Kuvimba kwa Tezi Dume (Benign Prostate Hyperplasia BPH) Featured

Jamaa anataka picha siyo michoro. Hata hivyo atapataje picha huku tezi dume limeshaondolewa? Hapo sasa!
 
nSpZPBqiung0CkOfDXZHqVWHAuAg9MkU-TfoJhw6PQ24jW8oKyFRFYlMeN83BqGZBDKifJrz8cLBwRs5pX6hpjoukTkrL6fOuyk3cmFteRijQ1Rh51UeaTjG3HQDYSXn8A

Watu wengi wamekuwa na shauku ya kutaka kujua ugonjwa wa saratani ya tezi dume, huku wakidhani ni mpya. Lakini ukweli ni kuwa umekuwapo miaka mingi na wengi wameugua.

Takwimu zinaonyesha wanaume wengi huugua ugonjwa huu unaoongezeka kwa kasi ya hali ya juu.

Kulingana na utafiti uliofanywa na Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORIC), kutoka mwaka 2006, zinaonyesha kuwa kila mwaka kumekuwa na ongezeko la kesi mpya ya wagonjwa saratani ya tezi dume.

Novemba ya kila mwaka, jumuiya za kimataifa huadhimisha tukio ambalo hujulikana kama Movemba.

Maadhimisho hayo huhusisha kukuza kwa masharubu, kukusanya fedha na kuleta mwamko na ufahamu wa masuala ya afya kwa wanaume kama vile saratani ya tezi dume.

Jina hilo la Movemba ni mchanganyiko wa neno ‘Masharubu na Novemba’.

Maadhimisho hayo ya mwezi mzima yanalenga kuongeza ufahamu na mwamko kwa kupima ili kugundua mapema.

Mwaka jana peke yake zaidi ya Dola za Marekani 120 milioni zilikusanywa.

Hadi sasa, Movemba imekusanya zaidi ya Dola 550 milioni kupitia wanachama wake milioni nne katika nchi 21 duniani kote.

Waziri mstaafu wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa alinukuliwa akisema asilimia 10 ya wagonjwa wanaosumbuliwa na aina mbalimbali za saratani wamejitokeza hospitalini kwa uchunguzi na matibabu.

Anasema asilimia 90 iliyobaki hawajafanya jitihada zozote kuhudhuria uchunguzi na matibabu.

Akizungumzia juu ya uchunguzi wa hali ya tezi dume nchini, Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Hospitali ya Apollo yenye makao makuu India, Dk Prathap Reddy anasema kuwa ugonjwa huo unaathiri watu wengi na kusababisha vifo vingi nchini kwa sababu ya ukosefu wa ufahamu wa kina juu ya ugonjwa huo.


Utaratibu wa uchunguzi wa saratani ya tezi dume haufanyiki kutokana na gharama na ukosefu vifaa vya uchunguzi nchini.

Watu wengi hurejea hospitali wakati ugonjwa huo upo katika hatua ya mwisho na hauwezi kuzuilika tena. Hata hivyo, kuna uwezekano wa ugonjwa huo kutibika endapo utagundulika mapema.

Pamoja na kuwapo kifaa maalumu cha utambuzi wa saratani ya tezi dume ‘chaprostate specific antigen’ (PSA) duniani, Watanzania wachache wana uwezo wa kupata huduma hii.

Kwa sababu kifaa hiki kina gharama kubwa na kinahitaji wafanyakazi wenye ujuzi na upimaji wenyewe ni gharama kubwa.

Mchungaji Dk Emmanuel Kandusi aliyenusurika na saratani ya tezi dume ana uzoefu wa kutosha juu ya ugonjwa huu na anajaribu kujenga ufahamu na uelewa kwa wananchi wenzake.

Tofauti na Watanzania wengi Dk Kandusi alikuwa na uwezo wa kupata matibabu ushauri kutoka nje ya nchi.

Wakati akiugua alikuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Apollo.

“Kutokana na maendeleo na upatikanaji wa vifaa muhimu na wafanyakazi wa kutosha katika hospital hiyo nilikuwa na uwezo wa kuokoa maisha yangu na kuanza kuwaelimisha wengine,” anasema.

Ukilinganisha mazingira yaliyoko katika hospitali za nje ya nchi kama Apollo na hali ya taasisi zetu za afya hakuna uwiano. Hadi sasa nchi ina kituo kimoja tu tiba ya mionzi ya saratani yaani ORCI.

Mahitaji ya wagonjwa wa saratani nchini haishabihiani na huduma zenyewe.

Kutokana na tatizo hili na ukweli kwamba ORCI hakiwezi kukidhi mahitaji yote ya wagonjwa wote wa aina mbalimbali za saratani, mathalani wagonjwa hulazimika kwenda kupata matibabu yao India hususani kwenye Hospitali za Apollo.

Saratani ya tezi dume ni aina ya saratani ambayo huanzia kwenye tezi za kibofu ya jinsia ya kiume itokanayo na ukuaji hafifu wa seli inayopelekea uvimbe katika tezi.


Baada ya hapo seli za saratani husambaa kutoka kwenye tezi dume kwenda sehemu nyingine za mwili hususan katika mifupa na matezi ambayo husababisha maumivu hasa katika kupitisha haja ndogo na wakati wa tendo la ndoa.

Hii ni aina ya saratani ambayo hushambulia zaidi wanaume walio juu ya miaka 50.

Tafiti zilizofanyika hivi karibuni zinaonyesha kuwa wanaume walio chini ya miaka 40 wana uwezo wa kupata saratani ya tezi dume kwa uwiano wa mtu mmoja kati ya 100,000.

Kwa wanaume walio kati ya miaka 70 na 74 wako katika hatari ya kupata saratani hiyo kwa wastani wa watu 1,326 kati ya 100,000.

Hali kadhalika inakisiwa mwanamume mmoja kati ya sita hupata saratani ya tezi dume katika maisha yao .

Kila mwaka kati ya wanaume wote wanaogundulika na saratani moja ya nne wana saratani ya tezi dume.

Desmond Tutu anasema ugonjwa huu wa saratani ya tezi dume kuwa hauna mipaka ya kijamii.

Dalili


  • Dalili za tezi dume ni matatizo katika mfumo wa haja ndogo pamoja na kwenda haja mara kwa mara hususan usiku na kushindwa kuistahimili kwa muda.
  • Hupata maumivu wakati wa mahusiano (ngono).
  • Matone ya damu kati haja ndogo, maumivu katika sehemu ya chini ya mgongo, upotevu wa hamu ya kula na kupungua uzito.



Ili kugundua saratani ya tezi dume, mgonjwa anahitaji uchunguzi wa kina katika njia yake ya haja ndogo ambako daktari hujaribu kuhisi uvimbe wowote utakao kuwa katika mfumo wa mkojo na matezi uchunguzi ambao hufuatiwa na vipimo vya damu.


Chanzo: Mwananchi

 
Baada ya miaka 50+ viungo vyote vya binafamu vinapungua uwezo wake wa kufanya kazi. Miongoni mwa viungo hivyo ni pamoja na tezi dume (prostate gland). Kazi ya tezi dume ni kuzalisha majimaji yanayohitajika kuosha na kusafirisha mbegu za kiume wakati Wa kujamiana ili zimwagike nje ya penis. Tezi dume linakaa kwenye njia ya mkojo. Baada ya miaka 50+ mwanaume anapaswa pia kupunguza (slow down) tabia ya kujamiana kila mara kwakuwa tezi dume limepunguza uwezo wake halisi Wa kutoa majimaji ya kutosha yanayohitajika kuzibeba sperms nje ya mwili wakati wa sex. Kama utaendelea na tabia yako ya ngono hata uzeeni, tezi dume litatafuta namna nyingine ya kuzalisha maji mengi yanayohitajika, miongoni mwa njia hizo ni kwa kutanuka na kuongezeka ukubwa wake kitendo kinachosababisha kuzuia njia ya haja ndogo na kusababisha mgonjwa ashindwe kukojoa vizuri. Hivyo speed ya kutanuka kwa tezi dume itategemea pia na kiasi cha ngono utakazofanya kwa siku,wiki,mwezi au mwaka. Baada ya miaka 50+ mwanaume anashauriwa apunguze ngono, angalau afanye mara moja tu kila baada ya wiki 2 inamtosha ili kuruhusu tezi dume kuzalisha polepole majimaji ya kutosha kwa njia ya kawaida. Hivyo epuka kuoa wasichana wadogo au kuwa na wanawake wengi katka umri mkubwa watakaokulazimisha ufanye ngono kila wakati kila siku na kulifanya tezi dume lifanye kazi ya ziada wakati limeshachoka. Kutanuka kwa matezi na viungo vingine kunapotokea hitilafu ni jambo la kawaida, mfano, kunapotokea upungufu wa madini joto (Iodine) mwilini husababisha tezi la shingo (thyroid) litanuke ili kujaribu kurekebisha upungufu huo, jambo linalosababisha uvimbe mbele ya shingo (goiter). Hata moyo unatanuka kupita kiasi mtu anapokuwa na shinikizo kubwa la damu la muda mrefu.

Uvimbe wa tezi dume unaweza kuwa wa kawaida (benign) au malignant (cancer) na dalili zake ni mkojo kutoka kwa shida na kuambatana na mauvimu au damu kidogo. Mgonjwa anajisikia kwenda haja ndogo kila wakati, maumivu, na homa kama atapata maambukizi kwenye mafigo. Tezi likitanuka kupita kiasi litasababisha kuzuia mkojo usitoke kabisaa kiasi cha kusababisha mgonjwa apatiwe usaidizi wa kukojoa kwa njia ya kupitisha mpira (catheter) sehemu za siri au ikishindikana kupasua tundu dogo la kukojolea chini ya kitovu. Wako wanaume wanaoanza kupata madhara ya kuvimba tezi dume mara tu baada ya kumaliza harakati za kujamiana (orgasm). Mzee wangu kimbilia hospitali mara moja kama unahisi una tatizo la kushindwa kukojoa vizuri kabla ya hujashindwa kabisa kukojoa. Kuwahi matibabu kutasaidia kuepusha kusambaa kwa chembe za cansa mwili mzima kama uvimbe utakuwa ni wa aina ya malignant.

Hata hivyo, ni rahisi pia kurithi tatizo la tezi dume kama umetokana na familia yenye historia ya akina-baba wenye tezi dume.
 
Naomba kujua tofauti ya mtu mwenye:
1.BUSHA.
2.TEZI DUME.
3.MSHIPA.

Ee Mola, tuepushe na magonjwa ya wazee wa Pwani !
 
Salamu !
Chai moto ya choya inapunguza athari za magonjwa ya wazee,kama saratani inayosababishwa na ulawiti na ufiraji !
 
Nimeeleza moja ya faida ya chai ya choya ni kupunguza kansa nk !

Hivyo,sijaeleza ili waendelee na ufiraji na kulawiti !
 
Salamu !
Chai moto ya choya inapunguza athari za magonjwa ya wazee,kama saratani inayosababishwa na ulawiti na ufiraji !

Ha ha ha. Mtoa uzi, para ya mwisho: Hivyo epuka kuoa wasichana wadogo! Wenyewe wanasema hao wasichana uwakatazao damu inachemka na wana miili ya moto!
 
Naomba kujua tofauti ya mtu mwenye:
1.BUSHA.
2.TEZI DUME.
3.MSHIPA.

Ee Mola, tuepushe na magonjwa ya wazee wa Pwani !

Busha (ngiri maji) ni maji yaliyotuama kwenye mfuko wa korodani (pumbu) kwasababu mbalimbali kama vile kuziba kwa mirija ya kusafirisha majitaka (lymphatics). Mishipa hii inaweza kuzibwa na minyoo midogo (filaria) inayoenezwa kwa kuumwa na mbu wa aina mbalimbali (Culex, ades, anopheles) na kusababisha matende na/au mabusha. Pia unaweza kupata busha kama ukiwa na hitilafu kwenye korodani (kupigwa, maambukizi kwenye korodani au kuzaliwa na hitilafu), mwanga wa tochi unapenya kwenye uvimbe wa busha. Mara nyingi hauna maumivu na unaweza kuzuia kwa kupambana na mazalia ya mbu, kulala kwenye chandarua na kunywa vidonge vya kuzuia mapusha na matende mara kwa mara. Upasuaji ndiyo matibabu ya busha lililozidi kiasi.

Mshipa/hernia (ngiri kavu) inasababishwa na kipande cha utumbo kushuka na kuelekea kwenye pumbu kupitia matundu (inguinal rings) yaliyotanuka kimakosa, hivyo kusababisha maumivu makali na uvimbe sehemu ya kinena. Uvimbe huu ni hatari sana unaweza kusababisha utumbo uonze kama ukibanwa sana. Uvimbe wa mshipa huwa unachezacheza (palsate) wakati wa kukohoa, na matibabu yake ni ya haraka (emergency) kwa njia ya upasuaji. Uvimbe wa hernia (mshipa) haupitishi mwanga wa tochi ukimulikwa. Sababu za mshipa ni kufanya kazi ngumu, mazoezi magumu, kubeba vitu vizito sana (mizigo, kunyanyua vyuma), kupata choo kigumu, kikohozi cha muda mrefu, kujisaidia bila kuchuchumaa au kuzaliwa ukiwa na hitilafu kwenye matundu ya inguinal.

Tezi dume linakaa kandokando ya njia ya kutolea mkojo (urethra) kutoka kwenye kibofu. Kazi yake ni kutoa majimaji yenye alikali ili kusafisha tindikali (acid) kwenye njia ya mkojo na ukeni ili kuzuia sperms zisiharibike zinapopita kwenye njia hizo. Pia inazibeba sperms kwenye maji hayo na kuzifanya zitoke kuelekea ukeni wakati wa kujamiana.
 
Busha (ngiri maji) ni maji yaliyotuama kwenye mfuko wa korodani (pumbu) kwasababu mbalimbali kama vile kuziba kwa mirija ya kusafirisha majitaka (lymphatics). Mishipa hii inaweza kuzibwa na minyoo midogo (filaria) inayoenezwa kwa kuumwa na mbu wa aina mbalimbali (Culex, ades, anopheles) na kusababisha matende na/au mabusha. Pia unaweza kupata busha kama ukiwa na hitilafu kwenye korodani (kupigwa, maambukizi kwenye korodani au kuzaliwa na hitilafu), mwanga wa tochi unapenya kwenye uvimbe wa busha. Mara nyingi hauna maumivu na unaweza kuzuia kwa kupambana na mazalia ya mbu, kulala kwenye chandarua na kunywa vidonge vya kuzuia mapusha na matende mara kwa mara. Upasuaji ndiyo matibabu ya busha lililozidi kiasi.

Mshipa/hernia (ngiri kavu) inasababishwa na kipande cha utumbo kushuka na kuelekea kwenye pumbu kupitia matundu (inguinal rings) yaliyotanuka kimakosa, hivyo kusababisha maumivu makali na uvimbe sehemu ya kinena. Uvimbe huu ni hatari sana unaweza kusababisha utumbo uonze kama ukibanwa sana. Uvimbe wa mshipa huwa unachezacheza (palsate) wakati wa kukohoa, na matibabu yake ni ya haraka (emergency) kwa njia ya upasuaji. Uvimbe wa hernia (mshipa) haupitishi mwanga wa tochi ukimulikwa. Sababu za mshipa ni kufanya kazi ngumu, mazoezi magumu, kubeba vitu vizito sana (mizigo, kunyanyua vyuma), kupata choo kigumu, kikohozi cha muda mrefu, kujisaidia bila kuchuchumaa au kuzaliwa ukiwa na hitilafu kwenye matundu ya inguinal.

Tezi dume linakaa kandokando ya njia ya kutolea mkojo (urethra) kutoka kwenye kibofu. Kazi yake ni kutoa majimaji yenye alikali ili kusafisha tindikali (acid) kwenye njia ya mkojo na ukeni ili kuzuia sperms zisiharibike zinapopita kwenye njia hizo. Pia inazibeba sperms kwenye maji hayo na kuzifanya zitoke kuelekea ukeni wakati wa kujamiana.
Mimi nilfanyiwa hiyo ya ngiri maji, pumbu haikuvimba sana na wala mie mwenyewe sikujua kama nina tatizo hilo, ilikuwa ya kulia lkn wakati niko theatre dkr akaniambia hata kushoto nayo ina tatizo na nikakubali kufanyiwa zote...tatizo langu ni kwamba mrija wa upande wa kulia kuunganisha kwenye uume huwa unaiuma sana na huwa inasababisha maumivu kwenye korodani ya kulia na some times uvimba kidogo....NAOMBA USHAURI WENU WADAU NIFANYEJE KWANI NIMESHAENDA HSPTL WAKASEMA SINA NGIRI, NIMEZUNGUKA HOSPITAL NYINGI NA NIPO TAYARI KWA OPERATION
 
Busha (ngiri maji) ni maji yaliyotuama kwenye mfuko wa korodani (pumbu) kwasababu mbalimbali kama vile kuziba kwa mirija ya kusafirisha majitaka (lymphatics). Mishipa hii inaweza kuzibwa na minyoo midogo (filaria) inayoenezwa kwa kuumwa na mbu wa aina mbalimbali (Culex, ades, anopheles) na kusababisha matende na/au mabusha. Pia unaweza kupata busha kama ukiwa na hitilafu kwenye korodani (kupigwa, maambukizi kwenye korodani au kuzaliwa na hitilafu), mwanga wa tochi unapenya kwenye uvimbe wa busha. Mara nyingi hauna maumivu na unaweza kuzuia kwa kupambana na mazalia ya mbu, kulala kwenye chandarua na kunywa vidonge vya kuzuia mapusha na matende mara kwa mara. Upasuaji ndiyo matibabu ya busha lililozidi kiasi.

Mshipa/hernia (ngiri kavu) inasababishwa na kipande cha utumbo kushuka na kuelekea kwenye pumbu kupitia matundu (inguinal rings) yaliyotanuka kimakosa, hivyo kusababisha maumivu makali na uvimbe sehemu ya kinena. Uvimbe huu ni hatari sana unaweza kusababisha utumbo uonze kama ukibanwa sana. Uvimbe wa mshipa huwa unachezacheza (palsate) wakati wa kukohoa, na matibabu yake ni ya haraka (emergency) kwa njia ya upasuaji. Uvimbe wa hernia (mshipa) haupitishi mwanga wa tochi ukimulikwa. Sababu za mshipa ni kufanya kazi ngumu, mazoezi magumu, kubeba vitu vizito sana (mizigo, kunyanyua vyuma), kupata choo kigumu, kikohozi cha muda mrefu, kujisaidia bila kuchuchumaa au kuzaliwa ukiwa na hitilafu kwenye matundu ya inguinal.

Tezi dume linakaa kandokando ya njia ya kutolea mkojo (urethra) kutoka kwenye kibofu. Kazi yake ni kutoa majimaji yenye alikali ili kusafisha tindikali (acid) kwenye njia ya mkojo na ukeni ili kuzuia sperms zisiharibike zinapopita kwenye njia hizo. Pia inazibeba sperms kwenye maji hayo na kuzifanya zitoke kuelekea ukeni wakati wa kujamiana.


Mungu akubariki kwa kazi nzuri.
 
Mimi nilfanyiwa hiyo ya ngiri maji, pumbu haikuvimba sana na wala mie mwenyewe sikujua kama nina tatizo hilo, ilikuwa ya kulia lkn wakati niko theatre dkr akaniambia hata kushoto nayo ina tatizo na nikakubali kufanyiwa zote...tatizo langu ni kwamba mrija wa upande wa kulia kuunganisha kwenye uume huwa unaiuma sana na huwa inasababisha maumivu kwenye korodani ya kulia na some times uvimba kidogo....NAOMBA USHAURI WENU WADAU NIFANYEJE KWANI NIMESHAENDA HSPTL WAKASEMA SINA NGIRI, NIMEZUNGUKA HOSPITAL NYINGI NA NIPO TAYARI KWA OPERATION

Pole sana, mara nyingi ngiri maji (busha) huwa haina maumivu, na hakuna sababu ya kufanyiwa upasuaji kama huna maumivu na uvimbe (mpira) ni mdogo tu, aliyekufanyia upasuaji alikusababishia majanga yasiyo ya lazima. Kutokana na maelezo yako nina wasiwasi kuwa ulikuwa huna busha (ngiri maji), vinginenyo ulihudumiwa na mtaalam asiye na ujuzi au uzoefu mkubwa wa kushuhulikia maradhi hayo. Mara nyingi Ngiri maji inahitaji upasuaji mdogo tu ili kuyamwaga maji na kupindua mfuko (tunica vaginalis) unaoruhusu maji kutuama kwenye pumbu. Labda wakati wa upasuaji mtaalamu alijeruhi au kufunga na viungo vingine visivyohusika na kusababisha shida yako unayojihisi. Rudi tena hospitali hata kama sio ile ile kitengo cha upasuaji (surgery) ukachunguzwe zaidi na kufaidika na utaalamu wa madaktari waliobobea na wenye uzoefu. Inshallah utapona. Tofautisha kati ya ngiri maji, ngiri kavu na shida nyingine za sehemu ya korodani kama uvimbe, maambukizi, na kuumia sehemu za mapumbu.
 
Uchakavu wa tezi dume na mwili kwa ujumla unaweza kuepukwa kwa kutumia viasili maalumu vinavyotokana na mimea.baadhi ya viasili hivyo muhimu ni kama beta carotenes,coumarins,dithiolthiones, glucosinalates, thiocynates,flavonoids,isoflavonoids,lignans,limonoids,polyphenols na sterols.viasili hivi hufanya mambo mengi sana mwilini baadhi ya mambo hayo ni kama antioxidants-kuzuia kuharibika kwa chembe hai,kuongeza kinga ya mwili,kuzuia kansa,kuondoa sumu mwilini,kuzuia uvimbe,kulinda mwili dhidi ya homoni mbaya,kurekebisha matumizi ya homoni mwilini.chanzo cha viasili hivi ni mimea.baadhi ya mimea hiyo ni karoti,spinachi,nyanya,magimbi,viazi vitamu,machungwa,malimao,ndimu,mabalungi,cabbage,broccoli,brussels sprouts,kale,pilipili,soya,mimea jamii ya mikunde,flax seed,dona za nafaka kama uwele mtama,ngano,ulezi,majani ya chai,cacao,zabibu nyekundu nk.
 
Asante sana kwa elimu hii! Naamini unautaalamu mkubwa na viungo vya uzazi vya mwanaume ndiomaana unatoa elimu hii, sorry, naomba unisaidie na hili: nina mdogo wangu (kwa sasa ana miaka 26) miaka kama mitatu iliyopita alikuwa akilalamika kuwa anaskia maumivu makali kwenye korodani zake hasa ya upande wa kushoto. Ilibidi twende hospitali kutafuta tiba. Baada ya kufanyiwa uchunguzi na wataalamu( kwa kuzigusagusa korodani zake hasa mishipa-hii ni kwa mujibu wa maelezo yake kuwa hakuna kifaa kilichotumika kumchunguza isipokuwa mikono ya daktari!).

Baada ya uchunguzi huo alishauriwa afanyiwe upasuaji mdogo kwenye korodani ya kushoto kwa maelezo kuwa kuna mishipa mingi imeota ambayo ilitakiwa kuondolewa. Madhara ya kutoitoa mishipa hiyo aliambiwa kuwa kwa baadae ingewezakumfanya asiwe na uwezo wa kumpa mimba mwanamke. Hivyo tulikubaliana afanye(ukizingatia daktari tulimuamini kwani ni specialist kutoka taasisi kubwa ya serikali hapa nchini). Sasa kilichonishangaza ni mara baada ya kupona kidonda cha oparesheni, korodani ilisinyaa na mpaka sasa imesinyaa(yaani ilikuwa ndogo sana kuliko ilivyokuwa mwanzo(SI KWAMBA MWANZO ILIVIMBA, ILIKUWA KAWAIDA TU) na pia si mara moja wala mara mbili namskia analalamika kuwa kuna kipindi anahisi maumivu kama yale yaliyosababisha afanyiwe opareshini japo yanakuja na kuondoka. Matatizo kama hayo yanasababishwa na nini? na kwanini korodani ilisinyaa baada ya oparesheni/ kuna uwezekano wowote wa kuwa iliharibiwa na oparesheni hivyohaiwezi kufanya kazi ten? Naomba msaada wako tafadhali.
 
Asante sana kwa elimu hii! Naamini unautaalamu mkubwa na viungo vya uzazi vya mwanaume ndiomaana unatoa elimu hii, sorry, naomba unisaidie na hili: nina mdogo wangu (kwa sasa ana miaka 26) miaka kama mitatu iliyopita alikuwa akilalamika kuwa anaskia maumivu makali kwenye korodani zake hasa ya upande wa kushoto. Ilibidi twende hospitali kutafuta tiba. Baada ya kufanyiwa uchunguzi na wataalamu( kwa kuzigusagusa korodani zake hasa mishipa-hii ni kwa mujibu wa maelezo yake kuwa hakuna kifaa kilichotumika kumchunguza isipokuwa mikono ya daktari!).

Baada ya uchunguzi huo alishauriwa afanyiwe upasuaji mdogo kwenye korodani ya kushoto kwa maelezo kuwa kuna mishipa mingi imeota ambayo ilitakiwa kuondolewa. Madhara ya kutoitoa mishipa hiyo aliambiwa kuwa kwa baadae ingewezakumfanya asiwe na uwezo wa kumpa mimba mwanamke. Hivyo tulikubaliana afanye(ukizingatia daktari tulimuamini kwani ni specialist kutoka taasisi kubwa ya serikali hapa nchini). Sasa kilichonishangaza ni mara baada ya kupona kidonda cha oparesheni, korodani ilisinyaa na mpaka sasa imesinyaa(yaani ilikuwa ndogo sana kuliko ilivyokuwa mwanzo(SI KWAMBA MWANZO ILIVIMBA, ILIKUWA KAWAIDA TU) na pia si mara moja wala mara mbili namskia analalamika kuwa kuna kipindi anahisi maumivu kama yale yaliyosababisha afanyiwe opareshini japo yanakuja na kuondoka. Matatizo kama hayo yanasababishwa na nini? na kwanini korodani ilisinyaa baada ya oparesheni/ kuna uwezekano wowote wa kuwa iliharibiwa na oparesheni hivyohaiwezi kufanya kazi ten? Naomba msaada wako tafadhali.

Mpe pole mdogo wako, Unajua nini!, pumbu ni mfuko mdogo sana kati kati ya mapaja lakini umeshindliliwa viungo vingi sana ndani yake. Kwenye kamfuko haka kuna tissues, korodani mbili, mirija (epididymis) mirefu sana zaidi ya mita 6 urefu na mirija mingine muhimu kwa uzazi. Ndani ya kamfuko haka pia kuna blood vessels, mishipa ya fahamu (nerves) mingi sana, mirija ya majitaka (lymphatic vessels) na kamba (spermatic cords) zinazozishikilia na kuzining'iniza korodani kutoka tumboni. Kazi ya viungo vyote hivi ni kuzipa korodani (testes) afya na mazingira mazuri ya kutengeneza sperms na kuzalisha homoni za kiume (androgens) hasa ile ya testosterone inayomfanya mwanaume awe mwanaume. Hii inapelekea korodani ziwe miongoni mwa viungo nyeti (sensitive) sana kwa mwanaume.

Hivyo basi, kitu chochote kwenye mapumbu kama vile upasuaji (operation), ajali, kupigwa, kukandamiza (kama vile kupanda baiskeli, kuendesha magari ya safari ndefu na madaladala mchana kutwa), joto kali, kuminya, kuvuta, kuvaa nguo zinazobana sana mapumbu, au maambukizi kwenye mapumbu kunaweza kusababisha hasara kubwa kwa mwanaume kwa urahisi.

Tatizo la kijana: Kutokana na wingi wa viungo ndani ya mfuko wa korodani inawezekana daktari kwa bahati mbaya wakati wa upasuaji huo alikata nerves na blood vessels zinazo-supply korodani husika, hivyo kusababisha kododani iparalize na kukosa damu ya kutosha inayopeleka virutubisho na hewa kwenye korodani husika, hivyo kusababisha korodani isinyae (dystrophy) kwa sababu ya kukatwa kwa mishipa hiyo muhimu. Hii ni kawaida kwa kiungo chochote kama kikiparalize huwa kinasinyaa iwe mkono au mguu.

Kuwa na subira: Mishipa ya damu na fahamu ina tabia ya kujitengeneza upya baada ya muda kupita, korodani inaweza kupata vyanzo vingine vya mishipa kutoka matawi (branches) mengine na kurejea hali yake baadaye.

Habari njema: Hata hiyo korodani moja nzima inaweza kumtosha kwa kazi za uzazi na uzalishaji wa homoni, aitunze vizuri isiudhulike. Hiyo korodani iliyosinyaa inawezekana nayo bado inafanya kazi. Mtu anaweza kubaki na kokwa moja tu bila kupungukiwa zaidi na kitu chochote.

Haya maumivu: Mpeleke hospitali akaripoti hayo maumivu ili apatiwe usaidizi, daktari atamchunguza, kufanyia vipimo (ultra sound), kumpa dawa, kurudia upasuaji au kuiondoa kabisa korodani yenye hitilafu kutokana na atakavyoona inafaa.
 
Pole sana, mara nyingi ngiri maji (busha) huwa haina maumivu, na hakuna sababu ya kufanyiwa upasuaji kama huna maumivu na uvimbe (mpira) ni mdogo tu, aliyekufanyia upasuaji alikusababishia majanga yasiyo ya lazima. Kutokana na maelezo yako nina wasiwasi kuwa ulikuwa huna busha (ngiri maji), vinginenyo ulihudumiwa na mtaalam asiye na ujuzi au uzoefu mkubwa wa kushuhulikia maradhi hayo. Mara nyingi Ngiri maji inahitaji upasuaji mdogo tu ili kuyamwaga maji na kupindua mfuko (tunica vaginalis) unaoruhusu maji kutuama kwenye pumbu. Labda wakati wa upasuaji mtaalamu alijeruhi au kufunga na viungo vingine visivyohusika na kusababisha shida yako unayojihisi. Rudi tena hospitali hata kama sio ile ile kitengo cha upasuaji (surgery) ukachunguzwe zaidi na kufaidika na utaalamu wa madaktari waliobobea na wenye uzoefu. Inshallah utapona. Tofautisha kati ya ngiri maji, ngiri kavu na shida nyingine za sehemu ya korodani kama uvimbe, maambukizi, na kuumia sehemu za mapumbu.
mkuu ubarikiwe sana, nashukuru kwa ushauri wako inshaallah nitarudi hospitali wanicheck tena....lkn kama hutojali nikutafute kama upo DAR ili nipate ushauri zaidi, kama una hospitali basi nitafarijika zaidi, NASUBIRI KUSIKIA KUTOKA KWAKO
 
Pole sana, mara nyingi ngiri maji (busha) huwa haina maumivu, na hakuna sababu ya kufanyiwa upasuaji kama huna maumivu na uvimbe (mpira) ni mdogo tu, aliyekufanyia upasuaji alikusababishia majanga yasiyo ya lazima. Kutokana na maelezo yako nina wasiwasi kuwa ulikuwa huna busha (ngiri maji), vinginenyo ulihudumiwa na mtaalam asiye na ujuzi au uzoefu mkubwa wa kushuhulikia maradhi hayo. Mara nyingi Ngiri maji inahitaji upasuaji mdogo tu ili kuyamwaga maji na kupindua mfuko (tunica vaginalis) unaoruhusu maji kutuama kwenye pumbu. Labda wakati wa upasuaji mtaalamu alijeruhi au kufunga na viungo vingine visivyohusika na kusababisha shida yako unayojihisi. Rudi tena hospitali hata kama sio ile ile kitengo cha upasuaji (surgery) ukachunguzwe zaidi na kufaidika na utaalamu wa madaktari waliobobea na wenye uzoefu. Inshallah utapona. Tofautisha kati ya ngiri maji, ngiri kavu na shida nyingine za sehemu ya korodani kama uvimbe, maambukizi, na kuumia sehemu za mapumbu.

kijana una vericocile nenda hosptal kubwa piga ultrs sound na gament analyss then ipasuaj stag 3 kama bado unaitaj mtoto
 
mpe pole mdogo wako, unajua nini!, pumbu ni mfuko mdogo sana kati kati ya mapaja lakini umeshindliliwa viungo vingi sana ndani yake. Kwenye kamfuko haka kuna tissues, korodani mbili, mirija (epididymis) mirefu sana zaidi ya mita 6 urefu na mirija mingine muhimu kwa uzazi. Ndani ya kamfuko haka pia kuna blood vessels, mishipa ya fahamu (nerves) mingi sana, mirija ya majitaka (lymphatic vessels) na kamba (spermatic cords) zinazozishikilia na kuzining'iniza korodani kutoka tumboni. Kazi ya viungo vyote hivi ni kuzipa korodani (testes) afya na mazingira mazuri ya kutengeneza sperms na kuzalisha homoni za kiume (androgens) hasa ile ya testosterone inayomfanya mwanaume awe mwanaume. Hii inapelekea korodani ziwe miongoni mwa viungo nyeti (sensitive) sana kwa mwanaume.

Hivyo basi, kitu chochote kwenye mapumbu kama vile upasuaji (operation), ajali, kupigwa, kukandamiza (kama vile kupanda baiskeli, kuendesha magari ya safari ndefu na madaladala mchana kutwa), joto kali, kuminya, kuvuta, kuvaa nguo zinazobana sana mapumbu, au maambukizi kwenye mapumbu kunaweza kusababisha hasara kubwa kwa mwanaume kwa urahisi.

Tatizo la kijana: Kutokana na wingi wa viungo ndani ya mfuko wa korodani inawezekana daktari kwa bahati mbaya wakati wa upasuaji huo alikata nerves na blood vessels zinazo-supply korodani husika, hivyo kusababisha kododani iparalize na kukosa damu ya kutosha inayopeleka virutubisho na hewa kwenye korodani husika, hivyo kusababisha korodani isinyae (dystrophy) kwa sababu ya kukatwa kwa mishipa hiyo muhimu. Hii ni kawaida kwa kiungo chochote kama kikiparalize huwa kinasinyaa iwe mkono au mguu.

Kuwa na subira: Mishipa ya damu na fahamu ina tabia ya kujitengeneza upya baada ya muda kupita, korodani inaweza kupata vyanzo vingine vya mishipa kutoka matawi (branches) mengine na kurejea hali yake baadaye.

Habari njema: Hata hiyo korodani moja nzima inaweza kumtosha kwa kazi za uzazi na uzalishaji wa homoni, aitunze vizuri isiudhulike. Hiyo korodani iliyosinyaa inawezekana nayo bado inafanya kazi. Mtu anaweza kubaki na kokwa moja tu bila kupungukiwa zaidi na kitu chochote.

Haya maumivu: Mpeleke hospitali akaripoti hayo maumivu ili apatiwe usaidizi, daktari atamchunguza, kufanyia vipimo (ultra sound), kumpa dawa, kurudia upasuaji au kuiondoa kabisa korodani yenye hitilafu kutokana na atakavyoona inafaa.


mpwa kaka mtu si ataparal...kabla ajamfikia mdogo wake kumweleza akuna maneno
 
Back
Top Bottom