Mwakiluma
Senior Member
- Jan 23, 2012
- 120
- 47
....Huyu si mwingine bali ni SAID MIRAJ...katika uchaguzi wa mwaka 2010 huyu ndiye mtu muhimu alichangia kushindwa vibaya kwa CUF katika nafasi ya urais kipindi hicho akiwa hana ugomvi wowote na chama...
Jinsi alivyohusika...
1. Ndiye aliyekuwa meneja wa kampeni wa Lipumba na kusababisha Lipumba apate kura kidogo mno...
2. Ndiye aliyemshauri Lipumba kuendesha kampeni ya mtu mmoja mmoja huku akijua kuwa nchi hii ilikuwa na wapiga kura zaidi ya millioni 20 hivyo kuwafikia wote ingekuwa ni ndoto katika kipindi kile cha kampeni....
3. Wakati tuhuma zikielekezwa kwa CUF na vyama vingine yeye hakujisumbua kujibu bali alikaa kimya....kisiasa hii ni mbaya sana kwani hata Kinana wa CCM alijibu kila tuhuma zilizoelezwa kwa chama chake na vyama pinzani hata zile za ufisadi pamoja na kweli kuwa chama chake kimechafuka...hata Mabere Marando alikuwa mbele kujibu kila shambulio lilioelekezwa kwao kama njia ya kuwapa imani wananchi
4. Huyu ndiye aliyeshauri Lipumba afungie kampeni Dar es salaam huku akijua kabisa kuwa CUF kina wafuasi wengi mikoa ya Lindi na Mtwara ambako angeongeza msukumo kwa wananchi...Mwenzao wa Chadema Dk. Slaa yeye alifungia kampeni Mbeya akijua fika kuwa ndiko alikuwa na wafuasi wengi...
Huyu jamaa hafai kuwa mwenyekiti wa chama chochote kile hata cha watoto kwani hana mbinu za ushindi...sio mwongeaji na hana mbinu za kisiasa...labda kama ADC haina Malengo Makubwa kisiasa...
Nawasilisha....
Jinsi alivyohusika...
1. Ndiye aliyekuwa meneja wa kampeni wa Lipumba na kusababisha Lipumba apate kura kidogo mno...
2. Ndiye aliyemshauri Lipumba kuendesha kampeni ya mtu mmoja mmoja huku akijua kuwa nchi hii ilikuwa na wapiga kura zaidi ya millioni 20 hivyo kuwafikia wote ingekuwa ni ndoto katika kipindi kile cha kampeni....
3. Wakati tuhuma zikielekezwa kwa CUF na vyama vingine yeye hakujisumbua kujibu bali alikaa kimya....kisiasa hii ni mbaya sana kwani hata Kinana wa CCM alijibu kila tuhuma zilizoelezwa kwa chama chake na vyama pinzani hata zile za ufisadi pamoja na kweli kuwa chama chake kimechafuka...hata Mabere Marando alikuwa mbele kujibu kila shambulio lilioelekezwa kwao kama njia ya kuwapa imani wananchi
4. Huyu ndiye aliyeshauri Lipumba afungie kampeni Dar es salaam huku akijua kabisa kuwa CUF kina wafuasi wengi mikoa ya Lindi na Mtwara ambako angeongeza msukumo kwa wananchi...Mwenzao wa Chadema Dk. Slaa yeye alifungia kampeni Mbeya akijua fika kuwa ndiko alikuwa na wafuasi wengi...
Huyu jamaa hafai kuwa mwenyekiti wa chama chochote kile hata cha watoto kwani hana mbinu za ushindi...sio mwongeaji na hana mbinu za kisiasa...labda kama ADC haina Malengo Makubwa kisiasa...
Nawasilisha....