Kuwawezesha wabongo weusi! - Wazo hatari?

Wakati kumpendelea mtz mweusi kwa hila itakuwa ni jambo baya, imefika mahali sasa ili mbele ya safari tusijejiingiza kwenye migogoro, kuwe na upendeleo maalumu wa kuwasukuma watz weusi ili nao wawe players katika uchumi wetu. Mfano, kazi nyingi za ujenzi zinataka mitaji mikubwa ambayo kampuni nyingi za wazawa hazinao. Badala ya kuwapa kila kazi ya ujenzi kampuni za watz wa kiasia/kizungu kama estim, daikin,barkeley electric,caspian etc kwasababu wana mitaji, kuwe na namna ambayo kampuni nyingine ndogo zinapewa guarantee za mitaji zinapopata kazi kama hizo kutoka kwa mabank na institution nyingine za fedha. Hilo kwa sasa halipo.
Halafu hawa watz wa kiasia na kizungu faida kubwa huwa inapelekwa nje wanakokuona ni safe. Pengine wasiwasi unatokana na sababu kuwa walio wengi ambao ni weusi hawana...itakuwaje wakiwabadilikia mbele ya safari!!

Tusisahau tuliwanyang'anya hao tunaowaita wageni kila kitu tukapeana wazawa! Kuanzia mashamba ya wagiriki, mabenki, nyumba za kupanga, makampuni binafsi etc etc. Tukachukua, tukayafilisi halafu tukataka kuwarudishia wageni. Makandarasi wazawa wengi walipewa kandarasi, wakashindwa. Mahoteli vile vile tukawapa wazawa kwa bei ya kutupa, nayo wameyafilisi! Sasa tunataka tuwezeshwe vipi?

Ukweli ni kuwa hakuna njia ya mkato katika maendeleo ya dhati. Tujifunge mikanda, tusikimbie umande n.k. na siku moja tutafika.

Amandla.........
 
Tusisahau tuliwanyang'anya hao tunaowaita wageni kila kitu tukapeana wazawa! Kuanzia mashamba ya wagiriki, mabenki, nyumba za kupanga, makampuni binafsi etc etc. Tukachukua, tukayafilisi halafu tukataka kuwarudishia wageni. Makandarasi wazawa wengi walipewa kandarasi, wakashindwa. Mahoteli vile vile tukawapa wazawa kwa bei ya kutupa, nayo wameyafilisi! Sasa tunataka tuwezeshwe vipi?

Ukweli ni kuwa hakuna njia ya mkato katika maendeleo ya dhati. Tujifunge mikanda, tusikimbie umande n.k. na siku moja tutafika.

Amandla.........

Fundi Mchundo, ulichosema ni kweli. Lakini wakati hayo yote yakifanyika, tulikuwa hatuko tayari kujitegemea na hasa hatukuwa na ujuzi wa kusimamia rasilimali tulizokuwa nazo. Wasomi wakati ule walikuwa wachache, na serikali iliamua kusimamia vitega uchumi vyote. Kama unavyojua, serikali ilikuwa ikiteua wasimamizi wa mashirika yaliyotaifishwa kwa kujuana na bila kuzingatia vigezo muhimu vya ujuzi wa usimamizi wa biashara zilizokuwa zikifanywa na makampuni hayo. Vile vile, serikali ilikuwa ikichukua kila pato la makampuni hayo, na kuyagawia ruzuku ambazo mara nyingi zilikuwa finyu kulingana na gharama za uendeshaji wa makampuni hayo.

Kwa sasa, tuna watu wengi zaidi wenye elimu nzuri zaidi. Vile vile, serikali iliamua kubinafsisha makampuni karibu yote iliyoyataifisha. Uzuri na ubaya wa hatua hizo unaweza kuzungumziwa. Ila jambo kubwa na ambalo nadhani inabidi kulifanya bila kusita, ni kuhakikisha kuwa waTanzania (bila kujali matabaka yao) wanakuwa na uwezo wa kufanya shughuli zao kwa tija na kunufaika na jitihada zao. Ilivyo sasa, watu wengi wenye asili ya nchi hii huonekana wasio na ujuzi, wasio na uwezo na hata wasio na thamani ya kutosha kusimamia jitihada zozoe za maendeleo ya nchi yao. Hii inathibitika katika mipango karibu yote ya maendeleo kupewa makampuni ya nje, uhamasishaji wa uwekezaji kupewa kipaumbele kwa watu wa nje n.k.

Kampuni ya mTanzania kudumu katika mazingira ya kibiashara ya nchi hii ni ngumu sana. Hakuna jitihada za maana za kuhakikisha mfanyabiashara huyo anapata mikopo anayotaka kwa wakati kama ilivyo kwa wengine (huu ni ukweli unaojaribu kupingwa na wengi), mazingira ya kibiashara kwa mTanzania wa kawaida ni ya kimtego-mtego. Ndio maana utakuwa umesikia Mawaziri wakitishia wachimba madini (mfano: Busanda) kutopewa leseni kama hawatafanya uchaguzi wanaoutaka. Mambo ni mengi ya kukwamisha jitihada za hao tunaowaita wazawa.
 
Nikiwa kama Conservative, naamini kabisa kuwatajirisha wazawa kulingana na vipaji - elimu zao ktk mazingira yetu ndio njia pekee ya kuanza mabadiliko ya kiuchumi yenye sura halisi ya - nini maendeleo..
__________________
kwa hiloo natumai huenda tukasogeaa kwani ndo silaha muhimu ya mtu maskiniii...
jamani lini tutahamsika kuondokana na ulalamishi na kuhamasika kuleta suluhuu ya maendeleooo...
 
Tusisahau tuliwanyang'anya hao tunaowaita wageni kila kitu tukapeana wazawa! Kuanzia mashamba ya wagiriki, mabenki, nyumba za kupanga, makampuni binafsi etc etc. Tukachukua, tukayafilisi halafu tukataka kuwarudishia wageni. Makandarasi wazawa wengi walipewa kandarasi, wakashindwa. Mahoteli vile vile tukawapa wazawa kwa bei ya kutupa, nayo wameyafilisi! Sasa tunataka tuwezeshwe vipi?

Ukweli ni kuwa hakuna njia ya mkato katika maendeleo ya dhati. Tujifunge mikanda, tusikimbie umande n.k. na siku moja tutafika.

Amandla.........

FM:

Kizazi kilicholelewa kuamini kuwa kufanya biashara ni unyonyaji kwanini kiwe na mafanikio kwenye biashara?
 
Lusekelo kachanganyikiwa.......hivi anataka watu weusi wawezeshwe vipi? si tulitaifisha mali zote za wageni tukagawana leo mbona bado tunalia mtu mweusi masikini?
kuna mtu amesema enzi zile tulikuwa hatuko tayari kujitegemea, jee unamaanisha sasa tupo tayari kwa kipimo gani?
 
Nachelea kuitwa mbaguzi
Ila nadhani kama kutakuwa na fairness ktk opportunities suala kuwaendeleza black itakuwa tunapiga hatua mbele ya ubaguzi.

Ila wanaowauza weusi kwa weupe ni viongozi wetu ambao ni weusi kwa asili.
 
..tuna safari ndefu sana ktk suala hili kutokana na sababu za kihistoria.

..wakati wa mkoloni kulikuwa na sheria inayokwaza wazawa/native/weusi kupewa mikopo. sheria hiyo ilikuwa inawatambulisha wazawa kama watu wasioaminika.

..sheria iliekeza kwamba chombo chochote cha fedha kitakachotoa mkopo hakitakuwa na nguvu yoyote ya kisheria ikiwa mzawa aliyekopeshwa atashindwa kulipa deni.

..miaka 6 baada ya kupata uhuru tukaja na siasa ya Ujamaa na Azimio la Arusha. kipindi hicho mfanyabiashara yeyote yule alionekana MNYONYAJI.

..Azimio la Arusha halikupokonya mali/biashara za wawekezaji wageni na kuwapa wazawa. kilichotokea ni mali za wawekezaji wageni kupewa SERIKALI kuziendesha.

..wazawa wana safari ndefu ya kujifunza. zaidi wanahitaji kuwezeshwa.
 
Jana kwenye TV walionyesha something to do with EPZ na kwamba wameshaanza kuwapa wafanyabiashara maeneo/leseni za kuwekeza...........angeona Lusekelo sijui angesemaje - wote walikuwa wahindi na waarabu, hakuna hata mzawa mmoja!!

On another note: baada ya kutaifisha vyanzo vya ubepari Tanzania, wazawa wengi got caught up in the utopian politics of those times, tukajiingiza kwenye ujamaa na kujitegemea, rudini vijijini, vijiji vya ujamaa, unyonyaji ni unyama (hata mirija ya kunywea soda ilipigwa marufuku!) and all the good stuff those times, etc lakini wale walionyang'anywa mali zao, hususan wahindi, waliendelea na biashara/commerce chinichini.

Loh and behold, when siasa za Rukhsa! came along, who was standing up straight in business? Wadosi! Who was able to make things happen for them and facilitate majambo mengimengi? Viongozi wazawa wale wenye vyeo vya juu kama mawaziri, wakuu wa mikoa etc! Hivi isn't it obvious that these two groups suddenly became rich beyond compare?

Swali lingine linakuja: Nini kifanyike? Solutions mbili zimeonyesha kufanikiwa kiasi depending on who you speek with. Moja ni ile ya Sauzi ya BEE, na nyingine ni ile ya Small Business Association (SBA) ya USA. Kama alivyosema Recta hapo juu kuwa makampuni mengi ya wazawa hayawezi compete na makampuni ya wadosi au wazungu - kubid kutengeneza an accounting system ya Tz Ports Authority, for example, a bidding company will need to put an untouchable bid security of $82,000! Makampuni yetu mangapi yataweza hii? But if there is a BEE or an SBA of some kind then banks could chip in if I, a mzawa, come to them with a guaranteed bid that I won but don't have the funds to go ahead with a project. The SBA in the USA guarantees that some contracts are to go solely to minority owned firms (even though sometimes white women get them simply because women are in the minority of businesses in the USA) Mfano hapa kwetu, kama Estim atajenga ghorofa basi atakayefanya wiring awe ni mnyalukolo mmoja mwenye kampuni yake iliyosajiliwa kihalali; kampuni ya usafi iwe ya halali ya yule mzawa mwenye kampuni inayofanya kazi hiyo; etc etc.

Sasa itakuwa vipi kama "mzawa" ni mzaliwa wa Tanzania lakini ni mdosi au mgiriki? Yeye ni mzawa kweli au udosi/ugiriki wake unamtoa kwenye uzawa? Maswala kama haya ndio yanayoweza kuonyesha mgawanyo wa matabaka ya rangi - bado ni ubaguzi ambalo lipo on a thin line love and hate.

My two cents......
 
Gelange Vidunda said:
Swali lingine linakuja: Nini kifanyike? Solutions mbili zimeonyesha kufanikiwa kiasi depending on who you speek with. Moja ni ile ya Sauzi ya BEE, na nyingine ni ile ya Small Business Association (SBA) ya USA. Kama alivyosema Recta hapo juu kuwa makampuni mengi ya wazawa hayawezi compete na makampuni ya wadosi au wazungu - kubid kutengeneza an accounting system ya Tz Ports Authority, for example, a bidding company will need to put an untouchable bid security of $82,000! Makampuni yetu mangapi yataweza hii? But if there is a BEE or an SBA of some kind then banks could chip in if I, a mzawa, come to them with a guaranteed bid that I won but don't have the funds to go ahead with a project. The SBA in the USA guarantees that some contracts are to go solely to minority owned firms (even though sometimes white women get them simply because women are in the minority of businesses in the USA) Mfano hapa kwetu, kama Estim atajenga ghorofa basi atakayefanya wiring awe ni mnyalukolo mmoja mwenye kampuni yake iliyosajiliwa kihalali; kampuni ya usafi iwe ya halali ya yule mzawa mwenye kampuni inayofanya kazi hiyo; etc etc.

Sasa itakuwa vipi kama "mzawa" ni mzaliwa wa Tanzania lakini ni mdosi au mgiriki? Yeye ni mzawa kweli au udosi/ugiriki wake unamtoa kwenye uzawa? Maswala kama haya ndio yanayoweza kuonyesha mgawanyo wa matabaka ya rangi - bado ni ubaguzi ambalo lipo on a thin line love and hate.

Gelange,

..i am with you 100%.

..sasa viongozi wetu hawaishi kwenda SA na USA lakini hawana habari na hayo uliyoandika.
 
Tunajua kwamba huwezi kunyea kambi hivi hivi tu. Waweza jua unalotenda sio sahihi ukiwa kambini ila ukitoka au kutolewa ndio unaona umuhimu wa ukweli. Sera ya uzawa ni sawa tu. Ndio maana nchi imeparaganyika kiasi hiki. Hao mafisadi papa hata ukiwaambia kuhusu uzalendo watakuelewa? Nashangaa mko nje lakini hamjui mifumo ya nchi mlizomo. Kuna sera zisizoonekana huko na zinafanya kazi na wazawa wa huko wanajua! Ndio maana tunakashifiwa na wageni kila leo. Utawezaje kumkirimu mgeni kulilo mwanao? Ndio wale ambao mgeni akija mtoto analala chini. Atakuchukia tu! Naweni nyuso!
 
Si makampuni yote yaliyo binafsishwa walipewa wageni. Hao mnaowaita wazawa walipewa mengine. Hoteli za kifahari kama Mikumi, Savoy ya Morogogoro, Hoteli za Shirika la Reli n.k. walipewa wazawa. Viwanda vya ngozi, viatu, nguo n.k. navyo walipewa raia. Vingine katika kutafuta wazawa vikaachiwa hadi mabati yakaezuliwa. Makandarasi wengi tu wazawa walipewa kazi, zikawashinda. Benki kama THB ilifilisika kwa kujaribu kuwawezesha wazawa. CRDB nayo almanusura iende huko huko kama si wadenish! Elimu bila uzoefu haina maana. Sisi tunadhani kwa sababu sasa tuna vijikaratasi vinavyosema kuwa tumeelimika basi kila kitu tunaweza. Sambamba na kuwawezesha raia wote wa Tanzania inabidi tuweke mkazo katika regulatory bodies kuhakikisha kuwa hakuna viujanja ujanja. Inabidi tuelimike kiasi cha kujua pale tusipo na uwezo napo. Tunapoona hilo tusisite kumkaribisha mwenye uwezo zaidi yetu lakini elimu yetu itusaidie kuhakikisha kuwa haki inatendeka, kwake na kwetu.

Tusitake ufahari wa haraka haraka. Hatutafika huko. Hata wakina Steve Jobs walianzisha kampuni zao gereji na hawakusita kukaribisha wenye uwezo zaidi kuwasaidia!

Amandla..........
 
Tunaposema "raia" tuna maana ya "wazawa".. na tunaposema "wazwa" tuna maana ya "watu weusi" au tunaposema "wazawa" tunamaanisha Mtanzania yeyote bila kuangalia rangi yake au nasaba yake?

Je unaweza kuliwezesha kundi moja la watu kwa minajili ya rangi zao bila ya kujikuta unavunja katiba?
 
Tunaposema wazawa tunamaanisha watanzania weusi. Ninaposema raia nina maanisha wale wote wenye sifa ya uraia bila kujali wameupataje, rangi yao, dini yao au jinsia yao.

Hilo la katiba silijui lakini ninavyofahamu neno uzawa linatofautisha watu kwa minajili ya rangi zao.

Amandla.......
 
Tunaposema "raia" tuna maana ya "wazawa".. na tunaposema "wazwa" tuna maana ya "watu weusi" au tunaposema "wazawa" tunamaanisha Mtanzania yeyote bila kuangalia rangi yake au nasaba yake?

Je unaweza kuliwezesha kundi moja la watu kwa minajili ya rangi zao bila ya kujikuta unavunja katiba?

Kwani "Kuwezeshwa" ni sawa na kupendelewa?
Nadhani la muhimu ni kuwawezesha ili finally waweze kuwa na "The piece of a pie" kwenye economic and social well being zao.
Unless kuna something i miss.
 
Tunaposema wazawa tunamaanisha watanzania weusi. Ninaposema raia nina maanisha wale wote wenye sifa ya uraia bila kujali wameupataje, rangi yao, dini yao au jinsia yao.

Hilo la katiba silijui lakini ninavyofahamu neno uzawa linatofautisha watu kwa minajili ya rangi zao.

Amandla.......

neno "wazawa" linatokana na neno zaa, na ni mojawapo ya unyambulisho wa neno hilo. Ni kutoka hapo tunapata zaliwa, zaana, zaliana, n.k Mara nyingi wanaposema "wazawa" wanamaana ya "wazaliwa" na katika kisiasa linataka kumaanisha "wazaliwa wa asili" wa mahali fulani. Mara zote halihusiani na rangi. Linahusiana na watu wa asili wa mahali fulani.

Kwa lugha ya wenzetu, ni sawa na "indigineous". Bahati mbaya sana kwa Tanzania huwezi kusema watu asili wa Tanzania ukamaanisha wote ni weusi kwani kuna watu wengine ambao ni waasili lakini siyo weusi (wabantu)(Wairaq, Wambugu).

Lakini zaidi pia ni kuwa "raia" (citizen) si lazima awe mzawa lakini mzawa si lazima awe raia vile vile. Mtu anaweza akawa mzawa wa Tanzania lakini si raia wa Tanzania (kahamia kwingine kwa mfano). Vile vile mtu ambaye ana rangi fulani si lazima awe raia wa mahali fulani, hivyo mtu mweusi wa Kenya akija Tanzania haina maana ana haki za raia wa Tanzania au awezeshwe kwa sababu ni "mweusi".

Hivyo, basi utaona kuwezesha kwa misingi ya uzawa au rangi ni makosa. Msingi pekee na bora zaidi ni ule wa uraia.

Baada ya kusema hivyo, kuna wakati ambapo jamii inalazimika kusahihisha makosa ya kihistoria (correcting historical wrongs) au makosa ambayo wahusika hawakuwa na nguvu juu yake. Katika kufanya hivyo, jamii inatakiwa kutunga sera ambazo zitasahihisha makosa hayo.

Masahihisho hayo ya kihistoria hayawezi kuwa ya kudumu na yasiyo na mipaka.
 
Makampuni yaliyo binafsishwa, yalibinafsishwa kwa makosa mbalimbali. Ubinafsishaji ule haukuwa wa wazi sana na vile vile haukuwa wa haki inavyotakiwa. Pia hakukuwa na masharti ya kutosha ya uendelezaji wa viwanda na makampuni hayo. Na kwa sababu hizo mengi hayakuendelezwa na hivyo matumizi yake yalibadilishwa na walioyanunua. Ukiachia mbali kuwa mengi ya makampuni yaliyobinafsishwa yalikuwa yameshakufa tayari. Ila sidhani kama mada hii inaruhusu kuzamia sana huko.

Kinachotakiwa ni kuweka usawa katika kuwezesha waTanzania wote katika kujiletea maendeleo yao. Siamini kuwa atakuja mtu kutoka nje ili kutusaidia kupata maendeleo ya nchi hii. Mifano ni mingi ya wale waliojidai kuja kutusaidia na wakaishia kutumaliza. Makampuni ya nje yote yanakuja na yatakuja nchini ili kuvuna zaidi ya wanachoweza kuvuna wakiwa kwao (pamoja na umasikini wetu). Hiyo ndio nia yao (hata kama haitatimia kwa kiwango hicho). Wakimaliza kuvuna, wataondoka na kutuachia magofu tujue tutakachofanya nayo. Hili litakuja kuonekana tu, muda si mrefu kama bado halijaanza kuonekana.

Taasisi zote za fedha zimeshikwa na watu wa nje au wenye asili ya nje ya nchi yetu. Hivyo si rahisi sana kwa "mzawa" kufaidika nazo.

Ndiyo, Elimu ni muhimu sana katika kufanikisha malengo yoyote tunayojiwekea. Ila elimu peke yake haitoshi kufanikisha malengo hayo. Lazima kuwe na conducive environment itakayosaidia kufanikisha kwa ufanisi unaohitajika malengo yote. Si muda mrefu tutaanza kuwa watumwa kwenye nchi yetu (kama bado hatujaanza kuhisi utumwa huo). Sasa tumeanza kuona wachina, wahindi, waAfrika Kusini waKenya na kadhalika wakija kufanya kazi ambazo hata sisi wenyewe tunaweza kuzifanya kwa ufanisi. Mifano iko mingi vile vile.

Serikali inalo jukumu la kuweka sawa hali ya uchumi. Uchumi wa nchi usipokuwa kwenye mikono ya waTanzania (bila kujali rangi zao) hakuna tija ya kudumu itakayopatikana. Watatuacha tukiwa fukara kwa kutuachia 3% (loyalty fee) tunayoitamani sana, siku watakapoona inafaa kwao kuondoka.

Hivi kweli tunaamini kwa elimu zote zinazopatikana duniani bado hatuwezi kujiendesha wenyewe? Mimi hilo siliamini hata kidogo. WaTanzania wengi wana elimu nzuri ila wanaona ni heri kutumika nchi nyingine (hasa za ulaya na Marekani) ambapo watalipwa vizuri zaidi, kuliko kutumikia wale wale wakiwa ndani ya nchi yao (Tanzania) kwa ujira mdogo.Tatizo hilo ni sugu na lazima litafutiwe dawa, kama kweli tunataka tuendelee.
 
Wale wanaopingana na makala hiyo ya Lusekelo wasome kuhusu Patriotic acts za wamarekani,acts ambazo zilikuwepo loongtime ago lakini haina maana kuwa hakukuwa na ubaguzi,sheria za kibaguzi zimeondolewa majuzi tu,tusijilazimishe kuwa watumwa ndani ya nchi yetu wenyewe kwa kujidai kuwapa kipaumbele wageni kwanza,acheni blah blah....Wazawa NI LAZIMA wapewe kipaumbele halafu kama kuna matatizo yatakayojitokeza basi yataundiwa sheria pia ili kufanya mabadiliko ili kuweza kurekebisha lolote litakalo jitokeza,nashangaa kwanini hakuna wanaodai kwanini majority wateseke ndani ya nchi yao,na hivyo la msingi ni mzawa kwanza,we tafsiri unavyotaka.
 
Wakati fulani nilikuwa nikitafakari jinsi ya kuinua standard of living of people in Tz nikajisomea development approaches mbali mbali kukawa na sehem moja ambapo wakazi group into three.

1. Two sector enrichment yaani unaendeleza kote rural (old) and mjini (modern) sector, wakatoa mfano wa Europe ndo wanatumia hii approach

2. Rural sector enrichment while maintaining the modern-hii unaamua kuendeleza watu wa vijijini kwa kuongeza kipato chao gradualy na kumaintain income ya modern sector- hii waliitumia Sri-lanka na imeleta mafanikio makubwa kuziba gap between rich and poor

3. Modern sector enrichment sasa hapo nchi nyingi za Africa ndo zinvyofanya na hali tunaishuhudia wenyewe ilivyo mfano Dar congestion na mauza uza kibao na pia nguvu nyingi ya serikali inabidi itumiwe hapo ili kuondoa uwezekano wa maafa kutokea; think of kipindu pindu cha mara kwa mara.

Sasa nikawa na waza sasa baada ya kusoma hii link je tatizo ni uzawa na rangi au tatizo ni approach tuliamua kuitumia ku kuza uchumi wetu? And according to that analysis conclusion ni kuwa income gap is not a problem of the stage of economic growth but more of the approach used.

kuna wakati nilisafiri kwenda Lushoto nikaona nyumba mbili nzuri sana zenye mandhari ya kupendeza nikazifurahia sana lafu sasa najiuliza hivi kubadili sura za rural landscape zetu zikafanana na zile tuna hitaji investors?

Kwa haraka haraka ni materials gani zilizotumika pale ambazo haziko locally produced? Ndipo nikaja na wazo mfano tukawa na sera ya rural development then tukawapa fursa vijana wa ardhi pale waje na bussines plan zao, engineers UDSm na hortculture SUA vile vile then then wangepewa hizo billion za JK tukaweka policy ambayo itawa spread in various places kulinda soko na kuwaamuru kutumia vijana wa VETA na locally produced materials hivi kweli kama watawajengea watu huko vijijini nyumba kwa mikopo ya muda mrefu say 15 years na riba nafuu watanzania watashindwa kulipia hizo nyumba? na je hapo watu wa modeling ebu fikiria hizi projects na hizo developed companys zita leta effect ipi kwenye rural income?

Then tuje kwenye kilimo na kufanya hivyo hivyo hivi wangapi watapenda kuendelea kukaa Dar kwenye usumbufu wa mpaka watu wengine wanugua presure kwasababu ya kukaa mno barabarani kwenye foleni? Tena ukasaidia serikali ikahamia Dodoma na ukapunguza wizara za serikali na kufuta paralel structure kibao zinazo dublicate mambo hapo jamani tutaongelea uzawa tena? La hasha lugha itakuwa kupeleka watoto shule maana ume add value kwenye elimu na kufanya kazi kwa bidii maana wavivu ndo watakua minority.

So the big problem there is not uzawa and uzaliwa but the issue is planning and approach used in bringing development. Tunatumia nguvu kuwaondoa machinga kariakoo wakati hawakuletwa kwa nguvu walivutwa na maisha mazuri Dar so the same kamba iliyowavuta ndo iwarudishe. I think we have big problem in planning our development na hizo MKUKUTA and other names zina amplify problems tu maana zinavuta watu kwenye center ya MKUKUTA ambayo ni DAR na huwezi ondoa umaskini wa Tanzania kwakuangalia DAR thats like reducing our country into a size of DAR.

Peleka projects rural kwakutumia realistic policies zinazo zingatia particularities za watu wako I mean available technology and resources and let them advance from there na usilazimishe wafanane na Europe ambapo hakuna hata udongo wakutosha na mawe na changarawe then una inflate bei za ujenzi as if hizo material na labour ni expensive kama Europe. Let us be ourselves hata nyumba za majani zikijengwa vizuri na kuwa kama za hoteli kubwakubwa si poa tu tena tutakuwa unique ila tu zimamoto ziwe karibu au tu advance tembe ya wagogo kwa kutumia architect wetu na engineers wetu then uone structures zitakazotokea hapo. Watanzania wote walio Ulaya watarudi wenyewe nyumbani bila kuombwa..

Hebu tujiamini what we have is Gold even if our eyes see udongo ila tu attitude na poverty is more of an attitude than anything.
 
Last edited:
Tatizo siyo kutoa dukuduku la kuneemesha watu weusi, tatizo ni namna unavyolitumia neno hilo katika kuleta hoja yako.

Hoja ya kuinua watu weusi kiuchumi Tanzania ni hoja ilengayo kuwajaza Mapesa watu wachache walioko madarakani.

Tunatakiwa kukaa chini na kushughulikia matatizo ya msingi Tanzania yanayo lenga katika kuimarisha miundo mbinu.
Leo hii hapa JF watu bado wanatetea kilimo cha jembe la mkono kwa nguvu zao zote, sijui wanafanya hivyo kwa uzoefu au kwa vile wao hawalimi?
Imarisha Kilimo.
Imarisha barabara.
Rekebisha sheria za uwekezaji.
Imarisha elimu, siyo ubabaishaji uliopo sasa hivi.

Hakuna haja ya kulenga kundi moja la watu kuna haja kulenga pale matatizo makubwa ya miundo mbinu yalipo.

Tunachimba Gesi lakini badoi tunapikia mkaa na kuharibu ardhi yetu.

Tumechina.
 
Madela wa Madilu,.
Leo hii haa JF watu bado wanatetea kilimo cha jembe la mkono kwa nguvu zao zote, sijui wanafanya hivyo kwa uzoefu au kwa vile wao hawalimi?
Mkuu akina nani hao wanaotetea kilimo cha jembe la mkono?..
Mii nadhani wewe ndio hukuwaelewa.. Ukulima unategemea na mazingira yako. Ardhi kubwa ya kilimo inayokaliwa na watu wengi (Wakulima) ni tofauti na ardhi kubwa ambayo haina watu wengi wakulima..
Wanachosema wengi ni kuwa na Ukulima wa kisasa lakini ktk mazingira yanayowapa watu wengi miliki ya uzalishaji huo tofauti na kusema au kutetea kuwa watu walime kwa jembe la Mkono.
Kwa hiyo unaposikia wakulima wadogo wadogo haina maana ni matumizi ya jembe la mkono ila ni ardhi kubwa iliyokaliwa na wakulima wengi hivvo mgawanyika wa ardhi unakuwa mdogo..lakini ukubwa wa shamba bado ni ule ule na unahitaji mtaji, vifaa na pembejeo sawa na zile zitazotumika ikiwa wakulima ni wachache ktk ardhi kubwa!
 
Back
Top Bottom