Kuzama sio kwenye maji tu

Kuzama sio kwenye maji tu

ShesRise_1

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2025
Posts
17,238
Reaction score
40,772
KUZAMA SIYO KWENYE MAJI TU

Tunaposema mtu amezama, mara nyingi tunafikiria amezama kwenye mto au bahari

Lakini katika maisha, kuna kuzama kwa aina nyingi

Wengine husema, Nimezama kwenye penzi

Lakini pia kuna watu waliozama kwenye maovu na tabia ambazo zinawatesa kila siku

Kuna kuzama kwenye kamari

Kuna kuzama kwenye pombe

Kuna kuzama kwenye dawa za kulevya

Kuna kuzama kwenye rushwa

Kuna kuzama kwenye uzinzi au umalaya

Kuna kuzama kwenye marafiki wabaya

Kuna kuzama kwenye madeni, uongo, au hata tamaa ya pesa za haraka

Kinachoumiza zaidi ni kwamba wengi wanaozama huko si kwamba hawajui
Wanajitambua kabisa

Wanajua wanachokifanya si sahihi Wanajua wanapoteza muda, kipato, familia, afya na heshima
Lakini wanashindwa kujinasua

Ni kama mtu anayezama majini Anaona kila kitu, anapambana kwa nguvu zote, lakini kadiri anavyojitahidi ndivyo anavyozidi kuzama 😔

Anatamani kutoka, lakini haoni njia 😟

Ninaamini sababu mojawapo inayowafanya watu washindwe kuacha tabia mbaya ni mazingira wanayoishi

Ni vigumu kuacha pombe ukiwa kila siku upo kwenye vijiwe vya pombe

Ni vigumu kuacha kamari ukiwa umezungukwa na marafiki wanaokushawishi kucheza kila siku
(Wadau wa betting wanaelewa)

Wakati mwingine mazingira humshinda hata mtu mwenye nia ya kubadilika 💯

Lakini je, mazingira ndiyo sababu pekee?
Au kuna mambo mengine kama , kuiga, marafiki, msongo wa mawazo, au kukata tamaa, kujilinganisha , sifa na kutokukinahi?

Karibuuunii wana JF

Je, umewahi kuzama kwenye tabia fulani ukashindwa kutoka, ingawa ulitamani kuiacha?

Ni kitu gani kilikufanya ushindwe kujinasua?

Kama uliweza kuacha, ni mbinu gani ilikusaidia?

- Umewahi kumsaidia mtu kuacha tabia mbaya?

Je ukifanyaje🤔

Ukiweka comment hapa anaweza akapona mtu hata kama asiposema karibuuni guys


Chombezo : umewasha mshumaa au kibatari?

ShesRise_1🤚
 
Andika bhana viporo vya nini sasa na wewe
kuna mda watu wanazaliwa na madeni. Ukizaliwa na madeni ndio hayo yanakuumiza sana

unless your debts are paid suffering will never actually leave you. Ndio maana kuzama kunatesa sana watu
 
KUZAMA SIYO KWENYE MAJI TU

Tunaposema mtu amezama, mara nyingi tunafikiria amezama kwenye mto au bahari

Lakini katika maisha, kuna kuzama kwa aina nyingi

Wengine husema, Nimezama kwenye penzi

Lakini pia kuna watu waliozama kwenye maovu na tabia ambazo zinawatesa kila siku

Kuna kuzama kwenye kamari

Kuna kuzama kwenye pombe

Kuna kuzama kwenye dawa za kulevya

Kuna kuzama kwenye rushwa

Kuna kuzama kwenye uzinzi au umalaya

Kuna kuzama kwenye marafiki wabaya

Kuna kuzama kwenye madeni, uongo, au hata tamaa ya pesa za haraka

Kinachoumiza zaidi ni kwamba wengi wanaozama huko si kwamba hawajui
Wanajitambua kabisa

Wanajua wanachokifanya si sahihi Wanajua wanapoteza muda, kipato, familia, afya na heshima
Lakini wanashindwa kujinasua

Ni kama mtu anayezama majini Anaona kila kitu, anapambana kwa nguvu zote, lakini kadiri anavyojitahidi ndivyo anavyozidi kuzama 😔

Anatamani kutoka, lakini haoni njia 😟

Ninaamini sababu mojawapo inayowafanya watu washindwe kuacha tabia mbaya ni mazingira wanayoishi

Ni vigumu kuacha pombe ukiwa kila siku upo kwenye vijiwe vya pombe

Ni vigumu kuacha kamari ukiwa umezungukwa na marafiki wanaokushawishi kucheza kila siku
(Wadau wa betting wanaelewa)

Wakati mwingine mazingira humshinda hata mtu mwenye nia ya kubadilika 💯

Lakini je, mazingira ndiyo sababu pekee?
Au kuna mambo mengine kama , kuiga, marafiki, msongo wa mawazo, au kukata tamaa, kujilinganisha , sifa na kutokukinahi?

Karibuuunii wana JF

Je, umewahi kuzama kwenye tabia fulani ukashindwa kutoka, ingawa ulitamani kuiacha?

Ni kitu gani kilikufanya ushindwe kujinasua?

Kama uliweza kuacha, ni mbinu gani ilikusaidia?

- Umewahi kumsaidia mtu kuacha tabia mbaya?

Je ukifanyaje🤔

Ukiweka comment hapa anaweza akapona mtu hata kama asiposema karibuuni guys


Chombezo : umewasha mshumaa au kibatari?

ShesRise_1🤚
kwa mfano wewe mdau na mtoa hoja ulipozama huko ulikozamia, je, ulitokatokaje na kujinasua na mpaka leo umejikuta JF?🐒
 
Hauwezi kupona kama hauko tayari ku delay gratification yaani, kukubali kuishi na maumivu ya sasa ili upate heshima na utulivu wa kesho.
 
kuna mda watu wanazaliwa na madeni. Ukizaliwa na madeni ndio hayo yanakuumiza sana

unless your debts are paid suffering will never actually leave you. Ndio maana kuzama kunatesa sana watu
Hiii comment anyway sawa🤝
 
sijui sijaeleweka sio kwamba mtu hana utayari ila sijui ni mazingira au anakosa ujasiri lakini ni kama anashindana na yeye mwenyewe
Nimekuelewa sana, nadhani maana yako ni kwamba mtu hawezi kutarajia matokeo mapya akiwa amekaa kwenye mazingira yale yale yanayotengeneza tatizo lile lile.

Labda mfano tutolee waraibu wa matumizi ya madawa ya kulevya, au vijana walio athirika na punyeto right?
 
Back
Top Bottom