Kwa failed system kama ya CCM ni kwamba Serikali haiendesheki na si hujuma

Unaweza ukawa na chembe chembe ndogo sana za hoja, lakini kwa hivi vyama vya Kichagga , Ccm bado inahitajika sana. CCM ni chama kizuri sana kilikuwa kinaharibiwa na Mafisdi na wale walioamini CCM ni wao na wao ndiyo CCM. Magufuli anarudisha hadi ya CCM, itachukua muda sana Upinzani huu wenye mrengo wa Ukabila, Udini na Ukanda kuiondoa CCM madarakani. Siyo mtazamo wangu, ni mtazamo wa Watanzania walio wengi. Ndivyo wasemavyo makazini, vijiweni, kwenye mikusanyiko ya starehe n.k.
Namimi huo ndio mtazamo wangu...vyama vya kichaga vitakaa sana benchi Ikulu itaendelea kuwa ya CCM kwa miaka milioni 2.
 
Ipi system ya chama gani wewe unaona ni succesfull na hayo mafanikio yameoneka
Wapi
ul
Hivi unamjibu vipi mtu anayekuuliza...UNITIBU TB unadhani ugonjwa gani mwingine una afadhali? CCM sio chama cha siasa, ni mfumo fulani unaotaka miliki maisha ya kila raia kwa mgongo wa siasa. Uliza lini CCM ilisajiliwa rasmi km chama cha siasa?Sasa hivi ndio wanajiita chama cha siasa.
 
Mwaka jana ulikuwa ni wakati muafaka sana kwa upinzani kusimama na kuwaeleza wananchi ni suluhisho lipi mbadala walilonalo, ili CCM iweze kuonekana imepitwa na wakati. Bahati mbaya sana kwa upinzani wakashindwa kuja na mawazo mbadala, wakashindwa kujenga hoja kwa vitendo ili wananchi wengi waweze kusema huu ni muda muafaka wa kuondokana na CCM.

JPM kupiga pushup jukwaani ulikuwa ni ujumbe mzito sana wa kisiasa, alionyesha watu kwamba mimi ninafanya hivi sasa mwambieni yule wa upande wa pili afanya kama nilivyofanya. Siku zote mpiga kura hutakiwa kuiona nuru ya matumaini kwa mgombea wa urais. Kati ya JPM na EL ni JPM aliyekuwa na nuru, aliyekuwa amebeba matumaini kwa maana halisi ya neno hilo. Ndio maana mwaka 2008 Barack Obama akaja na kauli mbiu ya Change, na alifanana na hayo mabadiliko.

Uchaguzi wa mwaka jana na matokeo yake ni somo tosha kabisa kwa upinzani, ni lazima wajipange ili waweze kupata mgombea mwenye nuru ya kweli, na sio kumtegemea mtu ambaye badala ya kuleta taswira ya change, anaanza kuwafanya watu wamuonee huruma. Kura za mahaba ni kitu kimoja, kusimamia mabadiliko na kuweza kuyaelezea kwa kirefu ni kitu kingine.
tehteh kura za mahaba...
 
Bado unazungusha mikono Nicholas umebaki nyuma sana Mbowe Kiongozi wako 2014 alisema wanaibadili Chadema toka kuwa chama cha harakati kua chama cha Siasa, Lowasa juzi hapa kasema anaibadili Chadema kutoka Harakati kua chama cha siasa ili atakapogombea urais iwe heri kwake.

Pokea ushauri badilikeni ktk chama chenu kupokea Amri toka kwa Mtei na Mbowe hata CCM wameacha siasa za Zidumu fikra za mwenyekiti.
Kwa akili yako KUHAMA TOKA KTK HARAKATI =HARAKATI NI MBAYA.
 
Kwa akili yako KUHAMA TOKA KTK HARAKATI =HARAKATI NI MBAYA.

Kumbe tunazungumza na Mtu asiye na utambuzi pole sana, kwa ufupi Chadema ni NGO siyo chama cha siasa ndiyo maana ilijiunga na NGO nyingine zisizojua kufanya uchaguzi CUF, NCCR na NLD lini walichaguana toka kuanzishwa.
 
pole sana, hata Saudi Arabia inawakamata, Iran, Iraq, Uturuki, Urusi, Uchina, na Tanzania pia tunawakata. Hiyo jumla inakupa UBEPARI? katibu huo ugonjwa unaoambukizwa na CCM. Ukisoma hapo juu na hichi ulichoandika ndio utaona ujamaa unawaandaa watu kuwa magaidi kwa zaidi ya 80%, wewe hapo bado kidogo tuu ukipigwa starter utakuwa iraq ukipigania kitu usichokijua utakifia lini na kikoje . Hiyo kutu ya ujamaa huwa ni road to nowhere.
Ubepari hauna wema kama unavyojaribu kuutetea. Sio huu uchwara tulionao hapa bongo, watu wanaonekana matajiri lakini wakifuatwa na jamaa wa TRA wanaanza kuwakimbia.

Wewe huujui ujamaa, umesimuliwa na hao waliokusimulia wala hukuwaelewa vizuri na hukujaribu hata kuwauliza maswali ili uelewa wako uweze kukua.
 
Kumbe tunazungumza na Mtu asiye na utambuzi pole sana, kwa ufupi Chadema ni NGO siyo chama cha siasa ndiyo maana ilijiunga na NGO nyingine zisizojua kufanya uchaguzi CUF, NCCR na NLD lini walichaguana toka kuanzishwa.
Haha..Wewe ndio unathibiitisha posting zangu nyingi tuu. HUWA NASEMA CCM NDIO CHAMA PEKEE KINAWEZA TUNGA UONGO UNAOTOSHA KUWADHURU WAO WENYEWE. Si wewe tuu unayeweza amini unayoasema, hata hapa kazi ktk hotuba zake huwa anarudia maneno yenye maana kuna vyama vyenya haya hapa na ni tishio kwa ccm?Kwa ujumla mnaweza amini haya yote kwa pamoja na bado mkajiona mna akili timamu.

1. Chadema ni chama cha kikanda.
2. Chadema ni NGO.
3. Chadema ni chama cha Kikristu.
4. Msaijli wa Vyama vya Siasa kafanya kazi yake vizuri chini ya ccm.Na report zao za ukaguzi zip sawa.
5. Msajili wa NGO yupo sahihi.
6.Msajili wa NGO hana CDM ktk list.
7. CDM inahubiri dini .
8. CDM ina watu wa dini zaidi ya moja .
9.Msajili wa vyama vya siasa anatoa cheti kwa NGO pia.

etc

Unadhani ni wewe pekee umewekwa nje ya milembe ktk hii nchi?Kwa sababua CCM inafikiri hii nchi ni ward kubwa sana ya vichaa. Ndio maana wanajipa kila jukumu la kuwasaidia watu kufikiri, kuwapanagia kila kitu km vichaa wengine.
 
Ubepari hauna wema kama unavyojaribu kuutetea. Sio huu uchwara tulionao hapa bongo, watu wanaonekana matajiri lakini wakifuatwa na jamaa wa TRA wanaanza kuwakimbia.

Wewe huujui ujamaa, umesimuliwa na hao waliokusimulia wala hukuwaelewa vizuri na hukujaribu hata kuwauliza maswali ili uelewa wako uweze kukua.
Sipo kutete ubepari, ila kuwaambia watz ugonjwa ni ujamaa na CCM ndio mikono yake.Una chochote cha kuwatetea wajamaa na madhara waliyokupatia.
 
Sasa Magu akipewa uenyekiti wa ccm ndo atajua figisu figisu za chama chake, watakapokuwa wanamzungusha kama pia!
I cant wait kuona kihoro atakachopata
 
Sipo kutete ubepari, ila kuwaambia watz ugonjwa ni ujamaa na CCM ndio mikono yake.Una chochote cha kuwatetea wajamaa na madhara waliyokupatia.
Hujui unachokiongea, katiba inasema hii ni nchi ya kijamaa lakini practically hakuna ujamaa, cha ajabu ni kwamba unaandika mambo ambayo huwezi hata kuyafafanua kwa faida ya mjadala.
Uwekezaji mwingi sana unafanyika ni jukumu langu mimi na wewe kujua ni wapi tuwekeze. Kunyooshea kidole CCM wakati hujachukua hatua yoyote ile ya kupambana na umasikini wako ni kupoteza muda.
Kuna fursa kibao tu za kupiga hatua, usitegemee CCM ikufuate nyumbani kwako na kukwambia fanya biashara fulani na utapata faida, idea inaanzia kwako binafsi. Usipoteze muda kwa kujifariji kwa kutegemea lawama. Vijana wenye umri mdogo kuliko wewe wanatoka kimaisha hapa hapa bongo, wewe umekwama kwenye akili za lawama. Badilika ndugu yangu.
 
Sasa ndo umeandika nini? Tehetehetehetehe. Wapinzani bana! Kila siku mnahangaika na makapi ya CCM
Mi huwa nacheka kuona ccm wanakupa buku 7 halaf unaenda kujiunga na kifurushi cha chuo halaf unashinda hapa kutetea chama kilichokufa...mlimtegemea magu awaokoe..lakini amefeli kwa haraka sana mpaka anatia huruma..
 
Unasikitisha sana, kwa sababu wewe mwenye thread umeachana na hoja unaanza kuandika mambo yasiyohusiana na thread yako mwenyewe!!. Mlitaka mabadiliko kwa kutumia mwanasiasa ambaye alipaswa kuondoshwa na mabadiliko!!.
Mlitaka kutuingiza chaka baya sana, mlikosa strategies nzuri, jipangeni upya.
Kama hivi bandari mmevuruga mizigo hakuna mtapata wapi kodi sukari mmepandisha bei na haipatikani kazi zimesimama elimu bure utapata wapi?
 
Ni mashudu wala sio pumba. Jamaa amekwama kwenye akili za kipuuzi za lawama. Vijana wadogo wanafanya kweli humu humu Tanzania yeye kakalia ujinga wa kusema fulani ndio tatizo.
Sasa hujui unachoongea.Thread imeweka wazi nani analalamika. Sasa umehama kwamba sio wewe na sick CCM yao ndio mnalia kuhujumiwa?

Mgonjwa kweli, huko kwenu unaitwa kichwa km utani ukadhani ni kweli una akili nje ya nyumbani kwenu.Ndio ukajiingiza kichwa kichwa. Vichaa wakijamaa ni hopeless kweli, kila kitu ni cha maonyesho hata huu ubishi kwako ni w amaonyesho hakuna unachojifunza.
 
Ubepari anaouzungumzia Nicholaus ni unyama wa hali ya juu. Marekani imewakamata vijana wa kiarabu na kuwatesa Guantanamo Bay kwa miaka mingi, mwisho wanawaachia bila ya ushahidi kama kweli walikuwa ni magaidi.

Marekani inawadanganya kina Nico kwamba yenyewe haihusiki na chanzo cha ugaidi bali inapambana na madhara yake!. Juzi juzi Obama amekiri kwamba Marekani ilihusika katika kuifanyia ukatili Libya mpaka Gaddafi akauwawa kikatili.

Awamu ya tano itawanyoosha sana watu wenye akili za Nico, wasiofahamu kuwa misingi ya ubepari wa magharibi ilichukua miaka mingi kuweza kuwekwa, wanataka watanzania waingie kichwakichwa katika kucopy na kupaste mambo ambayo hawayajui vizuri.

Kila biashara kubwa inayohusisha mabepari ni lazima iwe na faida kwao kwanza. Migodini kuna wazungu ambao huko Ulaya walikuwa wafungwa lakini matajiri wa kimarekani na kicanada wakaongea na serikali zao ili hao wafungwa waje kufanya kazi afrika, kwani watapata pato halafu mlundikano wa wafungwa wa huko kwao utapungua.

Nico usiwathamini sana mabepari, lazima uwe na pride yako, lazima uwe na kiburi chako ambacho kinakuwa ni identity yako kila uendako.

Hiyo ya migodini ndg ni bonge la strategy lakini ni kweli? Au propaganda zao!!
 
Kama hivi bandari mmevuruga mizigo hakuna mtapata wapi kodi sukari mmepandisha bei na haipatikani kazi zimesimama elimu bure utapata wapi?
Mkuu CCM ni uzao wa upumbavu wa kijamaa.Huwa wanazama ktk chain ya problems, kwa akili zao huwa hawajui wapi pana shida.Km wajenzi wa mnara wa babeli. Wao ktk kusikia habari nzuri na kugombania wako mstari wa kwanza ktk utendaji ndio wendawazimu ktk plan unaonekana.
 
Kama hivi bandari mmevuruga mizigo hakuna mtapata wapi kodi sukari mmepandisha bei na haipatikani kazi zimesimama elimu bure utapata wapi?
Mkuu kwanini unasema Bandari imevurugwa? Ina maana ulikuwa unafuraia ujinga ulikuwa unafanyika pale?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom