Kwa nini Rais analazimisha kitu ambacho hana madaraka nacho ya Kikatiba? (Video)

nafikiri aliongelea mtu wa kuteua tume. sijaona kwenye majadiliano haya kama si Rais ni nani mwingine anayepaswa kuteua tume kwa sheria zilizopo, wengi wanasema tume iteuliwe na wananchi wenyewe - kivipi?

Prof. Shivji alipendekeza tume iteuliwe na vyuo vikuu na vyama vya kitaaluma je itakubalika na wote?

nilisikia wengi wa wanaharakati wanasema wananchi hawajashirikishwa lakini hawasemi walihoji wangapi?
au wanasema maoni ya wananchi hayajajumuishwa je ni wangapi walioshiriki na ni wawapi?

Hili si tatizo kubwa hivyo. Ni suala la kuweka Principle tu. Kwa mfano sasa hivi Rais anateua mwenyekiti wa bodi na mawaziri wanateua wajumbe wa bodi! Kwanini RAis hateusi wote kwa mpigo? Lakini kwenye Katiba Rais anateua mwenyekiti na Katibu na wajumbe 116!! Rais ndiye anaiitisha Bunge la Katiba na kazi yote mwisho inamrudia yeye kwa maamuzi. Really?
 
Hili si tatizo kubwa hivyo. Ni suala la kuweka Principle tu. Kwa mfano sasa hivi Rais anateua mwenyekiti wa bodi na mawaziri wanateua wajumbe wa bodi! Kwanini RAis hateusi wote kwa mpigo? Lakini kwenye Katiba Rais anateua mwenyekiti na Katibu na wajumbe 116!! Rais ndiye anaiitisha Bunge la Katiba na kazi yote mwisho inamrudia yeye kwa maamuzi. Really?

Hivi wewe unajua maana ya taasisi ya urais???
 
Tume zote zizowahi kuundwa ili kukusanya maoni ya wananchi na hatimaye kufikia kufanyiwa marekebisho ya katiba ndiyo yaliyotufikisha hapa tulipo. Rais haaminiki kwa sababu watangulizi wake ambao walikuwa wenyeviti wa CCM hawakufanya marekebisho ya katiba kwa kufuata maoni ya wananchi. Je kwa mantiki hiyo tutawezaje kumwamini rais wa sasa ambaye ni mwenyekiti wa Chama kisichotaka mabadiliko kuwa atazingatia maoni ya wananchi katika kuandika katiba mpya? Kwa mtazamo wangu kinachofanyika sasa na kitakachofanyika ni kurejea yaleyale ya tume zilizopita

Ni kweli mkuu kwani Raisi wetu amezoea kusema hata wenzangu walifanya hivihivi kwanini mimi ninapotakiwa kufanya napingwa ?
Wengi tulijua anataka kufanya jambo tofauti lakini yeye kumbe
Nia yake ni kuendelea na makosa ya watangulizi wake .

Mimi binafsi nitashindwa kumtofautisha na dikteta kama atasaini mswada wa kuwafunga watu wanaoujadili.Nijuavyo udikteata ni kuwanyima watu haki hasa ya kujieleza.Kama mtu amenyimwa haki ya kujieleza katika jambo lolote hata kama ni kutetea jambo ambalo wengi au wachache hawalipendi ana haki gani tena.
 
Hiyo katiba mpya itaundwajwe bila ya Rais?? yaani utaratibu uweje labda tusaidiana hapa maana mimi nashindwa kuwaelewa wengi wenu???

Mkuu ninavyoelewa kuna mwanataaluma mmoja amependekeza raisi apelekewe majina ya wanataaluma, wanaharakati, etc (watu kutoka makundi ya kijamii) ambao wameteuliwa na wananchi. Watu hao au majina hayo yatakayopelekwa kwake yeye atachagua kamati kutoka kwenye hayo majina. In other words, wananchi hatutaki kamati iliyoteuliwa na Kikwete/CCM bali wanakamati wapendekezwe na jamii/wananchi na yeye atachagua katika kundi hilo i.e. atatoa short list wa watu wa kamati kutoka kundi hilo. Raisi hawezi kuchagua kamati yeye,(kupendekeza watu wake) kwasababu him and his part tayari watakuwa na influence interest zao kwenye katiba. Watanzania wanataka watu neutral watakaowakilisha mapendekezo yao. Kwa mtizamo wangu raisi anaelewa kabisa wasomi/watanzania wanaolalamika wanataka nini, lakini anatumia ujinga wa watanzania wengi wakutokuelewa kama mtaji wake wakujichukulia madaraka mikonono na hii ni hatari sana.
 
Hili si tatizo kubwa hivyo. Ni suala la kuweka Principle tu. Kwa mfano sasa hivi Rais anateua mwenyekiti wa bodi na mawaziri wanateua wajumbe wa bodi! Kwanini RAis hateusi wote kwa mpigo? Lakini kwenye Katiba Rais anateua mwenyekiti na Katibu na wajumbe 116!! Rais ndiye anaiitisha Bunge la Katiba na kazi yote mwisho inamrudia yeye kwa maamuzi. Really?
Bado una circumlocute!.... be straight na utuambie utaivunjaje katiba iliyopo na kuweka katiba mpya, bila kuwa na sheria inayoonyesha utaratibu wa kuipata hiyo katiba mpya.
Naomba pia utujulishe kwanini President (a major part of bunge) asiwe kewnye hiyo equation.Kama awepo, role yake iwe ni ipi?
 
Mzee Mwanakijiji,
Mimi niliwahi kusikia viongozi tena wanasiasa wakisema wananchi wengi hawaifahamu Katiba, wakahoji ni wangapi huisoma na kadhalika kumbe viongozi karibu wote hawafahamu hata Umuhimu wa katiba na hasa inapokuwa MPYA...sasa naanza kuelewa kwa nini wana CCM hawakuona makosa ktk katiba ya mwanzo wala hawaoni umuhimu wa katiba mpya. Hata Jumuiya tu za watu katiba haifanyiwi mchakato na kwa maamuzi ya mwenyekiti (mtu mmoja).. role yake hukabidhiwa na wanachama kama watakavyokabidhiwa wengine...lakini bado watu hawaelewi.

Pengine JK anachozungumzia ni kufanya marekebisho makubwa sana ya katiba iliyopo na sii kuunda katiba mpya. Labda wale mnaokubaliana na JK mnaweza kutuambia hiyo tume ya rais itakusanya vipi mawazo ya wananchi? Hiyo tume itaifanya kazi vipi hadi wananchi waridhike ikiwa tume haijui wananchi wanataka kipi?

Maanake rahisi mtu kuuliza ni wananchi au wanaharakati wangapi hawakuhusishwa, wakati mtu huyo huyo anajua fika kwamba hata yeye mwenyewe hajahusishwa na wala hana mtu hata mmoja anayemjua kahusishwa mbali na wabunge na viongozi lakini anauliza kutaka hesabu ya wananchi ambao hawajahusishwa..Kwa yaliyopitishwa bungeni wewe umehusishwa vipi?
 
Mkuu ninavyoelewa kuna mwanataaluma mmoja amependekeza raisi apelekewe majina ya wanataaluma, wanaharakati, etc (watu kutoka makundi ya kijamii) ambao wameteuliwa na wananchi. Watu hao au majina hayo yatakayopelekwa kwake yeye atachagua kamati kutoka kwenye hayo majina. In other words, wananchi hatutaki kamati iliyoteuliwa na Kikwete/CCM bali wanakamati wapendekezwe na jamii/wananchi na yeye atachagua katika kundi hilo i.e. atatoa short list wa watu wa kamati kutoka kundi hilo. Raisi hawezi kuchagua kamati yeye,(kupendekeza watu wake) kwasababu him and his part tayari watakuwa na influence interest zao kwenye katiba. Watanzania wanataka watu neutral watakaowakilisha mapendekezo yao. Kwa mtizamo wangu raisi anaelewa kabisa wasomi/watanzania wanaolalamika wanataka nini, lakini anatumia ujinga wa watanzania wengi wakutokuelewa kama mtaji wake wakujichukulia madaraka mikonono na hii ni hatari sana.

Hao watu wanaopelekwa kwa rais ili awachague watapatikana kwa utaratibu upi??

Je wasipokubaliana (which is obvious) kila kikundi cha watu kikata kipate zaidi ???

Kwa utaratibu huo wala huwezi kupata katiba mpya (forget it) kila siku kutakuwa na mijadala ya nani aingie na kwanini??
 
Mkuu ninavyoelewa kuna mwanataaluma mmoja amependekeza raisi apelekewe majina ya wanataaluma, wanaharakati, etc (watu kutoka makundi ya kijamii) ambao wameteuliwa na wananchi. Watu hao au majina hayo yatakayopelekwa kwake yeye atachagua kamati kutoka kwenye hayo majina. In other words, wananchi hatutaki kamati iliyoteuliwa na Kikwete/CCM bali wanakamati wapendekezwe na jamii/wananchi na yeye atachagua katika kundi hilo i.e. atatoa short list wa watu wa kamati kutoka kundi hilo. Raisi hawezi kuchagua kamati yeye,(kupendekeza watu wake) kwasababu him and his part tayari watakuwa na influence interest zao kwenye katiba. Watanzania wanataka watu neutral watakaowakilisha mapendekezo yao. Kwa mtizamo wangu raisi anaelewa kabisa wasomi/watanzania wanaolalamika wanataka nini, lakini anatumia ujinga wa watanzania wengi wakutokuelewa kama mtaji wake wakujichukulia madaraka mikonono na hii ni hatari sana.
Babu yangu Ikwiriri atamchagua nani?...
Hebu niambie mtanzania wa kawaida atamchaguaje mtu wa kumuwakilisha wenye tume. Atumie criterion gani?
 
Yaani hapa sioni haja ya kutoka jasho.
Rais akiandika sheria inayomuwezesha kuingia nyumbani kwako muda wowote, na bunge likapitisha, na mahakama kuu ikahalalisha constitutionality ya hiyo sheria.... basi mkuu hutakuwa na jinsi.
Unanikumbusha US History 205 (pre civil war US history) ambapo waingereza waliandika Quartering act, 1764 inayoruhusu askari wa uingereza kuingia nyumba yeyote ile na kupata mkogo na usingizi wa pono chumba chochote anachohitaji.... na Parliament ya UK ikapitisha.
Once yo have the legislature(more than two thirds), you can be a dictator, easily!

Ajaribu basi kuandika hiyo sheria auone mziki wake!
 
Mzee Mwanakijiji,
Mimi niliwahi kusikia viongozi tena wanasiasa wakisema wananchi wengi hawaifahamu Katiba, wakahoji ni wangapi huisoma na kadhalika kumbe viongozi karibu wote hawafahamu hata Umuhimu wa katiba na hasa inapokuwa MPYA...sasa naanza kuelewa kwa nini wana CCM hawakuona makosa ktk katiba ya mwanzo wala hawaoni umuhimu wa katiba mpya. Hata Jumuiya tu za watu katiba haifanyiwi mchakato na kwa maamuzi ya mwenyekiti (mtu mmoja).. role yake hukabidhiwa na wanachama kama watakavyokabidhiwa wengine...lakini bado watu hawaelewi.

Pengine JK anachozungumzia ni kufanya marekebisho makubwa sana ya katiba iliyopo na sii kuunda katiba mpya. Labda wale mnaokubaliana na JK mnaweza kutuambia hiyo tume ya rais itakusanya vipi mawazo ya wananchi? Hiyo tume itaifanya kazi vipi hadi wananchi waridhike ikiwa tume haijui wananchi wanataka kipi?

Maanake rahisi mtu kuuliza ni wananchi au wanaharakati wangapi hawakuhusishwa, wakati mtu huyo huyo anajua fika kwamba hata yeye mwenyewe hajahusishwa na wala hana mtu hata mmoja anayemjua kahusishwa mbali na wabunge na viongozi lakini anauliza kutaka hesabu ya wananchi ambao hawajahusishwa..
Katiba ya marekani imeandikwa na watu wawili tu.
 
MwDashi1, Mzee Mwanakijiji, mie naona hata hadhira Rais anayotumia kutueleza mabo mazito (Wana CCM wa Dsm) HAIFAI. Kusoma hotuba zilizoandikwa na Salva na Makamba mdogo haUBUNIFU wa Rais. Kwanini asiitishe Mkutano wa Waandishi wa Habari na kujibu maswali yao?
 
Alipotoa hotuba ya kufunga mwaka jana,Kikwete alisema vizuri sana kuhusu katiba mpya na uandikwaji wake.Alistahili pongezi hata kutoka kwa Mbowe kwani hilo ndilo limekuwa hitaji kubwa kwa taifa kwa sasa ili lipige hatua.Raisi amegeuka.Anasema hafanyi kitu kipya.Anarudia walichowahi kufanya watangulizi wake.Hana mpango na katiba mpya,anaendeleza viraka.Ama hakueleweka mwanzoni au amebadili mawazo katikati ama ameamua tu kudanganya na kukana.Analazimisha aeleweke kama anavotaka yeye sio kama anavyotamka.Kumbeza Mbowe kwamba mwanzo alimpongeza na sasa anapinga mchakato wa katiba ni kutufanya wote wajinga.Ile nia aliyoionyesha siku ya kufunga mwaka haiakisi kinachoendelea kwenye mchakato wa katiba.Lakini yeye anataka aendelee kupongezwa!Ni bora hata Kombani aliyewahi kusema katiba mpya sio kipaumbele cha serikali ambayo yeye ni waziri wake wa katiba!Watu tukamwona alienda kinyume na raisi wake kumbe tu mmoja wao ni fundi wa kubadili maneno ili atimize anachokitaka.
 
Sasa hapo ndiyo tuseme unakubaliana na mchakato unaopendekezwa
Labda nikusaidie tu ya kwamba wazo linaweza kutoka kwa mtu mmoja na katiba ikaandikwa na mtu mmoja lakini mchakato wa kuunda katiba lazima uhusishe wananchi wote kulingana na mazingira mliyopo.. Labda soma mchakato wa katiba ya Marekani (ingawa sipendi sana kuiga) na kisha nambie nafasi ya rais wao. Bofya
 
Mkuu ninavyoelewa kuna mwanataaluma mmoja amependekeza raisi apelekewe majina ya wanataaluma, wanaharakati, etc (watu kutoka makundi ya kijamii) ambao wameteuliwa na wananchi. Watu hao au majina hayo yatakayopelekwa kwake yeye atachagua kamati kutoka kwenye hayo majina. In other words, wananchi hatutaki kamati iliyoteuliwa na Kikwete/CCM bali wanakamati wapendekezwe na jamii/wananchi na yeye atachagua katika kundi hilo i.e. atatoa short list wa watu wa kamati kutoka kundi hilo. Raisi hawezi kuchagua kamati yeye,(kupendekeza watu wake) kwasababu him and his part tayari watakuwa na influence interest zao kwenye katiba. Watanzania wanataka watu neutral watakaowakilisha mapendekezo yao. Kwa mtizamo wangu raisi anaelewa kabisa wasomi/watanzania wanaolalamika wanataka nini, lakini anatumia ujinga wa watanzania wengi wakutokuelewa kama mtaji wake wakujichukulia madaraka mikonono na hii ni hatari sana.

kama mlikuwa na mawazo mazuri kama haya kwa nini mlisusa kuyapeleka kunakohusika?sasa ona sheria imeshapita ndo mnakurupuka kuanza kutoa maoni. me napata shida sana kuelewa ni kwa nini wabunge wa cdm na nccr mageuzi waliamua kuwasaliti watanzania wenzao kwa kususa mjadala?may be things could be different tunapojadili hili suala leo hii. kwa nini wasingeshiriki kuwakilisha maoni yetu then yakataliwe ndio tuanze kufikiri nini cha kufanya?why???????
 
Najiuliza kila mara; HIVI NI KWANINI TZ & VIONGOZI WAKE NI VIGUMU SANA KUIGA MEMA?

1) Angalia sheria za usimamizi na mgawanyo wa rasilimali hasa ardhi, madini, mali-asili na nishati
2) Angalia sheria na sera za elimu toka msingi mpaka vyuo
3) Angalia mgawanyo wa mihimili ya dola na umuhimu wake kwa Tz kama taifa k.m. kisheria, kijamii & kisiasa
4) Angalia sera na sheria za uchumi & fedha
5) Hili la mchakato wa katiba mpya na ukilaza wa bunge la makinda (ccm) vinatia kinyaa
6) nk

Hitimisho huwa: HUWA WANA UWEZO WA KUIGA (na kutunga) MABAYA.
So at least they're capable of something just as 50 yrs since independence bore witness.
 
Jamani heeeee mnakuwa kama hamuelewi kwani CCM si ni kundi la washikaji waliolifikisha taifa hili mahali lilipo sasa kwenye umasikini wa kutupwa!!!!!!!!!! Wanacho ngangania kufanya ni kuweka mfumo wa kujilinda pamoja na vizazi vyao waendelee kuibia taifa hili, sijui tumewakosea nini maskini na watoto wao wamekuwa wezi wakubwa!!!!!!!!!! Wanataka mfumo wa kuwalinda waendelee kutuburuza, watu waambiwe waelimishwe wajue hawa jamaa ni wezi wa rasilimali zetu wanafilisi nchi hawana mpango wa kusaidia chochote!!!!!!!!!!!!!Tuingoje kwenye kura za maoni tuipige chini ili tupate katiba itakayo kuwa na maadilimeme kwa taifa letu!!!!!!!!!! Hawawezi kujinyonga ni ngumu tutumie akili ya ziada!!!!

Mkuu naona unajichanganya tu, mwanzoni umesema inaundwa katiba itakayowalinda wao, halafu unasema tuipige chini hiyo kwenye kura za maoni. Wao wakiamua ndivyo itakavyokuwa, wakitaka ipite itapita, wakitaka isipite haitapita.

Na kama wengi wetu hatujui ni kuwa CCM hawatoki madarakani kwa namna yoyote ile, hiyo ndio dhamira yao na sababu wanazo, tena za msingi tu kwao.

CCM wamejiandaa kwa lolote hilo lazima tulijue, kuchekeana nao kama Mbowe alivyompa sifa Rais kwa kuanzisha mchakato ni kutokuwakujua CCM ni akina nani. Kuna principle moja tu nnaifahamu mimi inatumika duniani, and do not get me wrong sina nia mbaya, ila wananchi wa nchi zilizokuwa zinagandamizwa hawakufanikiwa kwa kuwaomba watawala wabadilke au kwa michakato ya katiba.

They went into the streets na kudai haki zao na damu ilimwagika, hapo ndipo mataifa makubwa yalipostuka na kuingilia kati na ndipo mambo yakabadilika. Tumeona Kenya na sasa nchi za kiarabu. Ila watanzania tunaweza kutake route ambayo si ya kihistoria na kufanikiwa, you never know. Mbele yetu naona giza tu, hii ni mpaka wajukuu zetu watatawaliwa na CCM ya wajukuu wa akina Nape.
 
Back
Top Bottom