BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
KUTOKA KIJIWE CHA POLISI WASTAAFU..
Siyo kila nikisikiacho huwa nakiweka katika ukurasa wangu. Leo nilitembelewa na Polisi wastaafu. Wamesafiri kuja kunipa pole. Walipobisha hodi nikaweka mikono nyuma nikisubiri waweke pingu. Badala yake wakashusha kreti ya soda kunihani msiba.
Baadaye soga likanoga na mmoja wao akajenga hoja hizi:
1. Hakuna ubishi kuwa baadhi ya wananchi wanabambikiwa Kesi na Polisi. Rais SSH aliishalikemea hili.
2. Chadema wamekuwa wahanga wakubwa na namba 1 hapo juu. Kasoro hii inazaa chuki ktk nchi.
3. Mbowe kupanga kulipua vituo vya mafuta mwezi Agosti 2020 na akaachwa hadi Julai 2021 ni kumkosea adabu JPM aliyefariki mwezi Machi 2021.
4. Wananchi hawana shida sana kwa Mbowe kushtakiwa. Wana shida kwa kujua mwisho wa siku ataachiwa huru baada ya kuteswa na kupotezewa muda wake. Angekuwa na DHAMANA wala usingeona kelele hizi.
5. Watu wote wanabambikiwa kesi humuita Rais kuingilia kati. Baadhi yao wameachiwa. Huruma ya Rais haiwezi kumfikia kila mtu. Uhuru alio nao Rais unatakiwa katika taasisi.
6. Rais SSH anatakiwa kuanza upya. Hili ni eneo gumu lakini linawezekana. Afikirie yote au baadhi ya haya:
I) Avunje na kuunda upya Baraza la Mawaziri.
Ii) Avunje au aunde uongozi mpya wa bunge (unprecedented but possible)
III) Aitazame tena ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali
iv)Abadilishe miwani yake anayovaa na kuitazama upya timu yake ya usalama (security advisors team).
v) Atangaze uhuru wa habari na uhuru wa shughuli za Kisiasa.
Baada ya kuwasikiliza kwa makini nikakubaliana na ukweli kuwa hekima inaongezeka ukistaafu.
Polisi wastaafu wameniongezea hamu ya kustaafu ili niwe na hekima kama yao.
Askofu Bagonza
Siyo kila nikisikiacho huwa nakiweka katika ukurasa wangu. Leo nilitembelewa na Polisi wastaafu. Wamesafiri kuja kunipa pole. Walipobisha hodi nikaweka mikono nyuma nikisubiri waweke pingu. Badala yake wakashusha kreti ya soda kunihani msiba.
Baadaye soga likanoga na mmoja wao akajenga hoja hizi:
1. Hakuna ubishi kuwa baadhi ya wananchi wanabambikiwa Kesi na Polisi. Rais SSH aliishalikemea hili.
2. Chadema wamekuwa wahanga wakubwa na namba 1 hapo juu. Kasoro hii inazaa chuki ktk nchi.
3. Mbowe kupanga kulipua vituo vya mafuta mwezi Agosti 2020 na akaachwa hadi Julai 2021 ni kumkosea adabu JPM aliyefariki mwezi Machi 2021.
4. Wananchi hawana shida sana kwa Mbowe kushtakiwa. Wana shida kwa kujua mwisho wa siku ataachiwa huru baada ya kuteswa na kupotezewa muda wake. Angekuwa na DHAMANA wala usingeona kelele hizi.
5. Watu wote wanabambikiwa kesi humuita Rais kuingilia kati. Baadhi yao wameachiwa. Huruma ya Rais haiwezi kumfikia kila mtu. Uhuru alio nao Rais unatakiwa katika taasisi.
6. Rais SSH anatakiwa kuanza upya. Hili ni eneo gumu lakini linawezekana. Afikirie yote au baadhi ya haya:
I) Avunje na kuunda upya Baraza la Mawaziri.
Ii) Avunje au aunde uongozi mpya wa bunge (unprecedented but possible)
III) Aitazame tena ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali
iv)Abadilishe miwani yake anayovaa na kuitazama upya timu yake ya usalama (security advisors team).
v) Atangaze uhuru wa habari na uhuru wa shughuli za Kisiasa.
Baada ya kuwasikiliza kwa makini nikakubaliana na ukweli kuwa hekima inaongezeka ukistaafu.
Polisi wastaafu wameniongezea hamu ya kustaafu ili niwe na hekima kama yao.
Askofu Bagonza