mkuu nguo za chama huwa navaa ila sijawahi tinga nazo mwanza mjini kwani mimi ninaishi USAGARA kama unaenda busisi.
Embu na we jaribu kuvaa labda wamenionea tu hao watu walionizomea,nimechukia kweli leo
Awali ya yote niwasalimieni nyote.
Nilikuwa na safari ya kutoka sokoni hapa mwanza mjini na niliitaji kwenda hadi Kilimahewa nikaona nipite Makoroboi ili nipande hiace pale karibu na mataa.
Nimekutana na dhahama na kunyanyapaliwa kusiko na mfano mara niitwe teja,fisadi wengine wananisukuma bila sababu kisa nimevaa tisherti ya Ccm,kosa langu ni lipi hadi kufikia hata wenye hiace wanakataa nisipande gari yao?
Nimepatwa na hasira sana!