Kwa nini mwanandoa unaficha ficha simu

Kwa nini mwanandoa unaficha ficha simu

Kwa nini wewe mwanandoa ufiche fiche simu yako na kukataza partner wako asiwe na uhuru nayo kama hakuna uchafu tena mkubwa unaoficha na unaona ni haki yako kuuendeleza ili michepuko ione iko huru na unaijali zaidi na huyo mwenzio si chochote cha kukuzuia. Ole

uaminifu hauko kwenye simu anaweza kukupa hata 24/7 ukae na simu yake lkn kama amedhamiria kuchepuka atafanya tu .. uaminifu na imani ndo vinatakiwa . na ukishaanza kuwa na hamu ya kuichunguza au kupekuwa simu ya mwenza na chanzo cha mpasuko wa ndoa
 
 
Last edited by a moderator:
Aaaghhhh!!!!! Inaboa sana kwaio asome kila kinachojili ktk maisha yangu ya kila siku?????? Kuna mambo ya kifamilia sio lazima ajue..... Mastory na mashosti zangu aaghhh mtupishe na nyie na ufukunyuku wenu

Mambo kama yapi ya kifamilia ambayo mme wako au mke wa ndoa hapaswi kuyajua? Labda kama mmeokotana kona bar,lkin navyojua mm huu ni mwamvuli unaotumika kuficha maovu sababu ya wrong choice!
 
Hoja siyo suala la kusoma kila kinachojiri.

Hoja ni kwa nini mtu upatwe na kiroho dunda kisa simu tu?

Ni mambo gani ya kifamilia ambayo hutaki mumeo ayajue?

Kwa nini mtu utake kumficha mumeo (ambaye ni sehemu ya familia) mambo ya kifamilia?

Ni ujinga mtupu na ndo maana kuna watu wanaona hayo mambo ya ndoa ni unafiki.

Unafiki unarun dunia nowdays
 
simu kitu km nnachangia nae vya ndani zaidi ya simu iliyovumbuliwa kuwasiliana tu
 
Mtu akificha sim yake n waz ana jambo baya hatak mwenzie ajue

Siyo hivo! Mfano Mimi nafichaficha sm staki mwenzangu aone mambo ninayofanya(siyo mabaya)na hii ni kutokana na akili take akiona kitu kidogo anapanic ka nini! Sasa kuepusha kuvuruga mahusiano pasipo sababu ya maana bora asiguse
 
Na nyie bana.. hivi kweli unazani kama mimi nna kitu cha kuficha nitakiacha tuu kwenye simu mpaka uje ukikute..? Labda na mimi niwe sina akili.. Smartphone siku hizi kuna apps kibao za ku hide content, bado option ya DELETE imejaa tele.. kwanini niviache..? Watu mnatafuta matatizo tuu ya bure..
 
Isitoshe sasa hivi mtu kama una siri zako unakua na simu yako ya private hiyo inakaa ofisini. Ukija home una sim ya home haina chochote..!
 
Kwa nini wewe mwanandoa ufiche fiche simu yako na kukataza partner wako asiwe na uhuru nayo kama hakuna uchafu tena mkubwa unaoficha na unaona ni haki yako kuuendeleza ili michepuko ione iko huru na unaijali zaidi na huyo mwenzio si chochote cha kukuzuia. Ole

case study! Nilitumiwa SMS zile za kufowadi na mfanyakazi mwenzangu jinsia ya kike! Mrs akadaka simu hajamaliza hata kusoma pressure juu! Nikamrush hospital baada ya siku 2 tukaruhusiwa! Nisikilizie timbwili ! Nikachukua jukumu la kuanza kujitetea kwa kitu ambacho mi hakinihusu.
Sasa kutokana na hali hiyo no bora mtu afichefiche simu kuepusha unnecessary ugomvi!.kipindi hiki watu tuna interaction na wengi Wa sehemu tofauti na ambao hatuwajui sasa hizi cm mmmmhhhhhh
 
Jamani mi nadhani ni vizuri kila mtu awe na uhuru na privacy yake na ndo maana ikaitwa privacy. Kuna mijitu yenye hila zao za moyoni...yanaweza kuanza kutuma tuma messages za ajabu ikawa tabu. Kila mtu awe na uhuru wake na simu ziwekwe password ikiwezekana.

wacha urongo bhana! mijitu imepataje no yako? Ukiona "mijitu" inawasiliana na wewe ujue wewe ni jitu mwenzao!
 
Michepuko kibao mie ---- nimpe simu yangu? To hell simpi hata iweje?
 
Siyo hivo! Mfano Mimi nafichaficha sm staki mwenzangu aone mambo ninayofanya(siyo mabaya)na hii ni kutokana na akili take akiona kitu kidogo anapanic ka nini! Sasa kuepusha kuvuruga mahusiano pasipo sababu ya maana bora asiguse

ukiona anapanic ujue si kitu kidogo. usimfanye mwenzio mjinga au taahira, na akipanic ni mabaya hayo yaache
 
Na nyie bana.. hivi kweli unazani kama mimi nna kitu cha kuficha nitakiacha tuu kwenye simu mpaka uje ukikute..? Labda na mimi niwe sina akili.. Smartphone siku hizi kuna apps kibao za ku hide content, bado option ya DELETE imejaa tele.. kwanini niviache..? Watu mnatafuta matatizo tuu ya bure..

wewe ni tatizo. uwe single basi upate uhuru wote. sio unakuwa na mtoto wa watu then unakukuruka na apps, mara delete, mara simu extra ya kuficha. shida zote hizo za kuficha za nini na kuwa mtu kumbe huwa huridhiki na mmoja ya nini. watu waficha simu ni vicheche tu. hamna cha zaidi cha kumficha mwenza zaidi ya huo uchafu
 
My phone is my phones...
My partner is my partner...
There is no any interaction btn my phone and my partner

So kila kimoja kikae kivyakeee, vikiingiliana tabu na matatizo huanzaaa
 
My phone is my phones...
My partner is my partner...
There is no any interaction btn my phone and my partner

So kila kimoja kikae kivyakeee, vikiingiliana tabu na matatizo huanzaaa

Swaaadakta ndugu,
Tena ikiwezekana kila mtu aweke na hizo password KABANG! presha za nini na wote ni viumbe dhaifu kwa wadhaifu na takatifu kwa watakatifu. Lol!:happy:
 
Swaaadakta ndugu,
Tena ikiwezekana kila mtu aweke na hizo password KABANG! presha za nini na wote ni viumbe dhaifu kwa wadhaifu na takatifu kwa watakatifu. Lol!:happy:

Kweli kabisaaaa.. mimi nligombana na my ex kwa sababu ya hilo swala la kuchokonoa my phone, so sitaki mtu agusee simu yanguu

SITAKIII NASEMA
 
Back
Top Bottom