Kwa nini Rais analazimisha kitu ambacho hana madaraka nacho ya Kikatiba? (Video)

Hayo mashangilio ni "tune" au ni wazee wanashangilia? Mimi sioni watu wanashangilia kiasi ya kelele zinazosikika
 
Katika kufanikisha mchakato wa Katiba mpya, swala lililokuwa muhimu lilikuwa ni kufanyia marekebisho katika Katiba ya zamani.
Ambayo yangempunguzia na kumuondolea madaraka Rais ya kuteuwa tume ya Katiba, pamoja na kuundwa kwa tume huru
ya uchaguzi. Ikiwa marekebisho hayo yamegomewa katukatu na Serikali ya Ccm, ina maana hakuna haja ya kutunga Katiba
mpya chini ya madaraka makubwa aliyokuwanayo Rais ambapo ataifanya Katiba ya kiccm zaidi ya kujilinda wenyewe na kulinda
maovu yao. Kinachotakiwa ni Wananchi wenyewe watunge Katiba wanayoitaka. Katiba tuliyonayo ni ya mfumo wa chama
kimoja, na ndio maana inahitajika kufanyiwa marekebisho kwanza kabla ya mchakato wa kuunda Katiba mpya kuanza.
Kwenye mfumo wa vyama vingi inahitajika hivyo. Kikwete kukanusha kama wewe sio Dikteta kitu hicho hakiwezekani, kwa
sababu ya ubovu wa Katiba tuliyonayo imeshakutia wewe katika hatia na kuingia katika mfumo wa Kidikteta.
 
Hayo mashangilio ni "tune" au ni wazee wanashangilia? Mimi sioni watu wanashangilia kiasi ya kelele zinazosikika

Unajua unapochaugua kuongelea masuala mazito kwa kuyatoa kama taarifa ambazo unaamini haziingii akilini kwa wepesi lazima uchague na audience itakayoweza kuvumilia huo upuuzi, na mkuu wa kaya analijua hilo kuliko vingine vyote nadhani!
Ndio maana hata kwenye kujibu madai ya walimu na mgomo waliotangaza mwaka jana nadhani, alipokataa kura za wafanyakazi, aliwaita hawa wanaotambuliwa kama 'wazee wa daresalama!'
Nina mashaka na vigezo wanavyotumia katika 'kuwachagua' kwa kuwa wamekuwa ni wepesi sana kupiga makofi kuliko hata kusikiliza, hadi unajiuliza hivi wanasikiliza kweli au wanafurahi kumuona mkuu wa kaya karibu yao!
 
mwanakijiji, i am sorry to say you are wrong. kama umemsikiliza vizuri jk leo amekuwa akinukuu katiba hii iliyopo ambayo ina mpa mamlaka ya kuunda Tume ya katiba.

Kwa hiyo kama aliyowahi kusema mnyika huko nyuma kilichotakiwa kufanywa bungeni ni kufanya mabadiliko ya katiba iliyopo sasa na kuigiza kipengele kitachowapa rasmi mamlaka kamili wananchi ya kuunda katiba yao wenyewe bila kuingiliwa na mamlaka yeyote kwahiyo mabadiliko ya katiba nchi hii hayawezekani kwa utaratibu uliopo inatubidi tuingie mtaani kudai haki ya kuamua namna nchi yetu itakavyotawaliwa.

We have to fight back otherwise forget about having the constitution with political and legal legitimacy.
Ndg zangu kitu kilichopo kwa sasa ni kuwahamasisha wananchi wajue kwa nini tunahitaji katiba mpya wala si malekebisho ya katiba!!!!!!! Watu wajue hata wizi wa mchana unaofanywa na CCMna wadau wao ni udhaifu wa katiba iliyopo!!!!!!!!Haiwezekani hawa CCM na mafisadi wake wakajitia kitanzi kwa kuunda katiba makini itakayo peleka wizi woote jela, pamoja na watoto wao!!!!!!!!Lazima wananchi wafanye maamuzi magumu, mbona Kenya walikataa katiba ya kubambikizwa na wakapata katiba mpya after a long struggle ????? Tuikatae hiyo mipango ya katiba ya kubambikizwa na kulinda wezi period!!!!!!!!!!Kuburuzwa ki hivyo haikubaliki!!!!!!!!!
 
Bunge la CCM bila aibu tena kwa ushabiki mkubwa kichama sheria batili ya Makinda inayojitia bingwa kupingana na katiba yetu:

1. Kwa kujiandaa kufunga Wa-Tanzania jela miaka mitatu eti kwa kupinga KATIBA YA KIKWETE na kwamba wala tusiwaze kutumia mamlaka yetu wenyewe kujadili, kupinga na kuunda katiba ya wananchi wenyewe? (The Doctrine of Ultraires)

2. Sheria inayotafuta kutugawa kimatabaka kwa maana kwamba KATIBA YA KIKWETE itapata kuundwa na hata kukosolewa tu na matajiri peke yao nchini ambao ndio wenye uwezo wa kukwepa kwenda jela Ukonga kwa kulipa faini ya milioni moja. (Malice)

3. Sheria iliotungwa sirini kwa maswahiba wachache kualikana wenyewe kwenye mijengo ya kifahari sehemu za mijini tu (Dar es Salaam, Dodoma na Zanzibar) KWA MWALIKO MAALUM ilhali wenye nchi kwa asilimia zetu zaidi ya 80 vijijini tukifungiwa milango nje. (Selective)

...
Jamani heeeee mnakuwa kama hamuelewi kwani CCM si ni kundi la washikaji waliolifikisha taifa hili mahali lilipo sasa kwenye umasikini wa kutupwa!!!!!!!!!! Wanacho ngangania kufanya ni kuweka mfumo wa kujilinda pamoja na vizazi vyao waendelee kuibia taifa hili, sijui tumewakosea nini maskini na watoto wao wamekuwa wezi wakubwa!!!!!!!!!! Wanataka mfumo wa kuwalinda waendelee kutuburuza, watu waambiwe waelimishwe wajue hawa jamaa ni wezi wa rasilimali zetu wanafilisi nchi hawana mpango wa kusaidia chochote!!!!!!!!!!!!!Tuingoje kwenye kura za maoni tuipige chini ili tupate katiba itakayo kuwa na maadilimeme kwa taifa letu!!!!!!!!!! Hawawezi kujinyonga ni ngumu tutumie akili ya ziada!!!!

 
Tume zote zizowahi kuundwa ili kukusanya maoni ya wananchi na hatimaye kufikia kufanyiwa marekebisho ya katiba ndiyo yaliyotufikisha hapa tulipo. Rais haaminiki kwa sababu watangulizi wake ambao walikuwa wenyeviti wa CCM hawakufanya marekebisho ya katiba kwa kufuata maoni ya wananchi. Je kwa mantiki hiyo tutawezaje kumwamini rais wa sasa ambaye ni mwenyekiti wa Chama kisichotaka mabadiliko kuwa atazingatia maoni ya wananchi katika kuandika katiba mpya? Kwa mtazamo wangu kinachofanyika sasa na kitakachofanyika ni kurejea yaleyale ya tume zilizopita
 
Tanzania tunachohitaji ni KATIBA MPYA! Katiba tuliyonayo imepitwa na wakati kwa kuwa ilitengenezwa wakati wa uhuru mwaka 1961. Katiba hiyo imekuwa ikifanyiwa mabadiliko (amendments) kuleta Jamhuri mwaka 1962, Muungano mwaka 1964, Chama kimoja mwaka 1965, Azimio la Arusha mwaka 1967 na chama kushika hatamu, vyama vingi 1992 n.k. Sasa imefika wakati katiba hii haifai tena, tunahitaji katiba mpya. Na katiba ni mali ya watanzania, si mali ya CCM, Kikwete, Kombani, Lusinde, Kilango wala Makinda. Kutunyima watanzania haki yetu ya kimsingi ya kuijadili katiba mpya iweje na hatimaye kuikubali ni kututukana. Hivi kwa kuchaguliwa kwao kuwa wabunge ndiyo kumewafanya wao kuwa wana akili kuliko watanzania zaidi ya milioni 43? Watanzania lazima tuamue, vinginevyo kuna watu wachache wanaotaka kulinda maslahi yao ambao wanateka mfumo mzima na wataendelea kufanya hivyo. Aliyeshiba hamjui mwenye njaa. Nakumbuka maneno ya binti mfalme Marie-Antoinette alipomuuliza mama yake, "Kwa nini watu wanaandamana, mama yake akajibu kwa kuwa hawana mkate. Binti mfalme akauliza kwa nini wasile keki?" Hapo wote waliokaa bungeni kujadili muswada wa katiba ndio kina Marie-Antoinette. Mpaka leo hawafahamu kwa nini tunaandamana!
 
Mkuu uko sahihi sana..hatuhitaji katiba ya KIKWETE wala ya CCM kwani katiba hiyo ndiyo iliyotufikisha hapa...nchi hii ni ya watanzania,siyo ya CHADEMA,CUF,NCCR wala CCM sasa imefika wakati watanzania waamue jinsi wanavyotaka taifa lao kuongozwa..Tume itakayoundwa na KIKWETE itakuwa ya watu wale wale na matokeo ya tume hiyo hata wananchi watoe maoni gani hatima ni ile ile...Katiba ya Kifisadi na chama kimoja,kama kweli watanzania sote tungeelewa umuhimu wa katiba katika maendeleo ya Taifa letu,tungesahau habari ya mimi CCM mimi CHADEMA na tungesimama pamoja kudai katiba ya tanzania itakayosimamia haki,usawa kwa raia wote..Chama kitakachoshinda uchaguzi kitatuongoza kwa kuifuata katiba hiyo..siyo Chama tawala kitengeneze katiba inayowawezesha wao kufanya watakalo

Tanzania tunachohitaji ni KATIBA MPYA! Katiba tuliyonayo imepitwa na wakati kwa kuwa ilitengenezwa wakati wa uhuru mwaka 1961. Katiba hiyo imekuwa ikifanyiwa mabadiliko (amendments) kuleta Jamhuri mwaka 1962, Muungano mwaka 1964, Chama kimoja mwaka 1965, Azimio la Arusha mwaka 1967 na chama kushika hatamu, vyama vingi 1992 n.k. Sasa imefika wakati katiba hii haifai tena, tunahitaji katiba mpya. Na katiba ni mali ya watanzania, si mali ya CCM, Kikwete, Kombani, Lusinde, Kilango wala Makinda. Kutunyima watanzania haki yetu ya kimsingi ya kuijadili katiba mpya iweje na hatimaye kuikubali ni kututukana. Hivi kwa kuchaguliwa kwao kuwa wabunge ndiyo kumewafanya wao kuwa wana akili kuliko watanzania zaidi ya milioni 43? Watanzania lazima tuamue, vinginevyo kuna watu wachache wanaotaka kulinda maslahi yao ambao wanateka mfumo mzima na wataendelea kufanya hivyo. Aliyeshiba hamjui mwenye njaa. Nakumbuka maneno ya binti mfalme Marie-Antoinette alipomuuliza mama yake, "Kwa nini watu wanaandamana, mama yake akajibu kwa kuwa hawana mkate. Binti mfalme akauliza kwa nini wasile keki?" Hapo wote waliokaa bungeni kujadili muswada wa katiba ndio kina Marie-Antoinette. Mpaka leo hawafahamu kwa nini tunaandamana!
 
Mkuu uko sahihi sana..hatuhitaji katiba ya KIKWETE wala ya CCM kwani katiba hiyo ndiyo iliyotufikisha hapa...nchi hii ni ya watanzania,siyo ya CHADEMA,CUF,NCCR wala CCM sasa imefika wakati watanzania waamue jinsi wanavyotaka taifa lao kuongozwa..Tume itakayoundwa na KIKWETE itakuwa ya watu wale wale na matokeo ya tume hiyo hata wananchi watoe maoni gani hatima ni ile ile...Katiba ya Kifisadi na chama kimoja,kama kweli watanzania sote tungeelewa umuhimu wa katiba katika maendeleo ya Taifa letu,tungesahau habari ya mimi CCM mimi CHADEMA na tungesimama pamoja kudai katiba ya tanzania itakayosimamia haki,usawa kwa raia wote..Chama kitakachoshinda uchaguzi kitatuongoza kwa kuifuata katiba hiyo..siyo Chama tawala kitengeneze katiba inayowawezesha wao kufanya watakalo

Hiyo katiba mpya itaundwajwe bila ya Rais?? yaani utaratibu uweje labda tusaidiana hapa maana mimi nashindwa kuwaelewa wengi wenu???
 
Unajua unapochaugua kuongelea masuala mazito kwa kuyatoa kama taarifa ambazo unaamini haziingii akilini kwa wepesi lazima uchague na audience itakayoweza kuvumilia huo upuuzi, na mkuu wa kaya analijua hilo kuliko vingine vyote nadhani!
Ndio maana hata kwenye kujibu madai ya walimu na mgomo waliotangaza mwaka jana nadhani, alipokataa kura za wafanyakazi, aliwaita hawa wanaotambuliwa kama 'wazee wa daresalama!'
Nina mashaka na vigezo wanavyotumia katika 'kuwachagua' kwa kuwa wamekuwa ni wepesi sana kupiga makofi kuliko hata kusikiliza, hadi unajiuliza hivi wanasikiliza kweli au wanafurahi kumuona mkuu wa kaya karibu yao!

Angalia hiyo VIDEO kwa makini, mashangilio yanayosikika hayatoki kwa wanamsikiliza; wengi wamekaa kimya kama wamenyeshewa na mvua
 
Hiyo katiba mpya itaundwajwe bila ya Rais?? yaani utaratibu uweje labda tusaidiana hapa maana mimi nashindwa kuwaelewa wengi wenu???

Rais yupo, lakini asiwe na sehemu yoyote katika kuunda katiba mpya. Pamoja na mapungufu mengi ya katiba ya sasa, kuna suala la mamlaka makubwa sana aliyopewa Rais. Ikumbukwe ya kwamba katiba hii ni ya zamani. Kuna wakati ilikuwa ni busara kumpa Rais mamlaka makubwa. Sivyo hali ilivyo sasa, hasa kwa kuwa tuko kwenye mfumo wa vyama vingi.

Mfano mmojawapo ninaweza kuutoa kwa haraka ni pale Ikulu panapofanyika vikao vya kamati kuu ya ccm. Wakayti wa Mwalimu, chama na serikali vilikuwa 'almost' kitu kimoja. Mkuu wa Mkoa alikuwa ndiye Katibu wa CCM wa mkoa. Mwenyekiti wa CCM alikuwa ndiye Rais. Hapakuwa na mwenye kuuliza swali. Kwa mantiki hiyo, Rais ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa CCM, chama pekee cha Tanzania ya wakati ule, na ambacho kilikuwa kikatiba kimeshika hatamu alikuwa anazo kofia zake mbili 'intertwined'. Aliweza kuitisha kikao cha kamati kuu ya CCM Ikulu. Lakini hata hivyo Mwalimu kwa miaka yote alipokuwa ana kofia zake mbili hakufanya hivyo! Vikao vya CCM vilifanyika Makao Makuu ya CCM Dodoma ama ofisi ndogo ya CCM Lumumba. Ikulu ni mahali pa vikao vya baraza la mawaziri ambayo ni serikali. Ndivyo ilivyo kwenye nchi zinazofuata mfumo wa vyama vingi. Huwezi kuona kikao cha Democratic Party Marekani kinafanyika White House!

Katiba imefanyiwa mabadiliko 'amendments' na kusema nchi yetu ni nchi ya vyama vingi. Sasa kwa nini bado jk na serikali yake wanaendelea kufanya kazi katika dhana ya enzi za chama kimoja? Ndani ya mfumo wa sasa ni kosa kwa Rais kufanya vikao vya kichama kwenye ofisi ya serikali. Hapo kunakuja kitu kinachoitwa kwa kiingereza 'conflict of interests' samahani sijui nitumie neno gani kwa kiswahili kuelezea dhana hiyo.

Sasa huo ni mfano mmoja tu, lakini jk kutokana na mapungufu ya katiba ya sasa amekuwa akifanya mambo mengi ambayo ni dhahiri hatakiwi kufanya, ila analindwa na katiba ambayo imepitwa na wakati. Tunapotaka kufanya mabadiliko ambayo yatapunguza mamlaka yake, yeye hapaswi kuwa sehemu ya mchakato huo. Hii ni pamoja na kuteua tume ya watakaokaa na kutunga muswada kamili. Kumwacha jk awemo kwenye mchakato huo ni kujidanganya ya kuwa atachagua watu ambao watakuwa na mtazamo tofauti na wake. Wewe umeona wapi hakimu anashitakiwa mahakamani kwa kosa la jinai halafu yeye ndiye anayepewa mamlaka ya kuchagua mwendesha mashitaka, hakimu na wazee wa mahakama?
 
Rais yupo, lakini asiwe na sehemu yoyote katika kuunda katiba mpya. Pamoja na mapungufu mengi ya katiba ya sasa, kuna suala la mamlaka makubwa sana aliyopewa Rais. Ikumbukwe ya kwamba katiba hii ni ya zamani. Kuna wakati ilikuwa ni busara kumpa Rais mamlaka makubwa. Sivyo hali ilivyo sasa, hasa kwa kuwa tuko kwenye mfumo wa vyama vingi.

Mfano mmojawapo ninaweza kuutoa kwa haraka ni pale Ikulu panapofanyika vikao vya kamati kuu ya ccm. Wakayti wa Mwalimu, chama na serikali vilikuwa 'almost' kitu kimoja. Mkuu wa Mkoa alikuwa ndiye Katibu wa CCM wa mkoa. Mwenyekiti wa CCM alikuwa ndiye Rais. Hapakuwa na mwenye kuuliza swali. Kwa mantiki hiyo, Rais ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa CCM, chama pekee cha Tanzania ya wakati ule, na ambacho kilikuwa kikatiba kimeshika hatamu alikuwa anazo kofia zake mbili 'intertwined'. Aliweza kuitisha kikao cha kamati kuu ya CCM Ikulu. Lakini hata hivyo Mwalimu kwa miaka yote alipokuwa ana kofia zake mbili hakufanya hivyo! Vikao vya CCM vilifanyika Makao Makuu ya CCM Dodoma ama ofisi ndogo ya CCM Lumumba. Ikulu ni mahali pa vikao vya baraza la mawaziri ambayo ni serikali. Ndivyo ilivyo kwenye nchi zinazofuata mfumo wa vyama vingi. Huwezi kuona kikao cha Democratic Party Marekani kinafanyika White House!

Katiba imefanyiwa mabadiliko 'amendments' na kusema nchi yetu ni nchi ya vyama vingi. Sasa kwa nini bado jk na serikali yake wanaendelea kufanya kazi katika dhana ya enzi za chama kimoja? Ndani ya mfumo wa sasa ni kosa kwa Rais kufanya vikao vya kichama kwenye ofisi ya serikali. Hapo kunakuja kitu kinachoitwa kwa kiingereza 'conflict of interests' samahani sijui nitumie neno gani kwa kiswahili kuelezea dhana hiyo.

Sasa huo ni mfano mmoja tu, lakini jk kutokana na mapungufu ya katiba ya sasa amekuwa akifanya mambo mengi ambayo ni dhahiri hatakiwi kufanya, ila analindwa na katiba ambayo imepitwa na wakati. Tunapotaka kufanya mabadiliko ambayo yatapunguza mamlaka yake, yeye hapaswi kuwa sehemu ya mchakato huo. Hii ni pamoja na kuteua tume ya watakaokaa na kutunga muswada kamili. Kumwacha jk awemo kwenye mchakato huo ni kujidanganya ya kuwa atachagua watu ambao watakuwa na mtazamo tofauti na wake. Wewe umeona wapi hakimu anashitakiwa mahakamani kwa kosa la jinai halafu yeye ndiye anayepewa mamlaka ya kuchagua mwendesha mashitaka, hakimu na wazee wa mahakama?

Maelezo yako mengi sawa...lakini hujajibu swali??

Ili tupate katiba mpya tufuate utaratibu upi??

Na huo utaratibu ambao ofisi ya rais haitahusika???

NONE
 
Rais yupo, lakini asiwe na sehemu yoyote katika kuunda katiba mpya. Pamoja na mapungufu mengi ya katiba ya sasa, kuna suala la mamlaka makubwa sana aliyopewa Rais. Ikumbukwe ya kwamba katiba hii ni ya zamani. Kuna wakati ilikuwa ni busara kumpa Rais mamlaka makubwa. Sivyo hali ilivyo sasa, hasa kwa kuwa tuko kwenye mfumo wa vyama vingi.

Mfano mmojawapo ninaweza kuutoa kwa haraka ni pale Ikulu panapofanyika vikao vya kamati kuu ya ccm. Wakayti wa Mwalimu, chama na serikali vilikuwa 'almost' kitu kimoja. Mkuu wa Mkoa alikuwa ndiye Katibu wa CCM wa mkoa. Mwenyekiti wa CCM alikuwa ndiye Rais. Hapakuwa na mwenye kuuliza swali. Kwa mantiki hiyo, Rais ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa CCM, chama pekee cha Tanzania ya wakati ule, na ambacho kilikuwa kikatiba kimeshika hatamu alikuwa anazo kofia zake mbili 'intertwined'. Aliweza kuitisha kikao cha kamati kuu ya CCM Ikulu. Lakini hata hivyo Mwalimu kwa miaka yote alipokuwa ana kofia zake mbili hakufanya hivyo! Vikao vya CCM vilifanyika Makao Makuu ya CCM Dodoma ama ofisi ndogo ya CCM Lumumba. Ikulu ni mahali pa vikao vya baraza la mawaziri ambayo ni serikali. Ndivyo ilivyo kwenye nchi zinazofuata mfumo wa vyama vingi. Huwezi kuona kikao cha Democratic Party Marekani kinafanyika White House!

Katiba imefanyiwa mabadiliko 'amendments' na kusema nchi yetu ni nchi ya vyama vingi. Sasa kwa nini bado jk na serikali yake wanaendelea kufanya kazi katika dhana ya enzi za chama kimoja? Ndani ya mfumo wa sasa ni kosa kwa Rais kufanya vikao vya kichama kwenye ofisi ya serikali. Hapo kunakuja kitu kinachoitwa kwa kiingereza 'conflict of interests' samahani sijui nitumie neno gani kwa kiswahili kuelezea dhana hiyo.

Sasa huo ni mfano mmoja tu, lakini jk kutokana na mapungufu ya katiba ya sasa amekuwa akifanya mambo mengi ambayo ni dhahiri hatakiwi kufanya, ila analindwa na katiba ambayo imepitwa na wakati. Tunapotaka kufanya mabadiliko ambayo yatapunguza mamlaka yake, yeye hapaswi kuwa sehemu ya mchakato huo. Hii ni pamoja na kuteua tume ya watakaokaa na kutunga muswada kamili. Kumwacha jk awemo kwenye mchakato huo ni kujidanganya ya kuwa atachagua watu ambao watakuwa na mtazamo tofauti na wake. Wewe umeona wapi hakimu anashitakiwa mahakamani kwa kosa la jinai halafu yeye ndiye anayepewa mamlaka ya kuchagua mwendesha mashitaka, hakimu na wazee wa mahakama?
Sasa huu ndiyo mfano gani?
Rais akitaka anaweza kulisha watu pilau ikulu kila siku, hiyo ni protocol issue ambayo haihusiki na katiba.
 
Pipijojo, kama hujui sheria kama mie hapa, kukaa chini na kuwasikia wataalam siyo dhambi.

Ona sasa unavyojidhihirisha ulivyo mweupe.SOBY, MM Mwanakijiji, JMushi1 na wengine, nimeupenda mjadala wenu zaidi ya hotuba.

Endeleeni kutufungua macho wengine. Naona ngoma bado mbichi sana.

Nimelipenda swali la "Maadamu Kikwete na CCM wana kila kitu, kwa nini hawajaandika wao peke yao katiba......?"
Kwenye mvutano huu,sijui ni kwa vipi katiba ya wananchi itapatikana...Given how serous the issue is to both sides.

And mostly the poeple's side...

Kwa upande mwingine,hata wakikubaliana,sidhani kama JK atakubali kuwepo na kipengele cha uwajibishwaji kwa marais waliostaafu endapo kuna ushahidi kuwa walihujumu taifa.
 
Kinachoitwa mamlaka ya Kikatiba hakitolewi kwenye sheria kinatolewa kwenye Katiba. Sheria hii iliyopitishwa ilitakiwa kwanza kufanyia marekebisho Katiba iliyopo sasa (na iridhiwe na BLW Zanzibar) halafu ndio kutoka hapo tunaweza kuzungumza mengine. Sheria hii imetoa madaraka kwa rais ambayo hana Kikatiba. Rais hana madaraka ya kuanzisha mchakato wa kuandika Katiba Mpya ya nchi. Period. Wengi wamekuwa wakijenga hoja ati kwa vile yeye ni Rais basi hayo madaraka yako inherent ndani ya ofisi yake. Hii si kweli. Je Rais ana madaraka ya kuanzisha cheo cha Makamu wa pili wa Rais wa Jamhuri ya Muungano? Wengine wanaweza kusema "ndiyo anayo" kwa sababu yeye ni Rais ukweli ni kuwa hana kwa sababu RAIS ANAYO MADARAKA YALE TU AMBAYO AMEPEWA KWENYE KATIBA.

Labda watu wamesahau tu; Disemba 31 mwaka jana Rais Kikwete alisema hivi akitoa ahadi ya Tume (msisitizo mweusi na mistari wangu):


a. Hivi nani alikuwa na Kikwete walipoamua kuanzisha mchakato huu (hakukuwa na kamati kuu ya CCM, NEC au Mkutano Mkuu wa CCM!)
b. Anayo haki ya kuanzisha tume ya maoni lakini Tume ya kusimamia kuandikwa kwa Katiba Mpya haipo - kwa sababu atakuwa amevunja ahadi yake ya "naapa kuilinda, kuitetea na kuihifadhi Katiba ya Jamhuru ya Muungano". Mgogoro huu nilikuwa nao pia na wabunge wa Zanzibar waliokuwa wanataka "muungano uvunjwe" wakiwa wameapa kuulinda!
c. Tunavyoona ni kuwa sheria hii imefanya yale ambayo Kikwete aliyataka yafanyika - yeye atakuwa muundani wa tume, yeye ataipa hadidu rejea na tume itaripoti kwake. Mjadala wote wa tangu Machi ulikuwa ni kiini macho tu kwani tayari Kikwete alishaamua nini kifanyike na kimefanyika na siwezi kushangaa kuwa hata Katiba yenyewe itakuwa vile ambavyo yeye anataka.

Mkitaka tuwavuruge kweli!

Watu wadai tuwe na nchi moja! (kanuni ya kulinda Muungano inatumika lakini Zanzibar hawatokubali).

Anajiingiza kwenye moto ambao atashindwa kuuzima huko mbeleni..heri nusu shari kuliko shari kamili. Sijui kwanini huwa anashindwa ku-fore see maamuzi yake yako likely ku create dillema zipi huko mbeleni. Kila uamuzi anaofanya unamwingiza kwenye sinto fahamu na ajabu he never learn from mistakes. Anashida kubwa huko mbele ya safari na inasikitisha kuona kwamba wanaomshauri possibly wanajua wanachokifanya penigne wameona ndiyo njia ya kum-weaken na ku take advantage ili interest zao ziwe fullfilled.
 
Nani kaamua kuwa chama chochote hakiruhusiwi kushawishi watu kuvunja muungano?

Na kwamfano watu wote wakigoma kuendelea na muungano atawafanya nini? Gosh! Hivi hawajui kuwa uki creat suspicion mtu ndo anakuwa suspicious zaidi? Badala ya kui-bold hiyo wangeacha watu wai discuss to the maximum na issue ikiwa saturated ni rahisi zaidi kufikia consensus na pengine ingeua kabisa haya malalamiko ya day to day..

Hofu haijawahi ku-solve problem zaidi ya kujenga panic na kuharibu jambo zaidi hadi likaleta madhara makubwa kamama pasingekuwa na hofu. Hofu ni silaha pekee ya uangamizi ambayo shetani amebaki nayo kwani bila hiyo amani na utulivu humwezesha mtu kutumia busara zaidi katika kuamua kuliko hisia.
 
kinachonisikitisha mimi ni unafiki wa wanasiasa wetu ambao kwa makusudi wanawapotosha wananchi na kupoteza muda kujadili watu badala ya lengo kuu ambalo ni kupata katiba. sioni mantiki ya wabunge wa cdm na nccr mageuzi kutoka ndani ya bunge wakati wa mjadala wa sheria ya kusimamia uundwaji wa katiba mpya while ile ndo ilikuwa opportunity ya kusema matakwa yao ambao naamini ni mawazo ya wafuasi wao pia ili yaingizwe kwenye hiyo sheria. nina maswali mengi saana kuliko majibu,
kama hamtaki Rais aongoze mchakato huu mnataka nani aongoze?
kwa nini mwanzoni mlimpongeza alipoamua kuanzisha mchakato huu na sasa mnampinga?
bila katiba mpya hapatatosha, and now, akiendelea na mchakato wa katiba mpya hapatatosha!!!tuwaeleweje?
mlidai katiba mpya,sasa mnadai marekebisho ya katiba ili tu kuondoa mamlaka ya Rais,naamini hata mkipewa hilo mtadai na jingine coz nimeanza kuhisi hamna malengo mazuri zaidi ya kufikiria fujo tu!!!kuna nafasi ya sisi wananchi kutoa maoni na pia kupiga kura ya maoni kuipitisha/kuipinga katiba mpya, tuacheni tutaamua wenyewe na sio nyie kutusemea....kama Rais atatumia madaraka yake vibaya, pia tume ya katiba na bunge la katiba, tuna akili timamu za kutambua kibaya na kizuri.wakituletea katiba mbovu tutaikataa kwa uthabiti wetu na kwa mapenzi mema kwa nchi yetu.acheni kutupotezea muda kwa malumbano yasiyo na tija, Kikwete yeye ni nani hadi atulazimishe Watanzania zaidi ya mil 40 tukubali katiba mbovu?acheni muda uzungumze.......na tuache kuishi kwa hisia katika mambo muhimu kwa nchi yetu kama katiba...
 
24 Reactions
Reply
Back
Top Bottom