Naomba nikueleweshe kidogo ndugu yangu since this is my carrier,IATA (inter carrier Agreement on passanger liability 1995)
Katika sheria za kimataifa za usafirishaji wa anga(international law of carriage) sheria mama itakayotumika katika kesi ni MONTREAL CONVENTION 1999 ambayo ilikuwa amended from WARSAW 1929 The hague protocal,Montreal protocal 123,Montreal 4 then Guadarajara,Guatamara za mwaka 1961 na 1971 then ndo ikaja hiyo Montreal ambayo inatumika hadi leo kweye hii convention passenger amelindwa kwenye mambo yafuatayo death on board,injury,delay,loss na vitu vingine vingine bt katika hizi sheria carrier anayohaiki yakujua descriptions za mzigo atakao usafirisha kabla ya safari hapa sheria zinaongelea abnormal cargo or dangerous cargo so kama carrier akupewa taarifa mapema kuwa mtu anayemsafirisha ni wa aina gani hapo hana kosa kuamkataa tatizo kubwa lilikuwa ni kama angemkubali na angefia ndani ya ndege shirika lingekuwa liable to pay more than ,113,100SDRS kama article 21 inavyoeleza so emirate walikuwa sahii kisheria japokuwa kibinadamu hawakuwa sahii.NAKARIBISHA WOTE WENYE UTATA WA KISHERIA NA HIZI INTERNATIONAL AIR LINE kwa ushauri wa kisheria bila malipo yoyote just ni pm tu.
Umeeleweka vizuri saana mkuu.
Kwa kuongezea tu kwa upande wa utaalam wa uendeshaji wa ndege
(Technical operations), nako kuna sheria mama zinazosimamia ujenzi na matumizi ya kila kifaa au kitu unachokiona kwenye ndege.
Kabla ndege haijakuwa certified kuchukua abiria ni LAZIMA vigezo na tests zote zipitishwe chini ya mamlaka ya nchi ijengayo.... Kama FAA, kwa Marekani, CAA ya Uingereza au JAR ya nchi za ulaya etc.
Falsafa mama, ni kuhakikisha usalama wa hali ya juu kabisa wa chombo na abiria. Kiti cha abiria wa ndege kinapitia tests za kila aina kuhakikisha umadhubuti wake na usalama katika matumizi pindi inapotokea ajali. Yaani hata kile kitambaa chake, huwezi kwenda Buguruni tu ukanunua ukaweka, ni vitambaa maalum vyenye uwezo wa kuvumilia moto hadi kiwango fulani. Kiti kina uwezo unaoeleweka kutozidi kilo 110 + au - 33%.
Hiyo na tests nyingine nying tu kikipita ndio huruhusiwa kufungwa kwenye ndege za ABIRIA ..... (PUBLIC TRANSPORT AIRCRAFT)
Nadhani hadi hapo utaelewa kwa nini rubani aliona kwa usalama wa marehemu, na abiria wengine haikuwa busara kumbeba abiria ambae amezidi viwango vya kubebeka.
Nilisha andika mwanzoni, kama rubani angelazimisha tu, kama kungetokea dharura yeyote, shirika lingewajibika na Insurance labda isingelipa. Na rubani atakuwa kajiweka mashakani kikazi.
Mungu amweke pema marehemu, lakini hili liwe fundisho kwa tuliobaki. Tusi assume kuwa kwa vile una pesa ya kulipia, sio kila kitu au mtu atchukuliwa na ndege. Ziko sheria zake na si za kawaida!