Kutoka KJ 832...JKT Ruvu

Kutoka KJ 832...JKT Ruvu

Mentor

JF-Expert Member
Joined
Oct 14, 2008
Posts
20,334
Reaction score
23,940
"Tuko na Halima Mdee, Nyambari Nyangwine, Tundu Lissu na wengine..."


Ujumbe mfupi from my young bro..naye yupo Ruvu...

Kila la heri huko...na muwe wazalendo kweli!!!
 
Hebu muulize ni kipi kipya wanachofundishwa tofauti na mwanzo ambacho kweli kitawafanya hawa wawe wazalendo.
 
Hawa ni wazee unadhani wataweza kula chakula
halafu wakimbie. Kichurachira,kukroo nani ataweza.

Hizo pit short&T shirt watavaa ama Kombati moja kwa moja. Watapigwa Nuwa kweli.
Miili yao imekomaa pia wiki 3 kwa Kuruta anatakiwa kukimbia smart area zote maana kijeshi wanasema hajui kutembea.

Naona kama kwa kuwa wanakwenda kama Waheshimiwa lazima Maafande watawanyenyekea.
 
Kweli jeshi limepooza wanaruhusu Kuruta kutumia simu na mafasibuku na twita???

Afande Marwa inakuwaje matwitta yanaopareti hadi geshini?? Mumeshindwa kazi??
 
Waheshimiwa wakirudi watuambie kama Malela bado anatafutwa au alipatikana. Pia watujuze hali ya Vibwende na kwa Babu.
 
Waheshimiwa wakirudi watuambie kama Malela bado anatafutwa au alipatikana. Pia watujuze hali ya Vibwende na kwa Babu.

Mkuu COPPER,Malela anaendelea kutafutwa kila depo Tz nzima.
 
Last edited by a moderator:
Kweli mmenikumbusha mbali sana enzi zangu za ruvu jkt enzi za mwalimu operation programe ya chama enzi za chama kimoja, ilikuwa fatiki mtindo mmoja nawakumbuka makuruta wenzangu fusi,kaburu,afande nyundo,mazani na ndabagoye pia ediwin tall na prosper mabingwa wa kujongo
 
Hawa wanataka kututania. Hebu wapigisheni kwata ile mliotupigisha enzi zile! Wenyewe watajifunza njia za kujongo. Nasubiri kusikia Mh. ... amekuwa Savimbi, mwingine malingerer, nk.
 
Kweli mmenikumbusha mbali sana enzi zangu za ruvu jkt enzi za mwalimu operation programe ya chama enzi za chama kimoja, ilikuwa fatiki mtindo mmoja nawakumbuka makuruta wenzangu fusi,kaburu,afande nyundo,mazani na ndabagoye pia ediwin tall na prosper mabingwa kujongo

Ulikuwa COY mkuu, mimi pia nilikuwa juko OP Program ya Chama. Tulianza na CO Col. Meena rukamaliza na Lt. Col Urio. Fusi na Kaburu ni kweli walikuwa huko intake hiyo,pia Michael Wambura, Faustine Ndugulile, Steven Omari, Dr Violet Lupondo, Dr Hamis Shabani, ZCO Ahmed Msangi, RCO Camillus Wambura, Ibrahim Natepe na wengine wengi. Maafande akina Cpl. Nyundo, Ssgt. Basekana, Major Dr. Omar, Major Rugaimukamu, Major Mwakitosi, WO II Manzani, Jerome, Sgt. Sahani na wengineo wengi. Nimelikumbuka sana Jeshi.
 
Kweli mmenikumbusha mbali sana enzi zangu za ruvu jkt enzi za mwalimu operation programe ya chama enzi za chama kimoja, ilikuwa fatiki mtindo mmoja nawakumbuka makuruta wenzangu fusi,kaburu,afande nyundo,mazani na ndabagoye pia ediwin tall na prosper mabingwa wa kujongo

CO alikuwa Col. Meena au mrhm ..., jina limenitoka. Namkumbuka Kitomari, afande medad, bila kusahau kwa bibi/babu.
 
Waheshimiwa wakirudi watuambie kama Malela bado anatafutwa au alipatikana. Pia watujuze hali ya Vibwende na kwa Babu.

Hahahaa! Unaikumbuka G coy? Ilipewa jina Go coy. Nakumbuka ilikuwa coy ya wazamiaji, ilipigwa bogi Cheetah.
 
"Tuko na Halima Mdee, Nyambari Nyangwine, Tundu Lissu na wengine..."


Ujumbe mfupi from my young bro..naye yupo Ruvu...

Kila la heri huko...na muwe wazalendo kweli!!!

Kwani Mhe. Tundu Lissu hakwenda JKT wakati ule ikiwa JKT ya ukweli ama ameamua/inaruhusiwa 'kubasti'

 
Ulikuwa COY mkuu, mimi pia nilikuwa juko OP Program ya Chama. Tulianza na CO Col. Meena rukamaliza na Lt. Col Urio. Fusi na Kaburu ni kweli walikuwa huko intake hiyo,pia Michael Wambura, Faustine Ndugulile, Steven Omari, Dr Violet Lupondo, Dr Hamis Shabani, ZCO Ahmed Msangi, RCO Camillus Wambura, Ibrahim Natepe na wengine wengi. Maafande akina Cpl. Nyundo, Ssgt. Basekana, Major Dr. Omar, Major Rugaimukamu, Major Mwakitosi, WO II Manzani, Jerome, Sgt. Sahani na wengineo wengi. Nimelikumbuka sana Jeshi.

Huyu Faustine ndiye yule aliyekuwa kipa wa timu? Nakumbuka jina la kwanza, mara ya mwisho nilimuona Muhimbili akisomea medicine. Dr Omar alifarika.
 
Hahahaa! Unaikumbuka G coy? Ilipewa jina Go coy. Nakumbuka ilikuwa coy ya wazamiaji, ilipigwa bogi Cheetah.

G COY naikumbuka, wao walipigwa bogi Chita, hata mm ilikuwa nipigwe bogi hilo nikajongo. Nasikia Chita MP ni simba na chui ni kweli au vipi? Medard namkumbuka sana alitupokea F COY ikiwa combania ya mapokezi 30/6/89, alitupiga cadebra hadi saa 5 usiku ndio akatupatia chakula yaani ugali wa mchana na maharage meupe kumbuka ndio tumetoka nyumbani siku ya kwanza hatuna mess tin wala chochote na baada ya hapo akatulaza ktk vitanga bila magodoro. Hakika kuna mengi ya kusimulia kuhusu msjeshi.
 
Back
Top Bottom