Kwa mara ya kwanza leo nimepigana

Kwa mara ya kwanza leo nimepigana

Shammy-

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2022
Posts
7,179
Reaction score
18,850
Katika makuzi yangu sikumbuki lini niliwahi kupigana na mtu na hata kama nilipokuwa najikuta niko kwenye ugonvi silaha yangu ilikuwa mdomo😁 nilipokuwa/huwa nikion naona mambo yamezidi nanyamaza na kuondoka eneo la tukio ili nsije bandwa😂! Kumbe bwana nilikuwa na ji underrate kumbe ninaweza bwanaa leo kidogo nimrarue mdada mmoja wa kikurya😄 ilikuwa hivi

Nilikuwa nimetoka shift ya mchana, nimechoka na njaa ikiwa imenikolea haswa ,nikaamua kupitia canteen ili nichukue chakula(take away) ili niende nacho nyumbani. Basi mhudumu akawa amenifungia sahani moja ,wakati ananiandalia ya pili mfanyakazi mwenzangu aliyekuwa anaingia shift ya usiku akaingia canteen pia. Sasa, yeye anataka kuhudumiwa kwanza wakati teye kanikuta!! Nikamwambia kwa heshima tu kuwa kila mtu ana haraka na ana njaa, siyo yeye peke yake so awe mpole zamu yake itafika!

Lakini majibu niliyoyapata kutoka kwake yalinitibua. Akanijibu kwa kejeli kwamba yeye anaenda kwenye majukumu, nikamwambia na mimi natoka kwenye hayo hayo majukumu. Hapo ndipo mzozo ukaanza. Chakula changu kilipokuja, akajitokeza kwa nguvu kama anataka kuchukua chakula kile kwa sababu naye aliagiza aina ya chakula nilichoagiza mimi,basi akawa amerusha hela hapo ,,hapo ndipo nikajua mambo yamebadilika.

Nikasema usinitanie nikamkwida shingoni uzuri alikuwa amevaa lab coat ko nikamkwida kisawa sawa hakuweza kufurukuta wakati nimemkwida si akaningata nikapenyeza mkono wa kushoto taratibu nikamminya chuchu si unajua chuchu zinavouma basi akawa amelegeza meno na kuishiwa nguvu nikatake advantage hiyo nikamzaba makofi mawili matatu ya nguvu si akawa amekimbia 😁 akacha na slippers zake! Matukio yote hayo yametokea within few mins halafu uzuri tulikuwa upande wa jikoni hatukuweza kuamuliwa kwa urahis ilikuwa ni nadra kuonwa na watu wengine ..bas hapa napoongea mkono unauma ila sio sana maana kaning’ata ila dam hazijatoka kuna alama kwa mbali..basi bwana siku yangu imeisha hivoo
 
Back
Top Bottom