Kutoka KJ 832...JKT Ruvu

Kutoka KJ 832...JKT Ruvu

G COY naikumbuka, wao walipigwa bogi Chita, hata mm ilikuwa nipigwe bogi hilo nikajongo. Nasikia Chita MP ni simba na chui ni kweli au vipi? Medard namkumbuka sana alitupokea F COY ikiwa combania ya mapokezi 30/6/89, alitupiga cadebra hadi saa 5 usiku ndio akatupatia chakula yaani ugali wa mchana na maharage meupe kumbuka ndio tumetoka nyumbani siku ya kwanza hatuna mess tin wala chochote na baada ya hapo akatulaza ktk vitanga bila magodoro. Hakika kuna mengi ya kusimulia kuhusu msjeshi.

Wanasema hivyo khs Cheetah k/sbb njia za usafiri ziko mbali na kambi, na ktkt ni pori nene. Medad alikuwa anapenda sana kumbua nyakati za usiku.
 
upuuzi mtupu. tunadanganywa na wanasiasa! kwanza wote tayari ni saa 11 jioni, sasa jkt ili iweje?
 
mh wemekwenda kuhamasisha au kutuzuga au nini haswa?

kwa hiyo wala rushwa watakuwa wazalendo na rushwa tena basi?

nashauri mh. raisi aende jkt arudishe uzalendo
 
mtu kama nchemba hapaswi kuwekwa pamoja na vijana waliotoka sekondari juzi ATAWAHARIBU BURE.
 
JKT za siku hizi makuruta wanao muda wa kuchat twitter au facebook?
 
Bwana wee mimi nilikuwa D COY hapo ruvu jkt op programe ya chama kweli enzi zile lilikuwa jeshi kweli sio hili la wabunge nakumbuka hemedi msangi na makele waliingia mitini wakatimkia ccp polisi moshi bila taarifa hasa makele tulimtafuta vibwende mpaka tukazani ameliwa na simba na walitoka kwenye order mara nyingi ,kwakweli makele tulijua ameliwa na simba kama malela it's true story kwa watu wa ruvu najua mtakumbuka .
 
Bwana wee mimi nilikuwa D COY hapo ruvu jkt op programe ya chama kweli enzi zile lilikuwa jeshi kweli sio hili la wabunge nakumbuka hemedi msangi na makele waliingia mitini wakatimkia ccp polisi moshi bila taarifa hasa makele tulimtafuta vibwende mpaka tukazani ameliwa na simba na walitoka kwenye order mara nyingi ,kwakweli makele tulijua ameliwa na simba kama malela it's true story kwa watu wa ruvu najua mtakumbuka .
Umenifurahisha sana!
 
Hii ya JKT kuna agenda imejificha,
tusubiri lipo litakalodhihirika bayana!
Je hawa Wabunge watashiriki mkutano wa Bunge la bajeti? Kama sivyo, itakuwa ni hujuma ili kupitisha uozo kiurahisi. Pia, Wapiga kura tutakuwa tumekosa haki ya kuwakilishwa.
 
Hawa ni wazee unadhani wataweza kula chakula
halafu wakimbie. Kichurachira,kukroo nani ataweza.

Hizo pit short&T shirt watavaa ama Kombati moja kwa moja. Watapigwa Nuwa kweli.
Miili yao imekomaa pia wiki 3 kwa Kuruta anatakiwa kukimbia smart area zote maana kijeshi wanasema hajui kutembea.

Naona kama kwa kuwa wanakwenda kama Waheshimiwa lazima Maafande watawanyenyekea.

Wakiwanyenyeke watakuwa watu wa ajabu kweli kweli, nakumbuka zamani JKT intake ya form 6 tulisulubiwa sana kuliko ya form 4, kisa "nyie ndio mnajifanya mnakwenda kuwa mabosi huko". Na kumbuka wkt ule maafande wengi elimu,ilikuwa issue. Afande: wewe Kuruta, kwa nini huri chakura? Kuruta: sina appetite afande; Afande:Kuruta pumba flu kwerikweri, kwa nini huazimi kwa Kuruta mwenzie?"
 
Huyu Faustine ndiye yule aliyekuwa kipa wa timu? Nakumbuka jina la kwanza, mara ya mwisho nilimuona Muhimbili akisomea medicine. Dr Omar alifarika.

Mkuu ndiye yeye huyo Faustine Ndugulile.
 
Tundu Lissu tulikuwa naye kwanza Mafinga JKT halafu tukapigwa bogi kwenda Itende JKT. Jamaa alikuwa mtata kama hivi alivyo sasa. Kademu kake kalikuwa kanaitwa Suzana, kembamba kivi. Mimi niliondoka na bogi la KMT Chita kulinda reli na madaraja ya TAZARA.
 
Yaani natamani, ila niko private sector kazi mwanzo mwisho
 
Back
Top Bottom