Kuwa makini sana unapomshauri mtu mambo ya mapenzi

Tuko

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
11,178
7,320
Ni rahisi sana kushauri hapa jukwaani.
Hata hivyo ni very tricky kushauri live hasa kwa rafiki yako. Ukweli ni kwamba mara nyingi rafiki yako anapokuhadisia juu ya mapungufu ya mpenzi wake, unaweza kupima na kuona kuwa ushauri sahihi ni kumwambia waachane. Ukimwambia hivyo atakukubalia, na kukushukuru, na kuendelea kumwaga ubaya juu ya huyo mpenzi wake kwako. Hata hivyo, wengi wa wanaopokea ushauri huwa hawaendi kuachana, na siku kadhaa baadaye utawakuta wanapendana sana na uwezekano ni mkubwa kuwa huyo rafiki yako alienda kumhadisia mpenzi wake jinsi alivyokuwa unamnanga na kumtaka waachane.
Yameshanikumba, na sasa niko makini sana kabla sijamwambia mtu, 'achana nae, hakufai'
naamini wanajamvi pia mpo ambao mmeshashuhudia hayo..
 
Hiyo ni kweli umeongea lakini mie sidhani ushauri unaopewa unaubeba kama ulivyo lazima uchuje au kwa lugha nyepesi husema "Ukipewa ushauri changanya na wako"
 
kama ni rafiki yako wa dhati kwa maana ile ya dhati hasa nibora umpe ukweli kuwa amwage anayemkondesha.

Hamna maana ya urafiki kama hutampa ukweli ikizingatia unaongea kwa goodwill.Think of unajua jamaa ni mume wa mtu na anamchukua rafiki yako why dont u expose kwake ili asijiaribieeeeeeeeeeeeeeeee?
 
Yap
Kama Dena
Alivyosema si
Kila unachopata hapa
ni ukweli unatakiwa uchambue
kidogo maana kumbuka kuna wengine
Ndo wako 18halafu wanakushauri uachane na
mtu uliye oana naye miaka 20 khaaaa inakubalika kweli?
 
vipi mdada akikwambia gf anatembea na mtu flani,how will dis sound?
I guess you don't have to jump into conclusion na wewe ukakubali moja kwa moja take your time na wewe kufanya uchunguzi wako kama kweli au lah!! Nafikiri hapo utakuwa umefanya jambo la busara
 
I guess you don't have to jump into conclusion na wewe ukakubali moja kwa moja take your time na wewe kufanya uchunguzi wako kama kweli au lah!! Nafikiri hapo utakuwa umefanya jambo la busara
if this is the case mbona wakaka mara nyingi tunapowaambia huyo dada flani hafai hamtusikii?au ni mambo ya kubuy buy time muda uogee?
 
Kama kweli wewe ni rafiki yao, wakigombana wakuatanishe uongea nao kwa pamoja kuliko kusikiliza upande mmoja na kutoa ushauri, maana kuna uwezekano ataenda kuhadhia mwenzake nawe utaumbuka na kuchukiwa na mmoja wao.
 
if this is the case mbona wakaka mara nyingi tunapowaambia huyo dada flani hafai hamtusikii?au ni mambo ya kubuy buy time muda uogee?
Unajua Mary kuna wengine wakiishasikia hivyo wanaanza kuhisi labda wewe haupendi mahusiano waliyonayo lakini si kweli inawezekana unasema kwa uzuri tu ila cha msingi ni kwa muhusika kuchukua jukumu la kufanyia kazi kile alichoambiwa na sio kuanza kumu-accuse mtu kuwa anawaonea wivu.
 
Kama kweli wewe ni rafiki yao, wakigombana wakuatanishe uongea nao kwa pamoja kuliko kusikiliza upande mmoja na kutoa ushauri, maana kuna uwezekano ataenda kuhadhia mwenzake nawe utaumbuka na kuchukiwa na mmoja wao.
Wakigombana halafu ukiamua uwakutanishe uongee nao mara nyingi mwenye makosa huwa hakubali kukutana na mwenzake ili kupata suluhisho.
 
Kuweni kama mbayuwayu ndugu zangu ushauri toka kwa mwenzio changanya na akili zako ndipo ufanye maamuzi. La sivyo itakula kwenu!! Wiseman say ''those who tell you about others, tell others about you'' Anania Komba (1999)
 
Unajua ishu hapa ni kuwa marafiki wanapenda sana kushea stori juu ya wapenzi wao. Then unakuta wakati saga linaanza, say infidelity au vurugu au chochote, rafiki anakuwa anafeel anavyotendewa rafiki yake. Pole sana, Mvumilie, jamani kwa nini anakuwa hivi n.k ni maneno ya faraja yanayotoka kwa rafiki kwenda kwa mtendewa. Along the process, mtu anaamua liwalo na liwe anaachana na mpenzi. Atamuhadithia rafiki yake wazo lake hilo. Utakuta kuwa yule rafiki alikuwa anaona saga zima hivyo naye anaamini kuanchana ndiyo njia sahihi, so anamwambia rafiki yake go on, piga chini.
Mapenzi ni mapenzi tu, wiki moja, mbili, wao kwa wao wapenzi wanawasiliana wanaelewana wanarudiana. Wewe rafiki bila kujua hili wala lile unakuja kuta rafiki yako yuko na wazamani aliyekuwa anamponda vibay, nawe ulishiriki kumshauri aachane naye. Na keshamuambia 'unajua hny, hata rafiki yangu fulani alinisahuri eti nikupige chini kipindi kile'...
 
Chukua ushauri chambua, pembua, changanya na zako.
 
Unajua ishu hapa ni kuwa marafiki wanapenda sana kushea stori juu ya wapenzi wao. Then unakuta wakati saga linaanza, say infidelity au vurugu au chochote, rafiki anakuwa anafeel anavyotendewa rafiki yake. Pole sana, Mvumilie, jamani kwa nini anakuwa hivi n.k ni maneno ya faraja yanayotoka kwa rafiki kwenda kwa mtendewa. Along the process, mtu anaamua liwalo na liwe anaachana na mpenzi. Atamuhadithia rafiki yake wazo lake hilo. Utakuta kuwa yule rafiki alikuwa anaona saga zima hivyo naye anaamini kuanchana ndiyo njia sahihi, so anamwambia rafiki yake go on, piga chini.
Mapenzi ni mapenzi tu, wiki moja, mbili, wao kwa wao wapenzi wanawasiliana wanaelewana wanarudiana. Wewe rafiki bila kujua hili wala lile unakuja kuta rafiki yako yuko na wazamani aliyekuwa anamponda vibay, nawe ulishiriki kumshauri aachane naye. Na keshamuambia 'unajua hny, hata rafiki yangu fulani alinisahuri eti nikupige chini kipindi kile'...
OFF TOPIC: Tuko hiyo avatar yako nilikuwa sijawahi kuiangalia vizuri l.o.l
 
angalia wa kumuomba ushauri,mtu mwenye matatizo ya kimapenzi au asiye na mpenzi sio mtu wa kumwomba ushauri otherwise awe ni mtu mwenye busara zake...moyo wa mtu unaficha mengi na siyo kila rafiki unayemwona anakupenda akawa anakupenda kweli au kukutakia mafanikio katika maisha yako ya kimapenzi..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom