VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Ukweli lazima usemwe. Bunge hili la sasa limepatikana kimagumashi sana. Ni zao la 'uchafuzi mkuu' wa mwaka 2020. Wapo Wabunge waliopita bila kupingwa kutokana na sarakasi zilizochezwa na CCM yetu na serikali katika mchakato mzima wa kiuchaguzi. Yakafuata 'madhila' makubwa wakati wa kampeni na hata siku ya kupiga kura. Mwisho wa yote, ni 'matokeo' yaliyotangazwa. Hakukuwa na haki iliyoonekana wala kuzingatiwa wakati wa uchaguzi wa 2020.
Ilikuwa wazi, kimaneno na kimatendo, kuwa Mwendazake alipania 'kuumaliza' upinzani Bungeni kwa namna yoyote ile kwenye uchaguzi wa 2020. Ndiyo maana uchaguzi ukawa uchafuzi. Alifanikiwa. Wapinzani wakasambaratishwa vya kutosha na kutisha. Baadaye, (kwakuwa ni kama nchi ilirudi kwenye mfumo wa chama kimoja kwenye macho ya kimataifa) ikaagizwa watengenezwe 'wapinzani' Bungeni. Wakapatikana akina Halima Mdee maarufu kama C...-19.
Kutokana na upatikanaji wake, Bunge hili lilishakosa uhalali tangu awali wa kuheshimiwa na kufuatiliwa. Limekuwa kama mkutano wetu wa CCM wa NEC, Mkutano Mkuu au KK. Katika muktadha huo, ni vigumu Bunge hili kuheshimika. Katika waliojitokeza kugombea na wasiojitokeza kugombea Uspika, hakuna mtanzania hata mmoja ambaye angewezwa kuliheshimisha Bunge hili la sasa. Bunge la chama kimoja litakuwa na 'maajabu' gani? Litakuwa na mijadala gani? Litamkosoa na kumsimamia nani? Spika Tulia hatakuwa na jipya.
Amini nawaambia, Bunge hili linateswa na upatikanaji wake. Ni kama 'void ab initio'.
Wasiojulikana sasa wamejulikana?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa)
Ilikuwa wazi, kimaneno na kimatendo, kuwa Mwendazake alipania 'kuumaliza' upinzani Bungeni kwa namna yoyote ile kwenye uchaguzi wa 2020. Ndiyo maana uchaguzi ukawa uchafuzi. Alifanikiwa. Wapinzani wakasambaratishwa vya kutosha na kutisha. Baadaye, (kwakuwa ni kama nchi ilirudi kwenye mfumo wa chama kimoja kwenye macho ya kimataifa) ikaagizwa watengenezwe 'wapinzani' Bungeni. Wakapatikana akina Halima Mdee maarufu kama C...-19.
Kutokana na upatikanaji wake, Bunge hili lilishakosa uhalali tangu awali wa kuheshimiwa na kufuatiliwa. Limekuwa kama mkutano wetu wa CCM wa NEC, Mkutano Mkuu au KK. Katika muktadha huo, ni vigumu Bunge hili kuheshimika. Katika waliojitokeza kugombea na wasiojitokeza kugombea Uspika, hakuna mtanzania hata mmoja ambaye angewezwa kuliheshimisha Bunge hili la sasa. Bunge la chama kimoja litakuwa na 'maajabu' gani? Litakuwa na mijadala gani? Litamkosoa na kumsimamia nani? Spika Tulia hatakuwa na jipya.
Amini nawaambia, Bunge hili linateswa na upatikanaji wake. Ni kama 'void ab initio'.
Wasiojulikana sasa wamejulikana?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa)