Daraja la tatu kwenye ndege???
Unadhani ni treni la Kigoma?
Usichokijua bro usikivalie njuga!
Kwa ufahamu wako tu:-
Ndege zinazokuja TZ za Emirates zina Business Class na Economy class.
Abiria anakadiriwa kuwa kilo 75 kwa viwango vya kimataifa.
Kiti cha abiria kina vipimo na umadhubuti maalum usiozidi kiwango fulani. Kwa unene wa marehemu, asingeweza kufit kwenye kiti, na cha muhimu zaidi, mkanda (seat belt) usingemtosha. Haiwezekani ... HAIWEZEKANI ... kuunganisha viti viwili au vitatu katika row moja akalie mtu mmoja, kwa usalama!
Ikitokea abiria amepata madhara yeyote yale na amezidi viwango basi sakata lote litamwangukia rubani, kwa vile insurance haitolipa!!!
Umeipata mkuu?? Usibishe kama uko kijiweni, sema ambacho una uhakika nacho.