Kwa hili la TBA Mhe. Magufuli umekosea!

Umentia shaka sana baada ya kumtaja E.MREMA kuwa ni mtu muadilifu aliyekumbwa na kumbakumba ya Magufuli....Kwani si ndo aliyekuwa akituhumiwa kwa ufisadi ndani TANROADS?au nimechanganya mambo!
 
Inawezekana Magufuli asiwe mkamilifu kama tulivyo binadamu wote. lakini mwandishi huyu anaonekana ama ameguswa moja kwa moja na maamuzi ya Magufuli au mtu wake wa karibu kaguswa. Isije haya nayo yakawa "majungu" kwani mtu kama Magufuli mara nyingi hufanya maamuzi sahihi ingawa yanakuwa magumu ambayo wana magamba wenzake hawayafanyi
 
TAARIFA KWA MTOA MADA!CEO WA TBA,muda wa kukaa pale umeisha tangu mwaka huu mwanzoni,na nafasi hiyo iliishatangazwa kwenye magazeti.kwa hiyo kutolewa kwake sio kuonewa hata kidogo.
<br />
<br />
inaonekana walikuwa wanatafuna wote pesa zetu ndo maana imemuuma
 
Habari imejaa chuki binafsi dhidi ya Magufuli.
<br />
<br />
hi habari co kwamba ina chuki binafsi,ila inaonekana huyu jamaa haya mambo km yalimkuta. Lakini wadau tuzingatie kwamba hakuna mtu aliyekamilika.. Magufuli,tunamjua ndio ni mchapakazi na vitu vng anavyofanya huwa ananukuu vifungu vya sheria. Lakini tufahamu pia huyu mzee ana hasira xana.. Huwa akiamua,ameamua na ni ngumu xana kuchukua ushauri akiamua kitu. Ni makosa ya kibinadamu ingawa yanawaathiri wengi ktk maamuzi yke,tumvumilie2 coz at list yeye anajituma na udhaifu wke huwa unawagharimu wachache. Hili swala la ufisadi,kinachombeba magufuli ni kuwajibika tu.. Lakini kama angekuwa mvivu cjui kama kwnye list ya magamba angekoxekana..
 
Umentia shaka sana baada ya kumtaja E.MREMA kuwa ni mtu muadilifu aliyekumbwa na kumbakumba ya Magufuli....Kwani si ndo aliyekuwa akituhumiwa kwa ufisadi ndani TANROADS?au nimechanganya mambo!

Mkuu si zilikuwa tuhuma tu, au alipelekwa mahakamani na kuhukumiwa?
 
Unfortunately Watanzania sasa hivi unataka ma-dikteta kwa hiyo nakuonea huruma ngoja wa chama cha! Waje shauri yako.
 
Unnecessarily circumlocution with obvious prejudices and hatred emotions against Magululi. Devoid of a substance and replete with animadversions, your statement explicitly evinces your grudges against Magufuli.
 
Habari imejaa chuki binafsi dhidi ya Magufuli.

Sina chuki yoyote na mhe. Magufuli. Kwanza ni kati ya viongozi wachache wenye kuthubutu ila kwangu hata kama utakuwa mzuri kiasi gani ikitokea uka-abuse sheria na taratibu huwa nashindwa kuvumilia. Cha msingi fanyeni utafiti wenu binafsi ili mjiridhishe na nyinyi. it has taken me time to have said this.
 
Na wewe "mwanitakiani", hayo yote uliyoyaeleza yakitokea ulikuwa ukifatana na magufuli bega kwa bega au ndio majungu yasiyo na mpango hayo? msituletee humu fitina zenu za kijinga. Unaelezea habari za watu kama upo nao bega kwa bega yanapotokea yote hayo? Huu ni umbea na usengenyaji wa hali ya juu.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Sijaelewa hapa, ina maana Magufuri yupo juu ya sheria? au una maana hao uliowataja ndio hawajui haki zao? na kama kumwamisha mtu kwenda Kigoma kuna ubaya gani?

Kuhusu swala la Mrema si kweli kwamba aliondolewa na Magufuri wala Magufuri hakuwa na uwezo huo ni nyie mnaoongea mambo ya mtaani ndio mnapindisha ukweli, ni kweli kuwa Mrema hakuwa na kosa lolote na pia alikuwa mtendaji mzuri lakini ujuwe kuwa muda wa mkataba wake TANROADS uliisha hata kabla ya Uchaguzi ni kwa vile Rais alisitisha mchakato wa kujaza nafasi yake ili kupisha uchaguzi hivyo ilikuwa ni lazima baada ya uchaguzi nafasi ijazwe, sheria ilikuwa inaruhusu extension ya mkataba ila tayari jamii ilikwisha potoshwa mengi juu ya Mrema na watu kama wewe wanaoongea bila kujuwa ukweli.

Unachosema hapa hakitoshi kumtoa CE wa Agency, ujuwe kuwa CEO wa Agency siyo mfanyakazi wa wakawaida wa Wizara hivyo hawezi kuamishiwa wizarani maana anafanya kazi kwa mkataba maalum, labda rudi utafute ukweli zaidi utuelete, maana hapa umechanganya ukweli na uongo kwahiyo habari nzima imekuwa uongo. Huyo CEO ama hana qualification au kuna kosa lilofanya ambalo wewe ulijui maana yeye na Magufuli wapo sawa kimadaraka na kisheria hakuna ambaye anaweza kunyea mwingine kiasi hicho kama hakuna mkondo wa sheria uliopita hapo.

Ni kweli ni Magufuri ni Bogus lakini unayosema hapa hayawezekani hata siku mmoja katika ofisi ya Umma, hata kama ungesema amemfanyia house boy wake bado ningeshangaa maana nao wana haki zao

Mkuu, hii story si ya kupika. Kilichofanyika kilikuwa ktk ofisi ya umma! nenda mwenyewe TBA au wizarani kwa waliofanya kazi na mhe. Magufuli utaambiwa behaviours zake. Mimi binafsi pamoja na kuwa tumeshafanya naye kazi kwa karibu hajanigusa, ila baadhi ya action zake ndio utata. Kwa wengi wasiomfahamu kwa karibu wataona ni 100% yupo perfect, si kweli. Unaongea kwa sababu hujapata kumjua vizuri, sikulaumu. He is capable of anything!
 
Penye blue pamenistua sana. Kuna kila dalili kwamba Magufuli amekugusa pabaya....... any way sisi masikio yetu, tutasikia akiwajibishwa maana kama kweli hafuati utawala wa sheria lazima itakula. Unajua nimejiuliza sana yaani magufuli katukana na kupiga teke milango ya serikali???????? This is too much bwana.[/QUOTE

Hapo penye blue ulipopa-cite hata mimi kwa kweli pamenishtua!! sipati picha, waziri anayeheshimika anafika kwenye ofisi halafu anapiga teke mlango huku akimwaga matusi???!!! gimme a break banaa!!! is it possible? am afraid kwamba mengi yaliyoelezwa hata kama ni ya kweli lakini yameongezwa chumvi!! Also, jinsi story yenyewe ilivyotolewa haioneshi kulenga kutoa taarifa kwa wadau bali inaonekana ni kama inayolenga kutaka kuongea mambo on behalf ya wale waliokuwa wanatakiwa kutoa kilio hicho! it sounds like mtoa mada ameathirika kutokana na kuondolewa kwa wale walioondolewa na magufuri----it's like ana maslahi nao fulani! anyway, inawezekana kilichoongelewa ni sahihi but my concern is over the tone of the writer!
 
TAARIFA KWA MTOA MADA!CEO WA TBA,muda wa kukaa pale umeisha tangu mwaka huu mwanzoni,na nafasi hiyo iliishatangazwa kwenye magazeti.kwa hiyo kutolewa kwake sio kuonewa hata kidogo.

Nafahamu unachokizungumza, walidelay hata kutangaza nafasi yake kwa kuwa anastaafu Desemba. Hoja ni staili aliyoondolewa nayo. Kwamba inatoa picha kutokana na mgogoro wa kumuonya Bw. Kapongo kwa utovu wa nidhamu imekuwa kama sababu. Na kwakuwa magufuli alitamka hadharani na ndicho kilichotokea tutaachaje kuamini kuwa ni abuse?
 
Na wewe "mwanitakiani", hayo yote uliyoyaeleza yakitokea ulikuwa ukifatana na magufuli bega kwa bega au ndio majungu yasiyo na mpango hayo? msituletee humu fitina zenu za kijinga. Unaelezea habari za watu kama upo nao bega kwa bega yanapotokea yote hayo? Huu ni umbea na usengenyaji wa hali ya juu.

Zomba mimi sina maslahi yoyote, mwenyewe pia nilipata mshtuko kwa mtu mzito kama yule kutatua matatizo kwa namna ile japo najua ndio tabia yake, ila last week alizidisha kwa sababu haikuwa siri. Nakushauri ufanye utafiti mdogo tu juu ya hilo linaloongelewa. Mtu akifanya vizuri asifiwe na akikosea akosolewe pia hata kama unampenda kiasi gani! Kwa kufanya hivyo ndio utamsaidia.
 
Kwani kuna mtu amewahi kusema Magufulu ni muadilifu? Muadilifu angesimamia wizi wa nyumba za serikali? Kuna tofauti kubwa kati ya kuwa muadilifu na kuwa mchapa kazi!
 
Zomba mimi sina maslahi yoyote, mwenyewe pia nilipata mshtuko kwa mtu mzito kama yule kutatua matatizo kwa namna ile japo najua ndio tabia yake, ila last week alizidisha kwa sababu haikuwa siri. Nakushauri ufanye utafiti mdogo tu juu ya hilo linaloongelewa. Mtu akifanya vizuri asifiwe na akikosea akosolewe pia hata kama unampenda kiasi gani! Kwa kufanya hivyo ndio utamsaidia.

Hamna cha utafiti wala nini, hayo ni majungu yasiyo na mpamgo. Hivi unakaa kufanya utafiti wa kusengenya mtu? badala ya kuwa busy kufanya utafiti wa kulisaidia taifa au kujisaidia mwenyewe> Mtaacha lini nyinyi kuwa na akili hizi mbovu na kuanza kuwa straight? kwani huko hamna wizi kweli? wizi watupu. mnaididimiza nchi kwa kufata maslahi yenu kiwizi na kusengenyana na kutiliana fitna na majungu kila kukicha, watu kama wewe hawatoki kwa sangoma kuroga wenzao. Wanasema "akumulikae mchana usiku atakuchoma", hao ndio watu kama wewe, wanaoacha kazi zao wakaanza kumulika ya watu. halafu unasema nakwenda kazini kufanya kazi kumbe anaemda kufanya umbea na kuja kulalamika JF. Huoni hata haya wala hujui vibaya? kuchunguza wenzako na kuwasengenya ni kama kula nyama ya nduguyo.
 
Kwani kuna mtu amewahi kusema Magufulu ni muadilifu? Muadilifu angesimamia wizi wa nyumba za serikali? Kuna tofauti kubwa kati ya kuwa muadilifu na kuwa mchapa kazi!

Ona na wewe nae, unatakiwa uwe Great mind na sio poor mind kwa wadhifa iliokuwa nao.

Great minds discuss ideas
Average minds discuss events
Poor minds discuss peoples

Unakuwa kama yule anaejiita mzee mwanakijiji? unasikitisha sana.
 
Magufuli hajawahi kuwa mwaminifu ndo maanaliuza nyumba za serikali mpakakwa hawala zake na mdogowe aliyekuwa shule asye na sifa za kuuziwa nyumba za serikali na sasa serikali inatumia mabilioni kwa mwaka kuwakodishia mawaziri na majaji! Kamahumjui magufuri utajua umepata waziri ni wa hovyo kuliko wote, mwonevu na katili kwa wanyonge, angalia alivyokuwa akichoma nyavu za wavuvi lakini walozitengeneza na kuziingiza hashughulikii kwa vile ni vigogo. Bora idd amini kuliko magufuli kwa kweli na fisadi wa 12 in the list of shame
unaweza kufupisha mkuu? All in all magufuli ni mtu makini sana
i dont think as you explained
anyway wakuu watasema
 
Hamna cha utafiti wala nini, hayo ni majungu yasiyo na mpamgo. Hivi unakaa kufanya utafiti wa kusengenya mtu? badala ya kuwa busy kufanya utafiti wa kulisaidia taifa au kujisaidia mwenyewe> Mtaacha lini nyinyi kuwa na akili hizi mbovu na kuanza kuwa straight? kwani huko hamna wizi kweli? wizi watupu. mnaididimiza nchi kwa kufata maslahi yenu kiwizi na kusengenyana na kutiliana fitna na majungu kila kukicha, watu kama wewe hawatoki kwa sangoma kuroga wenzao. Wanasema "akumulikae mchana usiku atakuchoma", hao ndio watu kama wewe, wanaoacha kazi zao wakaanza kumulika ya watu. halafu unasema nakwenda kazini kufanya kazi kumbe anaemda kufanya umbea na kuja kulalamika JF. Huoni hata haya wala hujui vibaya? kuchunguza wenzako na kuwasengenya ni kama kula nyama ya nduguyo.
Haya na yawe majungu hebu jibu yafuatayo:
Magufuli hakuuza nyumba za serikali hadi kwa ndugu yake alikuwa akisoma chuo kikuu na hawala yake?
Sasa hivi serikali haitumii mabilioni kulipia mahoteli mawaziri na majaji kwa maamuzi mabaya ya Magufuli?
Hakuchoma nyavu za maskini wavuvi bila kushughulikia walioziingiza au wewnye viwanda vyake?
Anayemfagilia magufuli ni yule asiyejua madikteta hutengenezwaje
 
Kwa msiomjua Magufuli mtashangaa na lazima mtamkosoa sana mtoa mada. kwa tunaomjua sina hata chembe ya kushangaa. Tatizo letu watanzania tunapelekwa na vyombo vya habari. kila media house ina mtu wake mwisho wa siku hatupati balanced story, magufuli atasifiwa wee nyuma ya pazia hamjui kitu. SWALI? HIVI ILE RIPOTI YA UUZAJI NYUMBA ZA SERIKALI BADO HAIJAKAMILIKA? mkiipata mtajua mtoa mada anamaanisha nini. Bora JF tunainteract kiukweli
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom