Kwa Kiswahili tofauti ya maneno ‘Kwenye’ na ‘Katika’ ikoje?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,300
33,917
Matumizi sahihi ya maneno haya kwa kweli huwa yananitatiza sana? Huwa napata shida sana kujua ni wakati gani wa kutumia kwa mfano neno "Kwenye " au wa kutumia neno "Katika" kwenye kuongea au kuandika

Hebu wajuvi wa Lugha hii tupeni wengine darasa tuelewe jinsi ya kuyatumia maneno haya kwa usahihi!
 
Matumizi sahihi ya maneno haya kwa kweli huwa yananitatiza sana? Huwa napata shida sana kujua ni wakati gani wa kutumia kwa mfano neno "Kwenye " au wa kutumia neno "Katika" kwenye kuongea au kuandika

Hebu wajuvi wa Lugha hii tupeni wengine darasa tuelewe jinsi ya kuyatumia maneno haya kwa usahihi!
Yanaweza kutumika kama mbadala wa mojawapo (interchangeably), kwani maana zake zinaendana.
 
Matumizi sahihi ya maneno haya kwa kweli huwa yananitatiza sana? Huwa napata shida sana kujua ni wakati gani wa kutumia kwa mfano neno "Kwenye " au wa kutumia neno "Katika" kwenye kuongea au kuandika

Hebu wajuvi wa Lugha hii tupeni wengine darasa tuelewe jinsi ya kuyatumia maneno haya kwa usahihi!


Neno "Kwenye" hutumika kumaanisha "ndani ya" mfano unaweza kumwambia mtu; "Tia maji kwenye ndoo", kwa kiingereza ni; Put water into a bucket. Hivyo neno "kwenye = into".

Neno "Katika" hutumika kwa maana ya; kuhusu, kuhusiana nk, mfano mtu anaweza kusena; Katika jambo hili hatuwezi kupata suluhu, Katika kitabu hichi huwezi kupata habari hiyo nk, In this book, you can't get that information. Hivyo neno "katika=in".

Pia kuna wakati inawezekana maneno hayo kutumika kwa pamoja katika kitu kimoja, mfano; kwenye kitabu hichi hakuna hiyo habari, pia; Katika kitabu hichi hakuna hiyo habari.
 
Neno "Kwenye" hutumika kumaanisha "ndani ya" mfano unaweza kumwambia mtu; "Tia maji kwenye ndoo", kwa kiingereza ni; Put water into a bucket. Hivyo neno "kwenye = into".

Neno "Katika" hutumika kwa maana ya; kuhusu, kuhusiana nk, mfano mtu anaweza kusena; Katika jambo hili hatuwezi kupata suluhu, Katika kitabu hichi huwezi kupata habari hiyo nk, In this book, you can't get that information. Hivyo neno "katika=in".

Pia kuna wakati inawezekana maneno hayo kutumika kwa pamoja katika kitu kimoja, mfano; kwenye kitabu hichi hakuna hiyo habari, pia; Katika kitabu hichi hakuna hiyo habari.
ushamaliza kila kitu
 
Nimelewa ila sijaelewa ni kwa nini hatuwezi kueleweshana mpaka tutumie Kiingereza!!

Mniwie radhi lakini...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom