Habari za jioni wakuu,
Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu, naomba kuuliza kuhusu swala hili.
Juzi nilisafiri kutoka Dodoma kwenda kibondo, kuna kitu nilinotice kuanzia Tabora, nyakanazi, hadi kibondo kwenyewe. Kuna baadhi ya nyumba juu kwenye paa la bati, kwenye migongo wameweka zile nyaya (senyenge) ambazo mara nyingi unakuta zinawekwa juu ya fence ya nyumba kama security (achana na zile electric fence).
Kwa watalaam wa kanda hizo, zile waya hua zinasaidia nini? Bahati mbaya sikufanikiwa kupiga picha.