Mara nyingi Dr. Slaa anapochangia hoja mbalimbali hapa jamvini kuna watu wengine wanatoa lugha za kejeli kwake na hata baadhi kumtukana. Lakini kwa nini basi haachi kuingia na kuchangia Hoja? (TUJADILI)
Binafsi naamini Slaa (PHD) ni mtu au ni kiongozi tofauti sana na viongozi wengine wa Tanzania na hasa Africa kwa ujumla, anaumia sana anapoona watu humu jamvini wanatoa hoja zinazodhihirisha kutokuelewa kwao kwa mambo ya kitaifa au tu kwa kuwa na maslahi binafsi na serikali au chama tawala.
Dr. Slaa anaumia sana kuona nchi inageuka mtaji wa watu wachache ambao unachochewa na watanzania wenyewe kutojitambua na kutotambua ni nini iliyohaki yao kutokana na rasimali za nchi yao waliyopewa na Mungu BURE.
Slaa Dr. ni mtu ninaye mhusudu, ninampenda, ninamheshimu, ninamdhamini na nitaendelea kufanya hivyo kwa nafsi yangu si kwa sababu ya chama chake, sura yake, imani yake na vitu vingine kama hivyo, ila ni roho yake ya kibinadamu, kusimamia haki, kuwa muwazi kwake binafsi, na hekima aliyopewa na MUNGU ili kutetea haki za wanyonge wana wa Taifa hili tunaoumia kwa maslahi ya watu wachache na familia zao na marafiki zao ambayo ni mazao ya msingi mbovu wa Taifa.
Hivi kweli kwa wengine (wanaojifanya miungu watu) wenye hadhi kama ya Dr. Slaa kitaifa na kimataifa wanaweza kujumuika na sisi hapa jamvini? ukizingatia wengine hapa JF ni fyatu.
Binafsi naamini Slaa (PHD) ni mtu au ni kiongozi tofauti sana na viongozi wengine wa Tanzania na hasa Africa kwa ujumla, anaumia sana anapoona watu humu jamvini wanatoa hoja zinazodhihirisha kutokuelewa kwao kwa mambo ya kitaifa au tu kwa kuwa na maslahi binafsi na serikali au chama tawala.
Dr. Slaa anaumia sana kuona nchi inageuka mtaji wa watu wachache ambao unachochewa na watanzania wenyewe kutojitambua na kutotambua ni nini iliyohaki yao kutokana na rasimali za nchi yao waliyopewa na Mungu BURE.
Slaa Dr. ni mtu ninaye mhusudu, ninampenda, ninamheshimu, ninamdhamini na nitaendelea kufanya hivyo kwa nafsi yangu si kwa sababu ya chama chake, sura yake, imani yake na vitu vingine kama hivyo, ila ni roho yake ya kibinadamu, kusimamia haki, kuwa muwazi kwake binafsi, na hekima aliyopewa na MUNGU ili kutetea haki za wanyonge wana wa Taifa hili tunaoumia kwa maslahi ya watu wachache na familia zao na marafiki zao ambayo ni mazao ya msingi mbovu wa Taifa.
Hivi kweli kwa wengine (wanaojifanya miungu watu) wenye hadhi kama ya Dr. Slaa kitaifa na kimataifa wanaweza kujumuika na sisi hapa jamvini? ukizingatia wengine hapa JF ni fyatu.