Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,320
Ni rahisi sana kushauri hapa jukwaani.
Hata hivyo ni very tricky kushauri live hasa kwa rafiki yako. Ukweli ni kwamba mara nyingi rafiki yako anapokuhadisia juu ya mapungufu ya mpenzi wake, unaweza kupima na kuona kuwa ushauri sahihi ni kumwambia waachane. Ukimwambia hivyo atakukubalia, na kukushukuru, na kuendelea kumwaga ubaya juu ya huyo mpenzi wake kwako. Hata hivyo, wengi wa wanaopokea ushauri huwa hawaendi kuachana, na siku kadhaa baadaye utawakuta wanapendana sana na uwezekano ni mkubwa kuwa huyo rafiki yako alienda kumhadisia mpenzi wake jinsi alivyokuwa unamnanga na kumtaka waachane.
Yameshanikumba, na sasa niko makini sana kabla sijamwambia mtu, 'achana nae, hakufai'
naamini wanajamvi pia mpo ambao mmeshashuhudia hayo..
Hata hivyo ni very tricky kushauri live hasa kwa rafiki yako. Ukweli ni kwamba mara nyingi rafiki yako anapokuhadisia juu ya mapungufu ya mpenzi wake, unaweza kupima na kuona kuwa ushauri sahihi ni kumwambia waachane. Ukimwambia hivyo atakukubalia, na kukushukuru, na kuendelea kumwaga ubaya juu ya huyo mpenzi wake kwako. Hata hivyo, wengi wa wanaopokea ushauri huwa hawaendi kuachana, na siku kadhaa baadaye utawakuta wanapendana sana na uwezekano ni mkubwa kuwa huyo rafiki yako alienda kumhadisia mpenzi wake jinsi alivyokuwa unamnanga na kumtaka waachane.
Yameshanikumba, na sasa niko makini sana kabla sijamwambia mtu, 'achana nae, hakufai'
naamini wanajamvi pia mpo ambao mmeshashuhudia hayo..