Dhana ya uwepo wa Muumba haikutokana na Biblia wala Quran, ilianza kama hoja ya kifalsafa na kisayansi hata kabla ya vitabu vya dini kuandikwa, ni wazi hili hukuwa ukilijua kabisa.
Mantiki yake iko hivi, imwengu una mwanzo hata sayansi kupitia Big Bang Theory inakubali hili, na chochote chenye mwanzo kimesababishwa na kitu kingine kilicho nje yake.
Hauwezi kuwa na ulimwengu tata wenye laws of physics bila kuwa na uncaused cause, biblia au Quran hazikuunda dhana ya Mungu, bali zimeelezea tu na kumpa sifa Muumba ambaye uwepo wake unathibitishwa na ulimwengu wenyewe.
Spiderman hana uhusiano na asili ya ulimwengu, yeye ni tabia tu ndani ya kitabu. Mungu ndiye aliyesababisha hata huyo mwandishi wa spiderman awepo.