Suzy Elias
JF-Expert Member
- Nov 9, 2021
- 1,067
- 6,193
Kurejeshwa Makalla ndani ya mfumo mwaka 2021 na kuwa RC Dar es Salaam tukubali ama tukatae ipo nguvu ya ushawishi wa JK ilitumika kumshawishi Rais Samia.
Ieleweke, Makalla ni swahiba na mwandani lialia wa Jakaya Kikwete na duru zilitabanaisha baada ya JPM kumfuta kazi Makalla kipindi kile mwana Msoga aliumia ki aina.
Ukweli ni kwamba, Makalla hana uwezo wa kuongoza kwa nafasi ya Mkuu wa Mkoa kwa sababu ni mswahili na mtu mwenye taralila nyingi huku utendaji ukiwa sifuri! Kwa ufupi, ni mjanja mjanja tu asiye na maarifa ya kuongoza.
Ni wazi sasa, huenda Rais Samia ameamua ampe Dar es Salaam mtoto wa zao lao yeye na Magufuli ndugu Chalamila na kumshusha mpendwa wa JK.
Kutolewa Dar es Salaam na kutupwa Mwanza ni sawa na kushushwa japokuwa majukumu ni yaleyale.
Je, ni mwanzo wa zao la JPM na Rais Samia kupewa sehemu nyeti?
Ni wazi hilo ni jaribu la kwanza kwa watu wa timu JK kutoswa.
Mda utasema.
Ieleweke, Makalla ni swahiba na mwandani lialia wa Jakaya Kikwete na duru zilitabanaisha baada ya JPM kumfuta kazi Makalla kipindi kile mwana Msoga aliumia ki aina.
Ukweli ni kwamba, Makalla hana uwezo wa kuongoza kwa nafasi ya Mkuu wa Mkoa kwa sababu ni mswahili na mtu mwenye taralila nyingi huku utendaji ukiwa sifuri! Kwa ufupi, ni mjanja mjanja tu asiye na maarifa ya kuongoza.
Ni wazi sasa, huenda Rais Samia ameamua ampe Dar es Salaam mtoto wa zao lao yeye na Magufuli ndugu Chalamila na kumshusha mpendwa wa JK.
Kutolewa Dar es Salaam na kutupwa Mwanza ni sawa na kushushwa japokuwa majukumu ni yaleyale.
Je, ni mwanzo wa zao la JPM na Rais Samia kupewa sehemu nyeti?
Ni wazi hilo ni jaribu la kwanza kwa watu wa timu JK kutoswa.
Mda utasema.