Kwa kugawa wanyama wetu tumeuza upekee wetu. Tumebaki na nini?

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Moja ya jambo muhimu katik biashara ni upekee wa bidhaa yako. Watu hawaji kununua kwako bidhaa au huduma kwa sababu ya huruma, ni kwa sababu una kitu wanachohitaji na unakitoa kwa ubora kuliko washindani wako.

Kwa miaka kadhaa huko nyuma Tanzania tumetokea kugawa wanyama wetu kwa mataifa mbalimbali. Inawezekana hii ilifanywa kukuza mahusiano na nchi hizo, inawezekana imefanywa tu kwa sababu ya tamaa ya wachache. Inawezekana pia tulilipwa fidia.

Ila tujiulize tunapoteza nini kwa kufanya hivyo? Je mtalii akiambiwa achague kwenda safari Dubai, sehemu yenye miundombinu na huduma bora kutuzidi, kweli atachagua kuja kwetu aache kule? Tena ukizingatia hawa hawa tunaowapa wanyama tunawapa pia nafasi ya kufungua mahoteli katika mbuga zetu na kuwa agents wa utalii, hawawezi kuwa wanavutia kuwapeleka watalii kwao badala ya kuwaleta huku kwetu?

Ujangili tumeshindwa pia kuudhibiti kwa maana hiyo kuna uwezekano kuna wanyama watapotea huku kwetu ila watakuwepo huko tulipowagawa. Hizi lawama atazibeba nani?

Kwa mtazamo wangu, dunia inahitaji mashirikiano kati ya nchi na nchi ila ni muhimu sana kumaintain competitive advantage uliyo nayo katika uchumi na biashara. Uzalendo unaanzia hapo.
 
Mm nilimuona Magufuli akimgawia ndege tausi rais Uhuru wa Kenya. Kuna wanyama gani tena wamegawa? Na nani kagawa kwa nani?
Afadhali hata hiyo ilifanywa kwa uwazi, na hata sisi tulipewa hao tausi kwa uwazi na rekodi ikawekwa.

Mimi huwa napinga sana ninapoona mtu anadai kutoa msaada kwa mwingine kwa kificho tena kwa kutumia mali si yako. Mwenye mali hawezi kesho kudai ile ilikuwa mali yake wala hawezi kwenda kuomba msaada kwa yule aliyesaidiwa kwa kigezo cha msaada huo wa nyuma kwa sababu ilifanywa kisirisiri bila yeye kushirikishwa. Shida ipo hapo. Nina experience kwenye hili.
 
Watalii wakija huku wanataka kwenda safari waone wanyama wakiwa katika mazingira yao halisi. Mbona zoo zipo kitambo na wanyama walichukuliwa toka kipindi cha ukoloni
Umeona hizo zoo za Dubai? Mazingira yakiwa makubwa wakaachiwa, haina tofauti na kule walipotoka. Ni kama wale waliohamishiwa Chato.
 
Mama hadi alitamani iwepo maritime yabkusafirisha wanyama hai sijui zanzbar kuna wanyama gani hadi waundiwe meli. Huyu bibie mpaka miaka 2030 ashahamisha serengeti yetu
 
Moja ya jambo muhimu katik biashara ni upekee wa bidhaa yako. Watu hawaji kununua kwako bidhaa au huduma kwa sababu ya huruma, ni kwa sababu una kitu wanachohitaji na unakitoa kwa ubora kuliko washindani wako.

Kwa miaka kadhaa huko nyuma Tanzania tumetokea kugawa wanyama wetu kwa mataifa mbalimbali. Inawezekana hii ilifanywa kukuza mahusiano na nchi hizo, inawezekana imefanywa tu kwa sababu ya tamaa ya wachache. Inawezekana pia tulilipwa fidia.

Ila tujiulize tunapoteza nini kwa kufanya hivyo? Je mtalii akiambiwa achague kwenda safari Dubai, sehemu yenye miundombinu na huduma bora kutuzidi, kweli atachagua kuja kwetu aache kule? Tena ukizingatia hawa hawa tunaowapa wanyama tunawapa pia nafasi ya kufungua mahoteli katika mbuga zetu na kuwa agents wa utalii, hawawezi kuwa wanavutia kuwapeleka watalii kwao badala ya kuwaleta huku kwetu?

Ujangili tumeshindwa pia kuudhibiti kwa maana hiyo kuna uwezekano kuna wanyama watapotea huku kwetu ila watakuwepo huko tulipowagawa. Hizi lawama atazibeba nani?

Kwa mtazamo wangu, dunia inahitaji mashirikiano kati ya nchi na nchi ila ni muhimu sana kumaintain competitive advantage uliyo nayo katika uchumi na biashara. Uzalendo unaanzia hapo.
Haya mawazo kama yako nilikuwa nayo nilipokuwa darasa la tatu. Wakati huu niliamini simba, chui na wanyama wote wako Tanzania tu
 
Haya mawazo kama yako nilikuwa nayo nilipokuwa darasa la tatu. Wakati huu niliamini simba, chui na wanyama wote wako Tanzania tu
Sijasema hivyo. Kwa hiyo unabisha kuwa ukiacha wale tausi tuliompa Kenyatta hatujawahi kugawa wanyama wetu kwa mataifa mengine?
 
Huwa nashangaa sana kuona watu wanachukulia maisha yetu na mali zetu simple sana,

Ila hawajui kuna mataifa yanatamani na wanalia kuona jinsi tusivyojali
Hakuna takwimu tunazozijua za wanyama,wadudu,na hata ndege wetu tulio nao

Hatuna Habari kabisa ni ndege aina ngapi wameisha na kutoweka kabisa Tanzania?

Sio kuibiwa tu bali hata kuuwawa na wawindaji au kuungua kwa moto na hata kwa kukatwa miti tu

Kuwalaumu hao ni kazi bure kwani wao ndio wanajiona wazalendo kuliko mtu mwingine yeyote

Wakipata vyeo tu wanaamua wanavyotaka kwa sababu hata wabunge hawana ubavu wa kuongea ingawa wana nguvu za soda

Nakumbuka kuna wakati Egyptian tortoise walitoweka na kupotea extinction
Ni viumbe wadogo wanaopatikana Egypt, Libya na Isreal tu

Mmarekani mmoja alipoona wanaisha aliumia sana kwa sababu wengi walikuwa wanauzwa kama pet

Ilibidi achukue baadhi na kuwapeleka America na kuwalea huko
Walipozaliana wengi akawarudisha Egypt
Hebu fikiria wao wameshindwa kuwalea mpaka kaja mtu kuwasaidia
Na hii ndio akili zetu waafrika wote

Leo tunao ila kesho watabaki kwenye picha tu, tuwalinde kwa pamoja na hata watoto marufuku Manati
 
Afadhali hata hiyo ilifanywa kwa uwazi, na hata sisi tulipewa hao tausi kwa uwazi na rekodi ikawekwa.

Mimi huwa napinga sana ninapoona mtu anadai kutoa msaada kwa mwingine kwa kificho tena kwa kutumia mali si yako. Mwenye mali hawezi kesho kudai ile ilikuwa mali yake wala hawezi kwenda kuomba msaada kwa yule aliyesaidiwa kwa kigezo cha msaada huo wa nyuma kwa sababu ilifanywa kisirisiri bila yeye kushirikishwa. Shida ipo hapo. Nina experience kwenye hili.
Funguka acha woga, hapa ni JF uko salama. Nani kamgawia nani na kamgawia mnyama gani?
 
Waachiwe kwenda jangwani?

Wataweza kumuona cheetah anawinda swala kama Serengeti?

Wataona Wilderbeast migration
Nimesema mazingira yakiwa makubwa kwa maana hiyo siyo typical zoo ambayo mnyama yuko ndani, mtalii yuko nje. Size siyo kama ya Serengeti ila ni kubwa kiasi cha mtalii kuwa ndani ya hifadhi na kupata experience ile ile. Tena kwa sababu ukubwa wake ni wa kiasi, wanyama wanaonekana kwa urahisi zaidi ambayo inaweza kuwa advantage zaidi kwao kuliko kwetu ambapo unaweza kukaa siku nzima haujamuona mnyama fulani. Hicho ndiyo nimeona mimi
 
Huwa nashangaa sana kuona watu wanachukulia maisha yetu na mali zetu simple sana,

Ila hawajui kuna mataifa yanatamani na wanalia kuona jinsi tusivyojali
Hakuna takwimu tunazozijua za wanyama,wadudu,na hata ndege wetu tulio nao

Hatuna Habari kabisa ni ndege aina ngapi wameisha na kutoweka kabisa Tanzania?

Sio kuibiwa tu bali hata kuuwawa na wawindaji au kuungua kwa moto na hata kwa kukatwa miti tu

Kuwalaumu hao ni kazi bure kwani wao ndio wanajiona wazalendo kuliko mtu mwingine yeyote

Wakipata vyeo tu wanaamua wanavyotaka kwa sababu hata wabunge hawana ubavu wa kuongea ingawa wana nguvu za soda

Nakumbuka kuna wakati Egyptian tortoise walitoweka na kupotea extinction
Ni viumbe wadogo wanaopatikana Egypt, Libya na Isreal tu

Mmarekani mmoja alipoona wanaisha aliumia sana kwa sababu wengi walikuwa wanauzwa kama pet

Ilibidi achukue baadhi na kuwapeleka America na kuwalea huko
Walipozaliana wengi akawarudisha Egypt
Hebu fikiria wao wameshindwa kuwalea mpaka kaja mtu kuwasaidia
Na hii ndio akili zetu waafrika wote

Leo tunao ila kesho watabaki kwenye picha tu, tuwalinde kwa pamoja na hata watoto marufuku Manati
Inasikitisha sana. Ndege wote wazuri wamepotea Dar, tumebaki na popo tu. Dar es Salaam hii hii kulikuwa na hadi vipepeo, sijui mara ya mwisho kuona kipepeo Dar ni lini.

Miaka michache ijayo utaona hadi Watanzania ambao hawajawahi kufika Serengeti wanapiga picha na wanyama wakiwa Dubai.
 
Inasikitisha sana. Ndege wote wazuri wamepotea Dar, tumebaki na popo tu. Dar es Salaam hii hii kulikuwa na hadi vipepeo, sijui mara ya mwisho kuona kipepeo Dar ni lini.

Miaka michache ijayo utaona hadi Watanzania ambao hawajawahi kufika Serengeti wanapiga picha na wanyama wakiwa Dubai.
Wee acha tu mkuu, wapenda asili tupo wengi ila hao wasiojali wana laana leo na kesho

Mkuu tuna farm mkoani huko na kuna maji tuliochimba wenyewe kwa kunywesha mifugo
Ndege wa aina zaidi ya kumi wanakuja hapo
Tatizo likawa kwa watoto wenye manati ikawa ndio sehemu ya mawindo yao

Ilibidi nitume vijana kukamata na kuwanyan'ganya manati
Huwezi kuamini within three weeks walijaza ndoo nne za manati na mwisho watoto wakaacha kuja kabisa
Ila kila wakikamatwa walikuwa wanapewa na darasa kuhusu kuwalinda badala ya kuwauwa

Haya yote tulikuwa tunafundishwa shuleni na manyumbani ila sio siku hizi
 
Moja ya jambo muhimu katik biashara ni upekee wa bidhaa yako. Watu hawaji kununua kwako bidhaa au huduma kwa sababu ya huruma, ni kwa sababu una kitu wanachohitaji na unakitoa kwa ubora kuliko washindani wako.

Kwa miaka kadhaa huko nyuma Tanzania tumetokea kugawa wanyama wetu kwa mataifa mbalimbali. Inawezekana hii ilifanywa kukuza mahusiano na nchi hizo, inawezekana imefanywa tu kwa sababu ya tamaa ya wachache. Inawezekana pia tulilipwa fidia.

Ila tujiulize tunapoteza nini kwa kufanya hivyo? Je mtalii akiambiwa achague kwenda safari Dubai, sehemu yenye miundombinu na huduma bora kutuzidi, kweli atachagua kuja kwetu aache kule? Tena ukizingatia hawa hawa tunaowapa wanyama tunawapa pia nafasi ya kufungua mahoteli katika mbuga zetu na kuwa agents wa utalii, hawawezi kuwa wanavutia kuwapeleka watalii kwao badala ya kuwaleta huku kwetu?

Ujangili tumeshindwa pia kuudhibiti kwa maana hiyo kuna uwezekano kuna wanyama watapotea huku kwetu ila watakuwepo huko tulipowagawa. Hizi lawama atazibeba nani?

Kwa mtazamo wangu, dunia inahitaji mashirikiano kati ya nchi na nchi ila ni muhimu sana kumaintain competitive advantage uliyo nayo katika uchumi na biashara. Uzalendo unaanzia hapo.
Ni kama mashimo ya Buzwagi na Geita
 
Ni kama mashimo ya Buzwagi na Geita
Just imagine daraja la Tanzanite tumelijenga kwa mkopo, tena mkopo tunaoulipia kwa kukamuana kwa tozo. Leo hii tunalingishia lile lipastic tuliloweka juu pale hatujiulizi kwa nini hatukujenga hilo daraja kwa mapato yatokanayo na madini hayo ili kweli tuwe na kitu tangible kuonyesha faida za madini hayo.
 
Hiyo mbuga inayotengenezwa dubai ni replica au ni mfanano na mbuga ya serengeti, hivyo ni tishio kubwa la utalii wetu hapo mbeleni........viongozi waliopewa dhamana wanahujumu nchi kwa maslahi yao binafsi, na kama ulivyodokeza, mbali na tishio la kutoweka wanyama adimu huko serengeti kutokana na kulegalega kwa shughuli za uhifadhi, pia hujuma zinaweza kufanyika dhidi ya wanyama tulio nao ili kuipa nguvu hiyo mbuga ya mchongo huko dubai...​
 
Damu nzito kuliko wanyama...

Mjinga anatetea walaumiwe walioingia mikataba, wakati mikataba ni maandishi tu yaliyoko kwenye makaratasi yakawekwa kabatini bila kumdhuru yeyote.

Ajabu anatokea mama yao anaenda kutekeleza kwa vitendo yale maandishi yaliyopo kwenye makaratasi, matokeo yake wamasai wanaanza kufukuzwa kama wanyama kwenye ardhi waliyokuwepo miaka yote bila kuwaathiri wanyama.

Huyu kipofu wa akili halioni hili, amejaa mahaba yanayo influence akili yake mpaka imedumaa, anajua kutetea kila kitu kama roboti lililosetiwa Uarabuni kwa ajili ya kazi hiyo.
 
Back
Top Bottom