Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Siku yangu ya leo imeharibiwa na story mbili kutoka kwa FL1 na Babra ambazo zote zinahusisha simu ya mkononi. Nimekwazika sana kwa hivyo vitendo vya hao wanaume. Kwa hiyo nimeonelea niandike kidogo kuhusu uzoefu wangu kuhusu tunavyotumia simu zetu (mimi na wife), labda inaweza kutusaidia sisi kwa kupewa ushauri na wadau au kusaidia wengine.
Kwangu na mama watoto (my wife wangu), simu zina mwenyewe kwa maana ya kutumia kwa wakati huo na pia kwa kuangalia nani aliichagua wakati inanunuliwa. Vinginevyo nina uhuru wa kuigusa na kutumia simu yake 24/7 naye pia anashika na kutumia simu yangu wakati wowote. Watu wote kwenye address book zetu wameingizwa kwa majina yao. Mimi nime-save jina la mke wangu kwa kuatnguliza "my sweety wife....". Pia mimi kanipa jina la "my darling husband". Mke wangu anatabia ya kufuta call records au sms lakini mara nyingi namwambia kuwa siyo vizuri kufuta zote kwani inaweza kuleta mashaka yasiyo na sababu. Kwa ujumla sijawahi kupata shida kuhusu simu yake naye hajawahi kuwa na tatizo na simu yangu pia. Kwa hiyo naamini wanaoficha/wanaoweka vikwazo (embargo) kuhusu simu zao hawajiamini kwenye suala la uaminifu katika ndoa/mahusiano. Vinginevyo sisi ndio hatujui maana ya hicho kitu kinachoitwa privacy kwenye simu ya mkononi.
Kwangu na mama watoto (my wife wangu), simu zina mwenyewe kwa maana ya kutumia kwa wakati huo na pia kwa kuangalia nani aliichagua wakati inanunuliwa. Vinginevyo nina uhuru wa kuigusa na kutumia simu yake 24/7 naye pia anashika na kutumia simu yangu wakati wowote. Watu wote kwenye address book zetu wameingizwa kwa majina yao. Mimi nime-save jina la mke wangu kwa kuatnguliza "my sweety wife....". Pia mimi kanipa jina la "my darling husband". Mke wangu anatabia ya kufuta call records au sms lakini mara nyingi namwambia kuwa siyo vizuri kufuta zote kwani inaweza kuleta mashaka yasiyo na sababu. Kwa ujumla sijawahi kupata shida kuhusu simu yake naye hajawahi kuwa na tatizo na simu yangu pia. Kwa hiyo naamini wanaoficha/wanaoweka vikwazo (embargo) kuhusu simu zao hawajiamini kwenye suala la uaminifu katika ndoa/mahusiano. Vinginevyo sisi ndio hatujui maana ya hicho kitu kinachoitwa privacy kwenye simu ya mkononi.