Habari za asubuhi ndugu zangu? Ningependa niende moja kwa moja kwenye mada ,nina mdogo wangu nilimwombea vyuo kupitia mfumo wa udahili nacte sikukamilisha kuomba yani niliomba course nne nikawa nimebakiza course moja ila nikatuma hivyo hivyo course nne nikiwa na mana kuwa hiyo nafasi moja iliyobakia nitaijaza kabla ya tarehe ya mwisho ila cha kushangaza jana usiku kuanzia mida ya saa tano usiku nimeingia kwenye profile lake wanaandika "The system is temporary closed running for selection ". Naombeni ufafanuzi kidogo labda hili lipo kwangu tu au ni kwa wote?