<br />Pole sana mkuu, ila ninachoshukuru ile situation ilinifundisha kujitegemea.
<br />halafu hv ni kwanini wanawake ndo huwa na roho mbaya sana kwenye hz ishu?<br />
Kwa maisha niliyoishi drs la 5 hadi 7 mungu ndo anajua.<br />
Leo hii mama yule akiniangalia usoni anainamisha kichwa,haamini kama ndo namalizia malizia university.<br />
Nakumbuka mama mzazi alinishauri enzi zile alipopewa ful stor na majiran kwa vile me nilikuwa sio muongeaji,"mwanangu wala usimchukie,soma hvyo hivyo tu,siku ukipata kazi mnunulie zawadi nzuri sana umpelekee"<br />
na nitalitimiza hilo!<br />
Khaaah! Hii thread imenikumbusha mbali sana,eeh mungu msamehe mama yule!
<br /><br /><br />
<br />
SIYO WANAWAKE TU HATA WANAUME WANA ROHO MBAYA. Nimekaa familia 3 tofauti. Ya 1 ilikuwa kwa uncle wangu, ancle alikuwa katili,mkali sana, lakin mkewe (aunt) yetu alikuwa mpole sana, hakutukatisha tamaa juu ya ukali wa ndugu yetu na yeye ndiye alisababisha hata ndugu wa mume wake tuweze kuishi pale au kuwatembelea. Ya 2 kwa uncle mwingine, uncle alikuwa mpole,mwenye upendo sana lakin mkewe mmh! Balaa mchoyo,mkali,mwongo na tabia zote mbaya unazozijua tulikaa kijeshijeshi,ki kimbizikimbizi. Ya tatu kwa kaka yangu, kaka yangu mkali,katili hana upendo hata kidogo lakin mkewe (wifi) yetu ni mpole,utu,mkarimu anatabia nzuri sana smtms nahisi kama siyo binadamu ni malaika ksb anatabia njema kupita kiasi, simchukulii kama ni wifi yangu bali ni dada yangu, tunakuwa karibu na familia yao ksb ya wifi na utu wa watoto wao tu lakin huyo kaka yetu ni balaa kwa roho mbaya, ila tunamshukuru mungu kwa kumpa mke mwema asiye na ubaguzi kwetu, tunampenda,tunamheshimu na tunamwombea uhai na afya njema zaid. Pamoja na kasoro zao hao wote bado nawapenda ksb kupitia hizo tabia zao nimejifunza mengi sana na zaidi ya yote ni UVUMILIVU NA KUJITEGEMEA PASIPOKUWA NA MAWAZO YA KUJIDEKEZA,MAZINGIRA YOYOTE NAWEZA KUISHI TENA KWA FURAHA NA AMANI MOYONI MWANGU.<br />
<br />
Kwahiyo mi naamini ubaya hauna jinsia ni TABIA INAYOWEZA KUTOKEA KWA JINSIA YOYOTE ILE. Tunachotakiwa kufanya ni kuvumiliana na kupendana tu pamoja na hizo kasoro zetu.
<br /><br /><br />
<br /><br />
kwa mtazamo wako,afadhali nani awe mkali kati ya mwanamke na mwanaume kwenye familia
Hakuna wa Ughaibuni humu watupe nao experience zao, hasa wale ambao karatasi zinawasumbua..
kuishi kwa watu lazima ubadilike
usiishi kama uko kwenu
hicho ndicho kilichonifanya nisiende kukaa kwa watu maishani mwangu. Naelewa kuwa kuna wengi situation zinawalazimu kufanya hivyo. Ila kama ni kuchagua kwa kweli kukaa kwa watu tabu. Nakumbuka nilienda kumtembelea ndugu yangu arusha, yani i had to pretend being a good girl. Kuamka saa kumi na mbili, wakati home kama siendi school nalala nitakavyo.
Kwa watu napiga kazi kweli kweli. Yani mpaka mtu unaaga wanakwambia njoo tena next holiday. Maana wanaona wamepata housegirl wa bure. Wengi hawalijuhi hilo kuwa huwezi kuishi maisha kama ya nyumbani kwenu ukiwa ugenini.
kwa watu nakumbuka nilienda kwa ba mdogo likizo
wakati wa kulala watoto wote wamewekewa net ya mbu
mie hakuna, eti watoto wanalala saa mbili mie nakosha vyombo
wakati mmoja ni mkubwa kuliko mie,kuanzia hapo sikupenda tena
kwenda kusalimia