Lakini Juni 20, mwaka huu, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake (CCM) Taifa, Sophia Simba, ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), aliwataka wanawake wa jumuiya hiyo wanaoishi na wanaume ambao si wanachama wa CCM kuwanyima waume wao unyumba kwa lengo la kuwakomesha. Ninyi wanawake wenzangu ambao waume zenu wapo katika vyama pinzani na mnajua wazi kuwa hawawapi ushirikiano wowote katika siasa ya CCM wanyimeni nonino, muone kama hawatarejea katika chama tawala, nonino nikiwa na maana ya tendo la ndoa, alisema Sophia huku akishangiliwa na wanawake wote kuonyesha kuwa alilolisema limewagusa.