Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,599
- Thread starter
- #101
Watu walikuwa wanacheat ndani ya ndoa zao kabla ya simu za mkono kuwepo na wataendelea kufanya hivyo hata kama mume au mke anakaa na simu ya mkewe 24/7. Kuwa na access na simu ya mkeo au mumeo saa yoyote unayotaka ili uipekuepekue simu na txt messages zilizoingia na kutoka haina maana kwamba huyo mwenzio hatoki nje ya ndoa hata kama hutaona lolote katika simu hiyo. Njemba aliyempiga mkewe kwa kukataa kumpa passwords za email addresses kwanza alianza kuichukua simu ya mkewe na kukaa nayo kwa masaa mengi tu lakini hakuambulia kitu ndipo alipoamua kuomba passwords za hizo addresses na mama kukataa katakata.
Kikubwa ni kuaminiana tu ukitaka kujipiga kifua eti nina access ya simu ya mke/mume wangu 24/7 hivyo hakufichi chochote na hatembei nje, basi unajidanganya sana.
Kuna mama mmoja hapa aliandika kwamba mumewe alikataa kata kata kwamba asiwe na simu ya mkono maana zinaongeza uwezekano wa kutembea nje ya ndoa. Mama huyo aliandika kwamba alinunua simu ya mkono bila kumtaarifu mumewe na huificha anakokua mwenyewe na mume hajaigundua kwa miaka sasa.
BAK,
Nadhani tunahitaji kuelewana kwanza kwenye hoja ya msingi. Sijasema popote kuwa, mtu akiwa huru na simu ya mwenzi wake ni sawa na kuipekua pekua. Pia simaanishi kwa lolote kuwa usipokuta call au sms za wapenzi wa mwenzi wako ina maana kuwa huyo ha-cheat. No, don't miss the point.
Swali langu la msingi ni kuwa, kama wewe na mwenzi wako mnashiriki kila kitu, unaanzia wapi kudai kuwa simu ni personal kwa hiyo hana ruhusa ya kuishika? Hapa tunaongelea suala la kuweka mipaka ya kugusa na hata kutumia simu ya mkeo/mumeo na vitu vingine kama email, bank cards etc.