Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,604
- 1,704
Kijani rijali ukishavuka umri wa miongo mitatu bila kuoa au kuwa na mtoto unasakamwa huko na kule. 'Hivi mwanetu utaoa lini?', utaulizwa na wajomba na shangazi zako. 'Yaani unataka tufe kabla ya kuona wajukuu?', utahojiwa na mabibi na mababu zako. 'Eti Kaka huna hata mtoto wa kusingiziwa', utasailiwa na dada na kaka zako. Jamani hivi kuoa na kuzaa ni wajibu? Si watu wameshaongezeka na kuijaza nchi? Ni dhambi na laana kutooa na kutozaa kama si mseja?