi ngapi? Nini manufaa ya safari hiyo kwa taifa?

Hivyo, sababu aliyotoa NI MTAZAMO TU. ina mashiko, hivi sasa mnajadiliana na mkuu na anakusikiliza.

Kwa upande mwingine hata utendaji, umebadilika KAMBAKU! Kwani husikii raia wanafurahia wakienda maofisini? Wanasema watumishi wamebadilika sana, wanajituma.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
hahaha mkuu una utani wa ngumi, si kweli kwamba naomba kireja reja, ila ni kweli nina elimu kiduchu maana sina PhD. Kwa maana hiyo tu ya kutokuwa na PhD na si kingine.
Duh! Kwahiyo hivi sasa usipokuwa na Phd, elimu yako ni kiduchu? !
 
Kusema ule ukweli, hakuna mtumishi yeyote wa umma mwenye akili timamu anayempenda Magufuli.
 
Ushauri murua kabisa, mleta uzi umesemea mioyo ya walio wengi sana, hongera
 
Hayo ni maoni yako ila kundi linalompenda nikubwa sana kuliko uzaniavyo, usije ukawa unashinda hapa jf na ikawa ndio tathimin yako kuwa Bw Pombe hapendwi.

Kwa sisi wafanyakazi tunampenda sana mfano tu mdogo wakubwa wengi wa Idara zama zilee walikuwa ni kama miungu watu ila sasa wamekuwa wa kaida sana tuu.na wamekuwa hata ushauri wakiomba kwa wafanyakazi wa chini,

Kikubwa usijidanganye wala kudanganywa na story za vijiweni.

Piga kazi mkuu kila kitu utakiona sawa tu.
Kaz mkuu kasimamisha kwa sbb ya uhakiki hewa. Mpaka uhakiki uishe watu watakuwa mabilionaire. NYIE SSM WANAFIKI SANA NA SLOGAN YENU. MNAHIMIZA WATU WAFANYE KAZ NA WAKATI KAZ ZENYEW MEZUWEKA UVUUNGUNI. WANAFIKI SANA NYIE.NCHI YA VIWANDA POOR SSM
 
Ushauri mzuri sana,wafanyakazi tuna hali ngumu sana)

["Hayo ni maoni yako ila kindi linalompenda nikubwa sana kuliko uzaniavyo, usije ukawa unashinda hapa jf na ndio ikawa tathimin yako kuwa Bw Pombe hapendwi.

Kwa sisi wafanyakazi tunampenda sana maana wakubwa wengi wa Idara zama zilee walikuwa ni miungu watu ila sasa wamekuwa wa kaida sana tuu.

Kikubwa usijidanganye wala kudanganywa na story za vijiweni"]
.

Hizi kauli mbili tata sana..sijui tuiamini ipi..NI MTAZAMO TU anasema wafanyakazi sasa wanakula raha za ajabu..OMEL123 yeye anasema hali mbaya..hawa wote ni wafanyakazi nadhani wa Serikali..Ila mtoa mada kuna baadhi ya shauri zako ni VALID zina mashiko..tutamwambia Mzee JPM afanye mambo mazuri
 
Naomba namba ya JPM nijitoe mhanga nimfowadie haka ka walaka kazito sana, au nipe email take maana mimi sina cha kupoteza iwe milioni saba, kifungo au vyote viwili.
Mkuu umesahau option ya tatu kuwa ben saananed u need to reconsider
 
Kwa jinsi ninavyokusoma,nawe hujiamini,unaogopa kutimbuliwa maana unauma kiaina na kupoza kiaina,why not so straight?!!
 
Kum
Raisi anafanya mengi mazuri lakini hili la kuamuru watendaji wake wasilipe madai ya PPF ya wastaafu wa ATCL hata pale mahaka inapo ipa PPF amri ya kukamata mali za ATCL na kuziuza kufidia madai hayo mimi sikubaliani nawe. Una minya mamlaka ya mahakama na kwa kuwa viongozi wote wanakuogopa basi haki sasa haitendeki mahakama haina sauti.
Kumbuka alishasema muhimili mmoja umejichimbia chini zaidi.
 
Kwel we2 Ninja,kwa ujumla nimelipenda andiko lako lenye mashko na kama sizonje kwel anapitia jf achukue huu ushaur na akaufanyie kazi,nilienda mafinga kwa lengo la kufanya biashara ya mbao nikiwa na kijisent kidogo il niboost kijimtaj changu lkn kwa kuwa co mzoef ilinipasa nijifunze kwa waliowazofu,ktk vijiwe vyote nilivyopita walikuwa wakimwongelea mzee wa kaya jins alivyobana mzunguko wa pesa hasa kwa wafanyakaz ambao wanasema wazuiwa kukopa kwan kukopa kwao walikuwa wanajitahd kujenga na mbao zilikuwa zinatoka kwa kas lkn pia malori meng yalikuwa yanasafirisha mbao kwenda maeneo tofauti2 lkn pia walinishaur kama umekopa na unataka kufanya h biashara ktk utawala huu n hatar kwa pesa yako kwan kunautitil wa kod hyo unaweza kuuwa mtaj lkn nilijkaza kwa kuwaambia n mtaj wa shamba na sasa nataka kutanua biasha zangu kidogo wakanip mahope kuwa nicarry on na biashara lkn walikuwa bado wanasema ngoja 2subir 2020,sasa huyu anaesema kuwa magu anapendwa na weng sizan kama anamtakia mema! hal ilipofkia sio pazur.
 
Mtoa mada umenena huo ndo ukweli kama atasoma ujumbe wako ni vema atilie maanani.msema kweli ni mpenzi wa mungu nawe umesema kweli siyo kama wale wanaomchekea hali hawataki kusema ukweli. Big up for your opinion
 
Aisee nipeni Post box ya Ikulu niandike hii barua niitume kwa Mkuu.
 
Mie nadhani mngemshauri mbowe kwamba kama upinzani tunatokaje hapa....mh rais hukumpigia kura hivyo achana naye.
Nyie ndiyo wale nawaitaga wachumia Tumbo. Yaani ww ukishashiba Leo basi, akili zenu ni Kama hayawani, yaani wanyama coz hamna ufahamu.huyo mshauri ameshauri vizuri sana, ww ilitakiwa uongeze ushauri wako mzuri zaidi ili umsaidie kiongozi wetu Kama unamtakia mema.

Nyie ndiyo wale bendera fata upepo, ili mradi tu ushibe, hata ukilishwa matope. Yaani ulimi wako hausikii na wala huitaji ladha. Ni Kama chatu. Ww ni kumeza tu. Shauri yako!
 
Yaaani point ipo pale kwenye Solution tuu!

Kusikiliza ushauri wa wasaidizi wake...likini pia sio kila ushauri ni wa kusikiliza..


Huko kwingine umeendika upuuzi tuu!

Yaani eti aachie wapiga deal ili 2020 ashinde?
1. Yale mambo ya flow metre feki kule bandarini yaendelee?

2.Makontena 3000 yapotee tena?
3. Tuendelee kuwa na wakuu wa idara watemi? Wasiokuwa na nidhamu?
4. Aruhusu madawa ya kulevya yaendelee kupitishwa pale airport?

5. Aruhusu tembo waendelee kuuwawa?

6. Aruhusu wale jamaa wa 7milion kwa dakika waendelee na biashara yao...

Mkuu kama umetumwa na wapiga deal wenzako kawaambie karata yenu imemangwa...

Sisi walalahoi tunampenda magufuli hivyo hivyo alivyo!

Magufuli nyooosha mbele kwa mbele.
Endeleeni kumsifia si zamu yenu sasa " kula nchi" ila uzuri Faru John hatabiriki muda wowote kibarua kinaota majani ndipo akili zitawarejea.
 
Back
Top Bottom