Kwa hili la TBA Mhe. Magufuli umekosea!

Haya na yawe majungu hebu jibu yafuatayo:&lt;br /&gt;<br />
Magufuli hakuuza nyumba za serikali hadi kwa ndugu yake alikuwa akisoma chuo kikuu na hawala yake?&lt;br /&gt;<br />
Sasa hivi serikali haitumii mabilioni kulipia mahoteli mawaziri na majaji kwa maamuzi mabaya ya Magufuli?&lt;br /&gt;<br />
Hakuchoma nyavu za maskini wavuvi bila kushughulikia walioziingiza au wewnye viwanda vyake?&lt;br /&gt;<br />
Anayemfagilia magufuli ni yule asiyejua madikteta hutengenezwaje
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Hafagiliwi mtu hapa. Kama umeona kafanya dhambi na ushahidi unaoi wa hizo dhambi, unangoja nini kwenda mahakamani? Magufuli hayuko juu ya sheria. Action speaks louder than words.

Tena kwa ushahidi kuwa hakuna aliye juu ya sheria, tumeshaona akishtakiwa waziri Maua Daftari na kashindwa kesi mahakamani. Sheria imefata mkondo wake.
 
Mkuu, hii story si ya kupika. Kilichofanyika kilikuwa ktk ofisi ya umma! nenda mwenyewe TBA au wizarani kwa waliofanya kazi na mhe. Magufuli utaambiwa behaviours zake. Mimi binafsi pamoja na kuwa tumeshafanya naye kazi kwa karibu hajanigusa, ila baadhi ya action zake ndio utata. Kwa wengi wasiomfahamu kwa karibu wataona ni 100% yupo perfect, si kweli. Unaongea kwa sababu hujapata kumjua vizuri, sikulaumu. He is capable of anything!

Siyo kuwa nabisha maneno yako la hasha! Nashangaa kwanini hao wanaofanyiwa wanakaa kimia na hawachukui hatua, Mi namjuwa na nilikwisha kusema humu mara zote kuwa si chochote.

Wanamsifia ndio waliokuwa wanamsifia Kikwete 2005 bila chembe ya ubongo.
 
Tatizo letu watanzania kiongozi akiwa anatoa matamko makali makali basi huyo huhesabiwa kama kiongozi mchapa kazi. Hebu niambie kwa sasa hivi kuna tofauti gani kiutendaji (impact kwa wananchi wa Tz) wakati Kawambwa ni waziri na sasa Magufuli. Sijaona tofauti yoyote, foleni ni ile ile, barabara ya Mandela haijaisha, barabara ya Kilwa vile vile. Ila Magufuli kisha ongea mengi(kupiga mkwara) bila matokeo yoyote.

Naunga mkono hoja ya Dr. Kitila
 
unaweza kufupisha mkuu? all in all Magufuli ni mtu makini sana<br />
I dont think as you explained <br />
anyway wakuu watasema
<br />
<br />
Umakini wa magufuli uko wapi? Anajua kupiga kelele tu na hana lolote la maana la kujivunia. Mtu makini asingeuza nyumba za serikali zilizo kwenye maeneo kama yale na kuwaambia mawaziri na viongozi wajao wakakaa manzese. Yale na maamuzi ambayo yamemuondolea magufuli umakini wowote na sifa yoyote. Tunapenda kusifia tu sababu magufuli anweza kucrame majina ya barabara na vijiji na fedha zake. He is a chemist na anao uwezo huo but that doesn't make him kiongozi wa kutukuka. Tanroads hadi sasa hakukaliki na miradi haina hela yeye kafanya nini? Kadanganya bungeni barabara ya kwenda lindi kilometa 60 pale somamga na nyamwage itaisha within the next four months. Go and see for yorself! Ile barabara haiishi hadi mwaka kesho kwani sisi ni wadau and we can estimate correctly the completion date, lakini yeye anadanganya uma kwa ajili ya kutaka sifa.
Samaki wake walienda wapi? Watu wamesota rumande miaka mingapi?
 
Bw. John Pombe Magufuli amekosea! Tumesikia mabadiliko yaliyotokea katika Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kuondolewa kwa CEO wake Bw. Makumba Kimweri na kupelekwa Wizarani. Magufuli amejizolea sifa nyingi miongoni mwa watz kama kiongozi mzuri na mchapakazi hasa kwa staili yake anayoitumia ya ufuatiliaji na udikteta. Kwani wakati mwingine sifa hiyo ni nzuri, lkn kuna nyakati inaweza pia kuleta madhara kwa sababu haizingatii utawala wa sheria (rule of law). Magufuli kwa waliofanya naye kazi kwa karibu wanaweza kukupa story tofauti na usiweze kuamini kama huyu ndiye yule Magufuli anayepambanuliwa miongoni mwa viongozi wengi kuwa ni muadilifu. La hasha! Magufuli hayupo hivyo, ni mnafiki anayevaa ngozi ya kondoo kuwahadaa Watz. Ni fisadi na mpenda majungu kupita kiasi. Magufuli anaweza kufanyia kazi hearsay as if amepewa taarifa za kweli na zilizothibitishwa, inategemea nani kawahi kumpa majungu na ni nani kwake.<br />
<br />
Kuondolewa kwa Mkurugenzi mkuu wa TBA Bw. Kimweri kulianza kama mchezo. Chokochoko ilianzia kwa mtumishi mmoja wa idara ya uhasibu Bw. Kapongo ambaye ni jamaa yake Magufuli, wengine wanasema ni mjomba wake alipopewa uhamisho kwenda Wizarani baada ya kuwepo kutoelewana na wafanyakazi wenzie. Kapongo alipopata barua ya uhamisho alianza kuwapiga mkwara wenzie kuwa wasubiri watakiona cha mtema kuni Waziri Magufuli akirudi toka bungeni, kwamba wamefanya kosa kumhamisha. Ukweli ni kwamba Kapongo hana sifa na hata wenzie wana-doubt kama ana cheti hata cha form IV tu achilia mbali cha taaluma ya uhasibu. Maana hajuwi kazi yoyote zaidi ya kusaini cheque tu, hata kuandaa vote book hafahamu!<br />
<br />
Magufuli alipoingia Dar toka bungeni Dodoma, Kapongo kwa kuujua udhaifu wa Waziri alimfuata akiwa na some docs zenye signature yake na bosi wake aitwaye Lyatuu na nyinginezo (God knows kama ni za kweli au si za kweli!) akamjaza maneno mengi sana kuwa Bosi wake Bw. Lyatuu ni mwizi sana anaiba pesa za Serikali etc. Magufuli bila kuuliza akatoa amri Kapongo arudishwe TBA na akaufuta uhamisho wake, at the same time akatoa amri kuwa kesho yake anataka Lyatuu aripoti Kigoma na Bw. Nsangalo aliyekuwa Mwanza aripoti Dar haraka sana. Bw. Kapongo aliporudishwa TBA akawatambia wenzie kuwa "si nilisema? Mmeona nini kimefanyika?". Baada ya tukio hilo ambalo Magufuli hakumshirikisha Katibu Mkuu wake wala Naibu katibu Mkuu wake, Bw. Kimweri alimuandikia barua Kapongo ya utovu wa nidhamu, kwa kitendo chake cha kuruka ngazi zote hadi kwa Waziri ilhali uongozi wa TBA haufahamu kama kulikuwa na matatizo hayo aliyodai Kapongo. <br />
<br />
Mbaya zaidi wiki iliyopita mwishoni baada ya kupokea barua toka kwa CEO wake Kimweri, Kapongo aliibeba barua hiyo na kwenda moja kwa moja kwa Magufuli kushtaki, kuwa Kimweri kamwandikia barua ya kumuonya. Magufuli bila kuuliza kitu alifunga safari hadi TBA, ambako aliingia kwa mkwara mkali, alianza kutukana kuanzia nje ya ofisi, alipofika mlangoni akafungua mlango kwa kuupiga teke. Akamaka "TBA mmejaa majizi matupu, hili lijizi likubwa liko wapi&#8230;" maneno hayo aliyaropoka mbele ya wafanyakazi waliopigwa na butwaa. <br />
<br />
Akapiga simu kwa Katibu Mkuu wake akisema akifumba na kufumbua anataka kumuona Bw. Nsangalo kakalia kiti chake. Aliendelea kubwata mbele ya wafanyakazi kuwa akiamka kesho yake Kimweri u-CEO atausikia tu. Kwakweli ilikuwa ni hali ya udhalilishaji kazini na mtu kama Magufuli kwa nafasi yake hakupaswa ku-handle situation hiyo kwa staili ya mithili ya mtu aliyepagawa.<br />
<br />
Kweli, kesho yake Magufuli akatoa amri Bw. Kimweri aondolewe TBA na kupelekwa wizarani na nafasi yake akakaimishwa msaidizi wake. Kama haitoshi sasa Magufuli anampigia debe swahiba wake aitwaye Mwakalinga ndio achukue nafasi ya Kimweri. Mwakalinga ambaye hana uwezo wa kushika nafasi hiyo jina lake kalipeleka kwenye Bodi na Bodi imekataa kupitisha jina hilo. <br />
<br />
Bodi ya wakandarasi sasa inatishia kufanya mgomo kupinga maamuzi ya kidikteta ya Magufuli. Hali si shwari tena TBA, ukali na njia anazotumia Magufuli bila utaratibu zinawafanya watu kuwa waoga, maana hawajuwi nani atasingiziwa nini wapi iwapo watatofautiana na Waziri wao. Magufuli anampigia debe Mwakalinga kwa sababu ya uswahiba walio nao na pia kwa sababu huyo Mwakalinga kwa kushirikiana na Kapongo ndio waliomjengea nyumba yake. <br />
<br />
Magufuli ili awe kiongozi mzuri inabidi afuate taratibu na sheria zilizopo, kama kuna wizi umefanyika anapaswa kuitisha Auditing team kubaini tatizo na si kukurupuka tu kwa majungu anayopelekewa na kuumiza wengine wasio na hatia. Mbona yeye mwenyewe ni fisadi? Kiongozi anayetumia nafasi yake vibaya ni ufisadi. <br />
<br />
Magufuli ameshindwa kuangalia rekodi ya utendaji kazi ya Bw. Lyatuu ambaye tangu ameshika nafasi hiyo TBA ameingiza miradi mingi na fedha nyingi kuliko alipokuwepo Bw. Nsangano (aliyerudishwa tena) aliyeiacha TBA na sh. 4m tu wakati Lyatuu ameiinua TBA kwa ukusanyaji mzuri wa madeni na kutafuta miradi inayoifanya TBA kujiendesha yenyewe. Magufuli amemrudisha Nsangalo aliyeshindwa kabla na ambaye hana PR yoyote kuwezesha TBA kupata miradi na kujiendesha. Alipohamishiwa Mwanza TBA huko imekufa, haina kitu kabisa na sasa kamrudisha Dar aiue pia.<br />
<br />
Magufuli tutamuamini vipi kuwa ni msafi baada ya kujijengea magorofa manne (4) yaliyopo kitalu 172 Upper Kinondoni, magorofa aliyojengewa kwa msaada wa Mwakalinga na Nsangalo, magorofa aliyowapangisha Wakandarasi aliowapa kazi mwenyewe! Magufuli anawezaje kufuta hisia zetu kuwa hachukuwi 10% za wakandarasi hao? <br />
<br />
Ndio maana pia Magufuli aliharakisha zoezi la kumuondoa Ephraem Mrema wa TANROADS, aliyetengenezewa zengwe na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Miundombinu by then Bw. Omar Chambo na kumpa nafasi hiyo Bw. Mfugale &#8211; swahiba wake pia. Ndio maana hadi leo TANROADS tangu aondoke Mrema bado hakujatulia. Hii ni kwasababu ya maamuzi yasiyozingatia sheria ya watawala wetu wanaoangalia interest zao kwanza. This is not health for our country's development.<br />
<br />
Magufuli anapaswa kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizopo akishauriana na subordinates wake kama Katibu Mkuu, naibu katibu Mkuu, Menejimenti, Bodi etc. alichokifanya TBA is very unethical and it is against good governance and rule of law. <br />
<br />
Kwani mtu kama Kapongo kama si majungu baada ya matukio hayo hakupaswa kumrudisha tena TBA, ambako hata yeye amechangia machafuko. Kama ni kuhamisha alipaswa ahamishe wote, kumrudisha Kapongo TBA tafsiri yake ni nini? Vyombo vinavyohusika fuatilieni hili na mtabaini mengi yaliyo nyuma ya pazia. <br />
<br />
Hayo ni maoni yangu.
<br />
<br />
Kafie mbele mnafiki mkubwa weye...unasubiri ufukuzwe wewe ndo uje na mashairi yako ili jukwaa liwe sympathetic na wizi wako. Magufuli ni waziri ambaye mziki wake wananchi wanaukubali. So far wewe kama wewe umelifanyia nini Taifa compared na Magufuli alcoholic John. Kweli watanzania wengi wanapenda viongozi nyolonyolo. Mlete mzee wako awe waziri...lakini mind you mpaka wananchi wamkubali jimboni kwake.
 
what ever we say,Magufuli amemzalilisha huyo bwana,mtu mwenyewe anaelekea kusastaafu,hapana kama upo ushahidi wa hayo matusi awajibike!hatuwezi kutetea viongozi wanaogeuka Miungu namna hii, khaaa!
 
alafu tumeshazoeshwa ufisadi hadi hatushtuki,yanatajwa maghorofa aliyonayo magufuli mnasema majungu badala ya kuomba uchunguzi!,shabaash JF People,tusipuuze tuhuma,ufanyike uchunguzi documa zimwagwe humu.
 
alafu huyu magufuli ndio moja kati ya expected tools za ccm uchaguzi ujao! Kama ndo haya this is too low for presidency,hekima muhimu bana sio kupiga teke milango ya watuhumiwa na matusi juu! Hapana aisee wakuu
 
wanitakiani... wewe wamtakiani Magufuli?

Waweza kuwa na hoja lakini nimesoma paragraph 1, nimeacha kwani ni matusi, attacks, attacks and attacks??

Ujumbe huwa haufikishwi hivyo

CHUKI ITAKUUA
 
Kwa kweli haya yana ukweli kiasi fulani hata kama mtoa mada amekuwa biased, Magufuli kwa kweli sio msafi kama anavyojionesha na kuaminiwa na Watanzania. Mimi najua uchafu wake wa kutembea na mabinti wadogo katika hosteli moja hapa Dar yaani ukimwona anatoka kwenye ufuska huo kama kanyeshewa. Yaani we acha tu.

Pia ukiongea na wafanyakazi katika wizara yake yaani watakupa stori tofauti na vile anavyojionesha mbele ya macho ya umma, na hata amewin some degree of public trust, hata wengine kumfikiria kuwa Rais au Waziri Mkuu, n.k. Watanzania fuatilieni mambo msihadaiwe kinafiki namna hii jamani.
 
Sina chuki yoyote na mhe. Magufuli. Kwanza ni kati ya viongozi wachache wenye kuthubutu ila kwangu hata kama utakuwa mzuri kiasi gani ikitokea uka-abuse sheria na taratibu huwa nashindwa kuvumilia. Cha msingi fanyeni utafiti wenu binafsi ili mjiridhishe na nyinyi. it has taken me time to have said this.
.............. oOOHPS THEN YOU HAVE WASTED YOUR TIME.......................... It has taken us no time to have known you.................. na crap zako
 
alafu tumeshazoeshwa ufisadi hadi hatushtuki,yanatajwa maghorofa aliyonayo magufuli mnasema majungu badala ya kuomba uchunguzi!,shabaash JF People,tusipuuze tuhuma,ufanyike uchunguzi documa zimwagwe humu.
Nani si gamba kule CCM..??? Tulipofikishwa ni kuchagua nani afadhari.................... Unadhani kwa nini tunamkumbuka sana Mkapa kuliko huyu JK..??? Yote ni magamba laniki kuna yenye ahueni...!!! Magufuli hoyeeeeee
 
Bw. John Pombe Magufuli amekosea! Tumesikia mabadiliko yaliyotokea katika Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kuondolewa kwa CEO wake Bw. Makumba Kimweri na kupelekwa Wizarani. Magufuli amejizolea sifa nyingi miongoni mwa watz kama kiongozi mzuri na mchapakazi hasa kwa staili yake anayoitumia ya ufuatiliaji na udikteta. Kwani wakati mwingine sifa hiyo ni nzuri, lkn kuna nyakati inaweza pia kuleta madhara kwa sababu haizingatii utawala wa sheria (rule of law). Magufuli kwa waliofanya naye kazi kwa karibu wanaweza kukupa story tofauti na usiweze kuamini kama huyu ndiye yule Magufuli anayepambanuliwa miongoni mwa viongozi wengi kuwa ni muadilifu. La hasha! Magufuli hayupo hivyo, ni mnafiki anayevaa ngozi ya kondoo kuwahadaa Watz. Ni fisadi na mpenda majungu kupita kiasi. Magufuli anaweza kufanyia kazi hearsay as if amepewa taarifa za kweli na zilizothibitishwa, inategemea nani kawahi kumpa majungu na ni nani kwake.

Kuondolewa kwa Mkurugenzi mkuu wa TBA Bw. Kimweri kulianza kama mchezo. Chokochoko ilianzia kwa mtumishi mmoja wa idara ya uhasibu Bw. Kapongo ambaye ni jamaa yake Magufuli, wengine wanasema ni mjomba wake alipopewa uhamisho kwenda Wizarani baada ya kuwepo kutoelewana na wafanyakazi wenzie. Kapongo alipopata barua ya uhamisho alianza kuwapiga mkwara wenzie kuwa wasubiri watakiona cha mtema kuni Waziri Magufuli akirudi toka bungeni, kwamba wamefanya kosa kumhamisha. Ukweli ni kwamba Kapongo hana sifa na hata wenzie wana-doubt kama ana cheti hata cha form IV tu achilia mbali cha taaluma ya uhasibu. Maana hajuwi kazi yoyote zaidi ya kusaini cheque tu, hata kuandaa vote book hafahamu!

Magufuli alipoingia Dar toka bungeni Dodoma, Kapongo kwa kuujua udhaifu wa Waziri alimfuata akiwa na some docs zenye signature yake na bosi wake aitwaye Lyatuu na nyinginezo (God knows kama ni za kweli au si za kweli!) akamjaza maneno mengi sana kuwa Bosi wake Bw. Lyatuu ni mwizi sana anaiba pesa za Serikali etc. Magufuli bila kuuliza akatoa amri Kapongo arudishwe TBA na akaufuta uhamisho wake, at the same time akatoa amri kuwa kesho yake anataka Lyatuu aripoti Kigoma na Bw. Nsangalo aliyekuwa Mwanza aripoti Dar haraka sana. Bw. Kapongo aliporudishwa TBA akawatambia wenzie kuwa “si nilisema? Mmeona nini kimefanyika?”. Baada ya tukio hilo ambalo Magufuli hakumshirikisha Katibu Mkuu wake wala Naibu katibu Mkuu wake, Bw. Kimweri alimuandikia barua Kapongo ya utovu wa nidhamu, kwa kitendo chake cha kuruka ngazi zote hadi kwa Waziri ilhali uongozi wa TBA haufahamu kama kulikuwa na matatizo hayo aliyodai Kapongo.

Mbaya zaidi wiki iliyopita mwishoni baada ya kupokea barua toka kwa CEO wake Kimweri, Kapongo aliibeba barua hiyo na kwenda moja kwa moja kwa Magufuli kushtaki, kuwa Kimweri kamwandikia barua ya kumuonya. Magufuli bila kuuliza kitu alifunga safari hadi TBA, ambako aliingia kwa mkwara mkali, alianza kutukana kuanzia nje ya ofisi, alipofika mlangoni akafungua mlango kwa kuupiga teke. Akamaka “TBA mmejaa majizi matupu, hili lijizi likubwa liko wapi…” maneno hayo aliyaropoka mbele ya wafanyakazi waliopigwa na butwaa.

Akapiga simu kwa Katibu Mkuu wake akisema akifumba na kufumbua anataka kumuona Bw. Nsangalo kakalia kiti chake. Aliendelea kubwata mbele ya wafanyakazi kuwa akiamka kesho yake Kimweri u-CEO atausikia tu. Kwakweli ilikuwa ni hali ya udhalilishaji kazini na mtu kama Magufuli kwa nafasi yake hakupaswa ku-handle situation hiyo kwa staili ya mithili ya mtu aliyepagawa.

Kweli, kesho yake Magufuli akatoa amri Bw. Kimweri aondolewe TBA na kupelekwa wizarani na nafasi yake akakaimishwa msaidizi wake. Kama haitoshi sasa Magufuli anampigia debe swahiba wake aitwaye Mwakalinga ndio achukue nafasi ya Kimweri. Mwakalinga ambaye hana uwezo wa kushika nafasi hiyo jina lake kalipeleka kwenye Bodi na Bodi imekataa kupitisha jina hilo.

Bodi ya wakandarasi sasa inatishia kufanya mgomo kupinga maamuzi ya kidikteta ya Magufuli. Hali si shwari tena TBA, ukali na njia anazotumia Magufuli bila utaratibu zinawafanya watu kuwa waoga, maana hawajuwi nani atasingiziwa nini wapi iwapo watatofautiana na Waziri wao. Magufuli anampigia debe Mwakalinga kwa sababu ya uswahiba walio nao na pia kwa sababu huyo Mwakalinga kwa kushirikiana na Kapongo ndio waliomjengea nyumba yake.

Magufuli ili awe kiongozi mzuri inabidi afuate taratibu na sheria zilizopo, kama kuna wizi umefanyika anapaswa kuitisha Auditing team kubaini tatizo na si kukurupuka tu kwa majungu anayopelekewa na kuumiza wengine wasio na hatia. Mbona yeye mwenyewe ni fisadi? Kiongozi anayetumia nafasi yake vibaya ni ufisadi.

Magufuli ameshindwa kuangalia rekodi ya utendaji kazi ya Bw. Lyatuu ambaye tangu ameshika nafasi hiyo TBA ameingiza miradi mingi na fedha nyingi kuliko alipokuwepo Bw. Nsangano (aliyerudishwa tena) aliyeiacha TBA na sh. 4m tu wakati Lyatuu ameiinua TBA kwa ukusanyaji mzuri wa madeni na kutafuta miradi inayoifanya TBA kujiendesha yenyewe. Magufuli amemrudisha Nsangalo aliyeshindwa kabla na ambaye hana PR yoyote kuwezesha TBA kupata miradi na kujiendesha. Alipohamishiwa Mwanza TBA huko imekufa, haina kitu kabisa na sasa kamrudisha Dar aiue pia.

Magufuli tutamuamini vipi kuwa ni msafi baada ya kujijengea magorofa manne (4) yaliyopo kitalu 172 Upper Kinondoni, magorofa aliyojengewa kwa msaada wa Mwakalinga na Nsangalo, magorofa aliyowapangisha Wakandarasi aliowapa kazi mwenyewe! Magufuli anawezaje kufuta hisia zetu kuwa hachukuwi 10% za wakandarasi hao?

Ndio maana pia Magufuli aliharakisha zoezi la kumuondoa Ephraem Mrema wa TANROADS, aliyetengenezewa zengwe na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Miundombinu by then Bw. Omar Chambo na kumpa nafasi hiyo Bw. Mfugale – swahiba wake pia. Ndio maana hadi leo TANROADS tangu aondoke Mrema bado hakujatulia. Hii ni kwasababu ya maamuzi yasiyozingatia sheria ya watawala wetu wanaoangalia interest zao kwanza. This is not health for our country’s development.

Magufuli anapaswa kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizopo akishauriana na subordinates wake kama Katibu Mkuu, naibu katibu Mkuu, Menejimenti, Bodi etc. alichokifanya TBA is very unethical and it is against good governance and rule of law.

Kwani mtu kama Kapongo kama si majungu baada ya matukio hayo hakupaswa kumrudisha tena TBA, ambako hata yeye amechangia machafuko. Kama ni kuhamisha alipaswa ahamishe wote, kumrudisha Kapongo TBA tafsiri yake ni nini? Vyombo vinavyohusika fuatilieni hili na mtabaini mengi yaliyo nyuma ya pazia.

Hayo ni maoni yangu.

Nafikiri hii habari imeandikwa kwa hisia sana.Tena imeegemea upande mmoja wa kulaumu tuu.Kwa sababu haijaainisha ni mazuri gani ambayo makufuli kafanya mpaka utuaminishe kwamba tunafikiri mtu mzuri kumbe sivyo..Lakini pia inaonyesha umehisi sababu unasema jamaa wanamjaza maneno,siamini kama una uhakika labda ungetuweka wazi kama walivyokuwa wanakwenda kwa makufuli walikuwa wanakuaga kuwa wanakwenda kumwajaza maneno..Pia tunataka kujua ufanisi wa hao unao waona ni bora kwako na uhusiano wako na wewe..Gomeni tupo watu wengi sana wenye uwezo wa kuja kufanya kazi TBA,..au vijana wa field huwaona.hawana pa kwenda.Lakini pia makufuli ni binadamu anaweza kuwa na mapungufu yake ,,,UKweli Makufuli ni moja ya VIONGOZI bora kwa SASA,wenye maslahi binafsi kuzidi maslahi ya UMMA huyu sio rafiki yao..MAKUFULI kuwa raisi WANGU.
 
Nafikiri hii habari imeandikwa kwa hisia sana.Tena imeegemea upande mmoja wa kulaumu tuu.Kwa sababu haijaainisha ni mazuri gani ambayo makufuli kafanya mpaka utuaminishe kwamba tunafikiri mtu mzuri kumbe sivyo..Lakini pia inaonyesha umehisi sababu unasema jamaa wanamjaza maneno,siamini kama una uhakika labda ungetuweka wazi kama walivyokuwa wanakwenda kwa makufuli walikuwa wanakuaga kuwa wanakwenda kumwajaza maneno..Pia tunataka kujua ufanisi wa hao unao waona ni bora kwako na uhusiano wako na wewe..Gomeni tupo watu wengi sana wenye uwezo wa kuja kufanya kazi TBA,..au vijana wa field huwaona.hawana pa kwenda.Lakini pia makufuli ni binadamu anaweza kuwa na mapungufu yake ,,,UKweli Makufuli ni moja ya VIONGOZI bora kwa SASA,wenye maslahi binafsi kuzidi maslahi ya UMMA huyu sio rafiki yao..MAKUFULI kuwa raisi WANGU.
MWELEZE HUYO............ Kuna watu kama akina Nyerere, Mandera hadi leo hii tunawasifia lakini si kwamba hawakuwa na makosa.......... Nyerere alishawahi kukiri kuwa si kwamba serikali yake ilifanya mazuri tu.... la hasha...... TATIZO LETU SISI TUNAIGA MABAYA NA KUYAACHA MAZURI
 
Tupe mafanikio ya TBA kwanza ndani ya 10miaka iliyopita ili tujue ufanisi wa aliyerudishwa wizarani
 
<br />
<br />
Umakini wa magufuli uko wapi? Anajua kupiga kelele tu na hana lolote la maana la kujivunia. Mtu makini asingeuza nyumba za serikali zilizo kwenye maeneo kama yale na kuwaambia mawaziri na viongozi wajao wakakaa manzese. Yale na maamuzi ambayo yamemuondolea magufuli umakini wowote na sifa yoyote. Tunapenda kusifia tu sababu magufuli anweza kucrame majina ya barabara na vijiji na fedha zake. He is a chemist na anao uwezo huo but that doesn't make him kiongozi wa kutukuka. Tanroads hadi sasa hakukaliki na miradi haina hela yeye kafanya nini? Kadanganya bungeni barabara ya kwenda lindi kilometa 60 pale somamga na nyamwage itaisha within the next four months. Go and see for yorself! Ile barabara haiishi hadi mwaka kesho kwani sisi ni wadau and we can estimate correctly the completion date, lakini yeye anadanganya uma kwa ajili ya kutaka sifa.
Samaki wake walienda wapi? Watu wamesota rumande miaka mingapi?
John alcohol Makufuli anabaki kiongozi BORA kwa sasa..Na ni lazima ana maadui wengi tuuu,,Tunaomuunga mkono ambao ni watanzania wengi tunajua kuwa wapo walionja joto ya makufuli hawakuishia hapo HAWAMPENDI wao na FAMILIA zao,pia inawezekana wapo ambao aligombana nao kwa mambo binafsi hawawezi KUMPENDA wapo ambo plan zao haziendi sababu yupo BWANA makufuli...sasa wewe utatuambia nini? CHUKI ZAKO ZITAKUUA...eti samaki SASA kosa lake nini,WATU WAMEKAMATWA na operation yake wapo mahakamani,samaki wanafunzi na watoto yatima walikula.SERIKALI inajua kwenye kina kina fulani kuna jodari,SAS UNATAKA makufuli awe JUDGE,MVUVI,na kila kitu.na utakufa kwa roho yako...WATU WENGI WANAMPENDA na WANAMPA SAPOTI YA KUTOSHA.
 
Mimi siku zote, nasema Magufuli is not coming clean! Hata kama kwa hili mtu katunga lakini ana mapungufu mengi. Kuna wakati alimtukana aliyekuwa anakaimu ukurugenzi TEMESA kwa kumwambia mtu aliyekondeana kama yeye hawezi kuwa mkurugenzi na hiyo alitamka mbele ya wafanyakazi wote.
Nadhani anahitaji kuelimishwa kuhusu uongozi bora, maana bila mtu wa chini wa juu pia hawezi kubakia pale. Kama anabagua wafanyakazi kwa maslahi binafsi inabidi sasa naye apishe wengine.
Hata hivyo vyombo vya usalama na PCCB vifanye kazi yao vizuri na kubainisha wizi wa TBA na kama kuna walioiba basi wachukuliwe hatua za kinidhamu na siyo kuhamishwa vituo vya kazi.
Bado nakumbuka hasara ya mabilioni kutokana na samaki wa Magufuli na wameshindwa kuwatia hatiani wavuvi mpaka leo hii.
Usitishaji ovyo wa mikataba uliigharimu nchi mbailioni ya fedha na zinalipwa kimya kimya kama haya ya Dowans.
 
Wakuu aliyosema mdau hapo yana ukweli na chumvi kidogo. ni kweli kabisa kila alichosema ndio Magufuli amefanya ila suala la kuwa eti kina Kimweri na Lyatuu ni wachapa kazi ni uongo tu inaonekana nae ameguswa. Hawa walikuwa na mtandao wa kula hela kuanzia wizarani na sehemu ya kuzitolea ilikuwa kwenye miradi ya TBA iliyo chini ya Lyatuu DSM. wanatenga pesa nyingi sana na hakuna kinachifanyika. Kimweri mwenyewe anajengwa nyumba na TBA mkoa for sure!! hawatumii makandarasi wanasema false account na wanatumia mafundi tu, the accountability wapi. Huyo Kapongo nae alikuwa anashiriki kwenye ulaji ila shida imekuja baada ya kutofautiana na Lyatuu.Wote ni wezi kuanzia whitsle blower hadi watuhumiwa, ifanyike auditing rahisi tu na CAG waone. mbaya zaidi watu wa CAG wakienda kukagua na walikuwa wanalambishwa sukari. kifupi ndio hivyo. I will b back
 
Ni vita vilevile vinaendelea katika Serikali yetu hii. Ukweli makundi yaliyopo na yalivyojikita ktk Utumishi huo wa umma, ni kama vile kutu kali ktk kisu. Kuna jambo hapo kama ni kweli yametokea yaliyotokea. Nina uhakika wataalamu watatuletea ukweli hapa.
 
Back
Top Bottom