kichunafk
JF-Expert Member
- Nov 18, 2013
- 992
- 479
Bado sijaona hoja ya kunishawishi kwamba ni kosa kubwa au si sawa kushika simu ya mwenzio.
Kama kweli kabisa hiyo simu haina chochote kile kilichokibaya kinachoweza kumfanya mwenzako achukie au akuhisi kwamba hauko mwaminifu, basi sidhani kabisa kama wewe mwenye simu utaona shida yeye akishika simu yako.
Mtu kama huna la kuficha wala hutapatwa na kiroho dunda kama mwenzako akishika simu yako. Na wala hutakuwa unaing'ang'ania kama ruba.
Hii ni common sense 101. Kama mtu huna la kuficha basi hutaificha simu yako!
As simple as 1,2,3 or A,B,C......not rocket science!
unachosema ni kweli ila pia inategemea na mwenza uliyenae.
Kuna wenza wengine wana-gubu. Hataki hata uwe na namba ya jinsia nyengine, utadhani wewe wajuana na wa jinsia moja tu.
Hata akute jina jipya kwa contacts, inakuwa tabu, maswali lukuki.
Inakera na kuumiza hasa pale unapojitahidi kuwa mwaminifu na kuacha yote yanaweza kumtia mashaka mwenza wako.
Nashauri, deal na simu yako kutokana na nature na mwenza uliyenae.
Ingawa hiyo isichukuliwe kama fimbo ya kufanya maovu.