Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,018
- 20,489
Wakuu wanamageuzi,
Poleni kwa propaganda za ccm kupitia magazeti yao ya Mtanzania nk.
Napenda kuwajuza kuwa kikao cha wakuu wa UKAWA bado kinaendelea vema kabisa, na mambo makubwa yote yameshapatiwa ufumbuzi ikiwemo taratibu za kumpata mgombea wa Urais na changamoto za vifungu vya katiba juu ya wagombea hao.
Pia utaratibu wa majimbo,vyote vimekamilika.
Hakuna chama kilichowasilisha barua yakujitoa wala aina yoyote ya kutokuelewana kunakoweza kupelekea kuvunjika kwa UKAWA kama ambavyo maadui zetu wanavyoeneza propaganda hizo,
Pia niwajuzi tu kuwa UKAWA hawajapokea ombi la mtu ama kikundi chochote kinachotaka kujiunga nao, na kwamba malengo na dhana nzima ya uwepo UKAWA yapo wazi kwa kila Mtanzania kuwa ni UMOJA WA KATIBA YA WANANCHI, na slogan ya ukawa ni "Utaifa wa Uzanzibar, Utanganyika na Utanzania"
Hivyo kikundi chochote kinachotaka kujiunga na Ukawa ni lazima kikubali kujikana na kuyabeba malengo ya wanaukawa. Sio UKAWA ufuate matakwa ya kikundi hicho.
Vuteni subira wakuu wa ukawa watatoa tamko rasmi baada ya kumaliza kikao chao.
Poleni kwa propaganda za ccm kupitia magazeti yao ya Mtanzania nk.
Napenda kuwajuza kuwa kikao cha wakuu wa UKAWA bado kinaendelea vema kabisa, na mambo makubwa yote yameshapatiwa ufumbuzi ikiwemo taratibu za kumpata mgombea wa Urais na changamoto za vifungu vya katiba juu ya wagombea hao.
Pia utaratibu wa majimbo,vyote vimekamilika.
Hakuna chama kilichowasilisha barua yakujitoa wala aina yoyote ya kutokuelewana kunakoweza kupelekea kuvunjika kwa UKAWA kama ambavyo maadui zetu wanavyoeneza propaganda hizo,
Pia niwajuzi tu kuwa UKAWA hawajapokea ombi la mtu ama kikundi chochote kinachotaka kujiunga nao, na kwamba malengo na dhana nzima ya uwepo UKAWA yapo wazi kwa kila Mtanzania kuwa ni UMOJA WA KATIBA YA WANANCHI, na slogan ya ukawa ni "Utaifa wa Uzanzibar, Utanganyika na Utanzania"
Hivyo kikundi chochote kinachotaka kujiunga na Ukawa ni lazima kikubali kujikana na kuyabeba malengo ya wanaukawa. Sio UKAWA ufuate matakwa ya kikundi hicho.
Vuteni subira wakuu wa ukawa watatoa tamko rasmi baada ya kumaliza kikao chao.