Wana-JF!
Kama mtakumbuka, wabunge wote wa CHADEMA hawakuweza kuhudhuria vikao vya bunge kwa wiki nzima hii kwa sababu kubwa kwamba wameguswa na tukio la mlipuko Arusha, hivyo iliwalazimu waende kwenye msiba wa wahanga kwenye ajali hiyo.
Kwa kuacha kwao kujadili bajeti kuu ya serikali, kwa mtu mwenye moyo wa huruma atasema kweli hili tukio limeathiri sana wabunge wa CHADEMA, na mtu anaweza kutoa credit kwa wabunge hao kuwa ni wazalendo.
Lakini kuna mtu mmoja ambae ni mkubwa kimadaraka huko CHADEMA, nae ni Dr Slaa, huyu yupo Germany kwa ziara anayoijua mwenyewe, lakini ni ukweli usiopingika kuwa bunge ni bora kuliko ziara ya Dr Slaa huko Germany, kwani bunge ni suala la kitaifa.
USANII UKO WAPI SASA?
Hapa unaweza kuona, kama kweli Dr Slaa ameguswa na tukio hili la mlipuko basi ni wazi angesitisha mara moja ziara yake na kuja kujumuika na wenzake katika mazishi!
Kama ambavyo wabunge wa CHADEMA walivyo jenga hoja kuwa, hawawezi kukaa bungeni huku chama chao kikiwa na tatizo hilo kubwa la mlipuko wa bomu.
Dr Slaa, kweli umeguswa na mlipuko wa bomu kama ulivyo eleza kwenye taarifa ya pole? kama ni hivyo, umewezaje kubaki Ulaya huku chama chako kikiwa kwenye wakati mgumu?
Kama mtakumbuka, wabunge wote wa CHADEMA hawakuweza kuhudhuria vikao vya bunge kwa wiki nzima hii kwa sababu kubwa kwamba wameguswa na tukio la mlipuko Arusha, hivyo iliwalazimu waende kwenye msiba wa wahanga kwenye ajali hiyo.
Kwa kuacha kwao kujadili bajeti kuu ya serikali, kwa mtu mwenye moyo wa huruma atasema kweli hili tukio limeathiri sana wabunge wa CHADEMA, na mtu anaweza kutoa credit kwa wabunge hao kuwa ni wazalendo.
Lakini kuna mtu mmoja ambae ni mkubwa kimadaraka huko CHADEMA, nae ni Dr Slaa, huyu yupo Germany kwa ziara anayoijua mwenyewe, lakini ni ukweli usiopingika kuwa bunge ni bora kuliko ziara ya Dr Slaa huko Germany, kwani bunge ni suala la kitaifa.
USANII UKO WAPI SASA?
Hapa unaweza kuona, kama kweli Dr Slaa ameguswa na tukio hili la mlipuko basi ni wazi angesitisha mara moja ziara yake na kuja kujumuika na wenzake katika mazishi!
Kama ambavyo wabunge wa CHADEMA walivyo jenga hoja kuwa, hawawezi kukaa bungeni huku chama chao kikiwa na tatizo hilo kubwa la mlipuko wa bomu.
Dr Slaa, kweli umeguswa na mlipuko wa bomu kama ulivyo eleza kwenye taarifa ya pole? kama ni hivyo, umewezaje kubaki Ulaya huku chama chako kikiwa kwenye wakati mgumu?