Numbisa
JF-Expert Member
- Dec 12, 2016
- 268,184
- 1,095,288
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania Simon Mwakifwamba, amelaumu kitendo cha msaniii mwenzao Wastara Juma kulalamika mitandaoni kuwa anaumwa na kuhitaji msaada, bila kutaarifu uongozi wake ili waweze kumsaidia. .
Akizungumza na EATV Mwakifwamba amesema ingawa wanafahamu kwamba Wastara ni mgonjwa, lakini taarifa za sasa hivi hajazipeleka kwao rasmi, na hivyo wameziona mitandaoni kama wasanii wengine walivyoona. .
Mwakifwamba ameendelea kwa kusema kuwa kitendo hicho si kizuri kwani inaonekana kama wamemtupa kitu ambacho sio kweli, kwani hata alipokuwa na matatizo kwa mara ya kwanza wao ndio walisimama mstari wa mbele kumsaidia, hata kabla mume wake Sajuki hajafariki. .
Licha ya hayo Mwakifwamba amesema wao kama shirikisho wameshaanza utaratibu wa kuweza kusaidia tatizo la Wastara ili aweze kupata matibabu.
Wiki iliyopita Wastara alitoa taarifa mitandaoni kuwa ana hali mbaya kwani mguu wake ambao ulishakatwa unazidi kumsumbua, na kuomba msaada kwa jamii kwa kumchangia chochote ili aweze kupatiwa matibabu. .
Hata hivyo, mapema January 2016 Wastara alitangaza mitandaoni kuwa na Hali mbaya ya mguu wake akisema anahitajika kwenda India na pesa hana, baadhi ya wasanii wenzake baada ya kusikia hilo walianza kuchangishana apate pesa za matibabu lakini usiku wa siku hiyo baadhi ya wasanii wenzake walishangaa Wastara akifunga ndoa na Sadifa iliyotajwa kuwa ya ghafla.
TAFF walikiri kushangaa waliyeambiwa ni mgonjwa anahitaji msaada akifunga ndoa kwa mujibu wa habari zilizochapishwa .
Akizungumza na EATV Mwakifwamba amesema ingawa wanafahamu kwamba Wastara ni mgonjwa, lakini taarifa za sasa hivi hajazipeleka kwao rasmi, na hivyo wameziona mitandaoni kama wasanii wengine walivyoona. .
Mwakifwamba ameendelea kwa kusema kuwa kitendo hicho si kizuri kwani inaonekana kama wamemtupa kitu ambacho sio kweli, kwani hata alipokuwa na matatizo kwa mara ya kwanza wao ndio walisimama mstari wa mbele kumsaidia, hata kabla mume wake Sajuki hajafariki. .
Licha ya hayo Mwakifwamba amesema wao kama shirikisho wameshaanza utaratibu wa kuweza kusaidia tatizo la Wastara ili aweze kupata matibabu.
Wiki iliyopita Wastara alitoa taarifa mitandaoni kuwa ana hali mbaya kwani mguu wake ambao ulishakatwa unazidi kumsumbua, na kuomba msaada kwa jamii kwa kumchangia chochote ili aweze kupatiwa matibabu. .
Hata hivyo, mapema January 2016 Wastara alitangaza mitandaoni kuwa na Hali mbaya ya mguu wake akisema anahitajika kwenda India na pesa hana, baadhi ya wasanii wenzake baada ya kusikia hilo walianza kuchangishana apate pesa za matibabu lakini usiku wa siku hiyo baadhi ya wasanii wenzake walishangaa Wastara akifunga ndoa na Sadifa iliyotajwa kuwa ya ghafla.
TAFF walikiri kushangaa waliyeambiwa ni mgonjwa anahitaji msaada akifunga ndoa kwa mujibu wa habari zilizochapishwa .