Kwa nini Mungu alimuumba binadamu?

Kwa nini Mungu alimuumba binadamu?

Hebu rudi kwenye post zako za nyuma mzee. Wewe mwenyewe ndiye uliyeleta hoja ya Spiderman ukisema kama Muumba ulimwengu ni fact kwasababu Biblia imeandika, basi Spider-Man is real because there's also a book about him.

Kitendo cha wewe kutumia Biblia kama kipimo cha kuthibitisha uwepo wa Mungu, ndicho kilichonifanya nikuonyeshe kuwa dhana ya Mungu haitegemei Biblia kama chanzo chake, ipo nje ya hapo!

Sasa kama ulikuwa unajua tangu mwanzo kuwa hiyo dhana haikutokana na Biblia, mfano wako wa Spiderman na vitabu ulikuwa unafanya nini hapa kama sio kupoteza muda wa uzi? Umeona hoja yako imefeli sasa hivi unaanza kurudi nyuma kinyamela!
Umeona sasa?

Mfano wa Spider-Man, Harry Potter, Superman nk niliutoa mwanzoni kabisa na sio kwasababu ya kujibu hoja ya kuwa Mungu naye ameandikwa.

Nilikuwa nakosoa dhana ya kuamini Mungu kwasababu kuna majina ambayo jamii fulani zimekuwa zikiyaabudu kama miungu kwa lengo la kutafuta ulinzi.

Hakuna sehemu nimesema Biblia wala Quran kuwa ndio chanzo cha kwanza kuhusu swala la Mungu.

Mara kadhaa humu nimekuwa nikisema mtu ndiye aliyemuumba Mungu kupitia mawazo yake baada ya kushindwa kupata majibu ya baadhi ya maswali.
 
Mimi ndio nimeleta mfano wa kisayansi kwa sababu facts zake ni ukweli unaoonekana unaounga mkono hoja yangu ya uwepo wa Muumba. Wewe badala ya kuleta hoja mbadala kupinga hizo facts, unaleta vitisho vya kisiasa eti kwa nini nachagua baadhi ya maeneo?

Sayansi yenyewe imejengwa juu ya kuchagua na kuchuja. Kama una hoja ya kisayansi inayothibitisha ulimwengu hauna mwanzo au haufuati sheria yoyote, ilete hapa mezani tuichambue. Acha kulialia kuhusu nani kaanzisha mada ya sayansi!
Kwa mfano wewe ukiniambia kitu fulani ni scientific fact, mimi nathibitishaje kujua kama hicho kitu kweli ni fact?

Au napaswa tu kukubali ni fact kwasababu wewe umekiita fact?
 
Katika falsafa, huo ulimwengu wako ulioupa uwezo wa kujiumba na kujipangia sheria bila kuwa na chanzo cha nje, ndio unaosadifu sifa za Mungu tunayemzungumzia.

Tofauti yangu na wewe ni kwamba wewe unajiita hujui kwa sababu pengine unaogopa tu kumtaja Mungu Mkuu, lakini kiuhalisia umeshakubali uwepo wa hiyo nguvu kuu! Umeelewa mzee?
Ulimwengu upi?
 
Back
Top Bottom