Kwa hili Wamarekani wanatudharau

Kwa hili Wamarekani wanatudharau

Mtoa mada acha unafiki, tafuta hela mkuu utakufa kwa kihiro kisicho na faida, urais ni taasisi na ina Washauri na wanajua nini wanakifanya, wewe unajua kuwa president Madiba (rip)aliishi pale Arusha for more than a week baada ya divorce na mama Nomzamo?
Siipendi dhambi ya unafiki...tafadhari niambie unafiki wangu uko wapi
 
Tatizo lenu mnalinganisha ukuu wa America na Tanzania. Chato haiwez linganishwa na DAR!! Biden akienda popote lazima mkuu wa NCHI husika awepo no way, but kwa vinchi vichanga kama sisi is not necessary!!
Katika kuheshimu utu na thamani ya raia wa nchi fulani,hakuna nchi ndogo wa kubwa...Rais wa Gambia akija Tanzania anapaswa kupewa heshima ile ile ya Raisi wa Russia akija Tanzania...hatumheshimu Raisi kwa maana ya mtu...ila thamani ya taifa na watu wake
 
Dooh!! Hebu hama kwa shemeji yako nenda kapange
Ni hivyo sio? Rais wa nchi uingie kwenye nchi nyingine mwenyeji wako asikutambue?
Bado Kuna uchafu wa siasa za Magufuli alizozifanya haujaondolewa kwenye taswira ya nchi kimataifa
Nchi bado inanuka
Huwa dhambi inaondolewa kwa Toba haitoki yenyewe
Asanteni.
 
Jamani Mimi nime sema sana humu kuwa heshima ya nchi ni uchumi imara, tujenge uchumi imara ili tuheshimike duniani.

Sasa concept hiyo Samia hana, haipo kichwani, na anapenda sana kujidhalilisha mwenyewe, Rais mzima utaendaje nje kucheza movie? , Hivyo vitu ni vidogo kiasi kwamba wasaidizi wake wana takiwa kufanya, ni aibu ya Karne, Biden Hana muda nae , Hana impacts na ideas za kuongea na Biden.
 
Ni hivyo sio? Rais wa nchi uingie kwenye nchi nyingine mwenyeji wako asikutambue?
Bado Kuna uchafu wa siasa za Magufuli alizozifanya haujaondolewa kwenye taswira ya nchi kimataifa
Nchi bado inanuka
Huwa dhambi inaondolewa kwa Toba haitoki yenyewe
Asanteni.
Acha kubwabwaja,Magufuli ndo amemzuia Baiden asimpokee Rais Samia?mbona waziri mkuu wa UK alifanya ziara Tanzania baada ya kifo Cha Magufuli,siyo kila kitu mmbebeshe Magufuli,nyie endeleeni kuhubiri kula kwa urefu wa kamba na kulamba asali mnafikiri hao mabeberu ni wenzenu
 
Rais wetu anakaribia kufunga wiki nchini mwao lakini mwenyeji wake ambaye ndiye mkuu wa nchi hajakutana na mgeni wake(Mh. Rais wetu)

Hii ni dharau...ifike mahali tuwe masikini jeuri, hivi Mh. Biden angefanya ziara nchini Tanzania, kweli Mhe. Rais wetu angekuwa bize na mambo mengine na kuicha hiyo shughuli kwa waandamizi wake???

Ifike mahali wizara ya mambo ya nje wajitafakari pia katika hili.
Awamu ya tano iliharibu sana diplomasia za nje, kuteka watu, wizi wa kura, kubambika wapinzani kesi...kwa utawala wa aina ile huwezi kuheshimika nje. Angalao mama anajitahidi kujieleza yeye hakukubaliana na utawala wa hovyo aina ile, wataelewa Sasa hatuko huko.
 
Kwa mfano Bideni akija Tanzania kupumzika Serengeti ana weza hasikutane na Mama Samia ?
Mbona nyie siyo waelewa? Rais Samia kaenda kuzindua sinema yake ya Royal Tour, ni ziara binafsi siyo ya Kiserikali. Sasa unataka Biden ampokee kwenye ziara yake binafsi?
 
Ni sawa uende nyumbani kwa mtu halafu uishie kupokelewa na hausi gelo ambaye atakuzungusha tu uone mazingira ya nyumba bila kukutana na mwenye nyumba.

Ndio kinachotupata sasa.
 
Rais wetu anakaribia kufunga wiki nchini mwao lakini mwenyeji wake ambaye ndiye mkuu wa nchi hajakutana na mgeni wake(Mh. Rais wetu)

Hii ni dharau...ifike mahali tuwe masikini jeuri, hivi Mh. Biden angefanya ziara nchini Tanzania, kweli Mhe. Rais wetu angekuwa bize na mambo mengine na kuicha hiyo shughuli kwa waandamizi wake???

Ifike mahali wizara ya mambo ya nje wajitafakari pia katika hili.
Jo Biden ni rafiki wa wana demokrasia tu.

Nje ya Hapo utasubiri sana hata ukikaa mwaka
 
Alikuja mke wa Bush Zanzibar, basi mawasiliano ya simu yakawa yanapotea, njia zilifungwa watu wasipite. Sometimes unaweza kuona kwanini waliweza kututawala kirahisi
 
Back
Top Bottom