Kuzidi kwa malalamiko ya kukamatwa barabarani je tatizo ni Trafiki wetu au sheria ndiyo mbovu?

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,295
21,435
Pasipo kupoteza muda!

Kumekuwepo na malalamiko mengi sana juu ya jeshi la polisi kitengo cha traffic kwamba wananyanyasa sana wenye magari barabarani!

Kuna watu wamefikia hatua hadi kuwaita Trafiki kwamba sasa NI WAKUSANYA KODI!
Mambo hayo yalinifanya nianze kuchunguza tatizo ni nini hadi tumefikia hapa! Nimejiuliza je; kama ni kweli, ina maana polisi wanapata wapi ujasiri Wa kubambikia makosa? Nikawaza tena, hao madreva wanakubali vipi kubambikiwa kosa? Je sheria zikoje? Madreva wanaouelewa Wa sheria barabarani?

Hizo leseni wanazipaje? Je madreva wanafuzu kweli mafunzo vyuoni?

Majibu ya maswali hayo ndiyo yamenifanya nijiulize sana! Niliamua kutembelea kituo kimoja cha polisi ili nipate kujua mambo haya, nikajibiwa watu hawazingatii usalama barabarani na wengi hawafahamu sheria na kuzizingatia, na bahati nzuri polisi mmoja akaniomba niambatane nae site ( tukaelekea barabarani nijionee). Ni kweli niligundua mambo mengi sana, nilijionea watu wakiendesha speed kubwa zaidi katika makazi (tochi), niligundua watu magari yao mengi ni mabovu, pia niligundua wale ambao sheria wanazijua na kuzizingatiwa walikaguliwa na kuruhusiwa waende!

Laikini kilicho nishangaza zaidi ni pale kila aliyekamatwa hakukosa sababu ya kujitetea, kuna watu walijitetea Kwa kudai wanaharaka, kuna wengine waliwapigia ndugu zao, wengine walilia machozi, wapo walikimbia n.k

Ingawa niligundua; miongoni mwa waliokamatwa wanawake ndiyo walionyesha kukubali kosa na kuandikiwa haraka kuliko wanaume;

NAOMBA TUJADILI JE; TATIZO NI TRAFIKI AU SHERIA NI MBOVU? KARIBUNI
 
Mkuu hao watu ni shida huko barabarani.
Yani kukuacha hivihivi kwao ni dhambi kubwa sana.
Kuna makosa mengine ni kumpa mtu onyo lkn wao wanataka faini.
Ma ukiongea nao sana wanataka ya kubrashi viatu.
Sasa kwa staili hiyo hatuwezi fika.
Unakuta mtu kwenye 30 umetembea 31 wao wanataka hela kweli.
Hawa jamaa hawafanyi kazi kwa weledi bali kwa manufaa yao tena binafsi maana hela hizo wanapeleka home na kidogo kwa Magufuli.
Sawa kuna watu wanavunja sana sheria za barabarani lkn wengine ni makosa madogo sana.
Lkn sawa
 
Kote kote kubovu tu..ila hasa kwa ndugu zetu maaskari.kusema ukweli hali ya uchumi wa nchi hii..kumewaongezea njaa isiyo na mfano..
 
Kuna siku nilikuwa nadrive, mtungi, triangle, bima leseni na gari lipo vizuri. Akanikagua police nikaambiwa sina first aid kit. Duh nilichoka maana ni gari private sio la abiria. Hawakosi makosa hawa jamaa!
 
Mkuu hao watu ni shida huko barabarani.
Yani kukuacha hivihivi kwao ni dhambi kubwa sana.
Kuna makosa mengine ni kumpa mtu onyo lkn wao wanataka faini.
Ma ukiongea nao sana wanataka ya kubrashi viatu.
Sasa kwa staili hiyo hatuwezi fika.
Unakuta mtu kwenye 30 umetembea 31 wao wanataka hela kweli.
Hawa jamaa hawafanyi kazi kwa weledi bali kwa manufaa yao tena binafsi maana hela hizo wanapeleka home na kidogo kwa Magufuli.
Sawa kuna watu wanavunja sana sheria za barabarani lkn wengine ni makosa madogo sana.
Lkn sawa
Mkuu kama speed limit ni 30, ww ukikutwa na 31 si ni kosa kabisa hilo au unamaanisha polisi wawe wanapuuzia kusimamia sheria?
 
Kuna siku nilikuwa nadrive, mtungi, triangle, bima leseni na gari lipo vizuri. Akanikagua police nikaambiwa sina first aid kit. Duh nilichoka maana ni gari private sio la abiria. Hawakosi makosa hawa jamaa!
Kisheria First aid kit ipo au haipo? Kama haipo kwanini ulikubali kuandikiwa?
 
Ndugu zangu tukubali speed limit nyingine ni zakukomoa na kupoteza masaa ya watu.Mi na safiri sana na gari kutoka Dar mpaka Bkb.
Kama speed limit zinawkwa sehemu ya makazi dar yote ingekuwa 50kmh.
Utakuta sehemu hakuna density inayo ridhisha wamewaka 50 kmh kilometa nzima unatembea mpaka unachoka.
Toka Tinde uende Kahama utalia Sehemu nyingine vibao hamna trafiki wapo juu ya miembe.
Tunapoteza manhour na womenhour kwa limit hizo.
iundwe kamati kuseti upya maeneo ya 50 kmh.
Viongozi na bendera zao wangekuwa wanabanwa na sheria hii wange
 
Mkuu kama speed limit ni 30, ww ukikutwa na 31 si ni kosa kabisa hilo au unamaanisha polisi wawe wanapuuzia kusimamia sheria?
Kuna kitu kinaitwa errors na calibration ,kifaa chochote kinachopima huwa kuna error allowance ya +/-5% ya kile kinachopimwa.

Maana yake ni kuwa kama spedometer ya gari ilikuwa inaonyesha au kusoma 50m/h inawezekana kabisa spidi halisi ikawa ni 55km/h au 45km/h,
The same applies kwa tochi zinazopima spidi za magari , kama askari amekupima spidi aka kukuta na tuseme 80km/h, kuna uwezekano spidi halisi ikawa ni 85 km/h au 75/h , ndo maana askari wenye shule hata akukute na spidi ya 85 km/h anaeweza asikukamate kutokana na fact kuwa either camera yake au spedometer yako haiko sahihi na kuna uwezekano kuwa spidi yako halisi ni 80km/h.
Ni vile tu mahakama zetu hazifanyi kazi kwa ufanisi lakini kesi kama hizi zingemalizwa kitaalamu matrafiki wasingekuwa wanatubambikia maana mahakama zingehusisha utaalamu kuamua hayo mambo.
 
Kuna kitu kinaitwa errors na calibration ,kifaa chochote kinachopima huwa kuna error allowance ya +/-5% ya kile kinachopimwa.

Maana yake ni kuwa kama spedometer ya gari ilikuwa inaonyesha au kusoma 50m/h inawezekana kabisa spidi halisi ikawa ni 55km/h au 45km/h,
The same applies kwa tochi zinazopima spidi za magari , kama askari amekupima spidi aka kukuta na tuseme 80km/h, kuna uwezekano spidi halisi ikawa ni 85 km/h au 75/h , ndo maana askari wenye shule hata akukute na spidi ya 85 km/h anaeweza asikukamate kutokana na fact kuwa either camera yake au spedometer yako haiko sahihi na kuna uwezekano kuwa spidi yako halisi ni 80km/h.
Ni vile tu mahakama zetu hazifanyi kazi kwa ufanisi lakini kesi kama hizi zingemalizwa kitaalamu matrafiki wasingekuwa wanatubambikia maana mahakama zingehusisha utaalamu kuamua hayo mambo.
Well said t bIj
 
Kuna kitu kinaitwa errors na calibration ,kifaa chochote kinachopima huwa kuna error allowance ya +/-5% ya kile kinachopimwa.

Maana yake ni kuwa kama spedometer ya gari ilikuwa inaonyesha au kusoma 50m/h inawezekana kabisa spidi halisi ikawa ni 55km/h au 45km/h,
The same applies kwa tochi zinazopima spidi za magari , kama askari amekupima spidi aka kukuta na tuseme 80km/h, kuna uwezekano spidi halisi ikawa ni 85 km/h au 75/h , ndo maana askari wenye shule hata akukute na spidi ya 85 km/h anaeweza asikukamate kutokana na fact kuwa either camera yake au spedometer yako haiko sahihi na kuna uwezekano kuwa spidi yako halisi ni 80km/h.
Ni vile tu mahakama zetu hazifanyi kazi kwa ufanisi lakini kesi kama hizi zingemalizwa kitaalamu matrafiki wasingekuwa wanatubambikia maana mahakama zingehusisha utaalamu kuamua hayo mambo.
Hapo kwenye error zizani kama ni kweli
 
Polisi wetu ni machinga kuna kosa la kumwelekeza mtu unakuta analazimisha fine
Kwa mfamo tail light moja haiwaki huku nyingine zinawaka badala ya kukuelekeza u fix wanalazimisha fine
 
Back
Top Bottom