Kutoka Kibanda Maiti - Zanzibar

Kutoka Kibanda Maiti - Zanzibar

Jamhuri ya Zanzibar

Senior Member
Joined
Jul 17, 2012
Posts
127
Reaction score
195
Wazanzibari wanadai mamlaka kamili ya nchi yaoMazruiMediaLive on USTREAM: We are broadcasting live from MazruiMedia Studio!. Local News

Mkutano mkubwa uliovuta hisia za wananchi wengi wa Visiwa vya Unguja na Pemba umefanyika leo hapa Unguja eneo la Kibanda Maiti. Mkutano huo uliokuwa ukitangazwa na vituo kadhaa vya radio hapa Visiwani imehudhuriwa na viongozi na watu maarufu hapa Zanzibar, huku Maalim Seif akiwa mzungumzaji mkubwa katika mkutano huo. Agenda ikiwa ni Muungano na Mamlaka kamili ya nchi ya Zanzibar.
Miongoni mwa mambo yalizungumzwa ni
1. Zanzibar kuwa na Serikali huru na yenye mamlaka kamili
2. Kuwa na Baraza lake la Mitihani - kwa madai kuwa NECTA inawafelisha Wazanzibar
3. Mamlaka ya huru ya Mapato na TRA kutokuwa na mamlaka ndani ya Zanzibar
4.Zanzibar kuwa na fedha yake - na sio kutumia shilingi ya Tanzania
5.Tume ya Uchaguzi yaani NEC na msajili wa Vyama kwa Zanzibar pekee
6. Zanzibar kuachiwa rasilimali zake
7. Wizara ya Mambo ya Ndani yake na wala sio ya MUungano
6.Wizara ya Fedha
7. Kushughulikia mambo yake ya kimataifa yenyewe
8. Kuwa na sera ya dini kwa sababu Zanzibar ni nchi ya Kiislam.
9.Kuwa na Bunge lake lenye mamlaka kamili
10. Kuwa na katiba yake ambayo haingiliani na katiba ya JMT

Madai mengi yametoa mwanga kwamba Wazanzibari wanaonewa na kunyanyaswa kwa sababu ya ujanja wa Mwl.Julius Kambarage Nyerere.

Kwa hapa Zanzibar, mazungumzo katika vijiwe vyote maarufu kama Jaws Corner, Malindi na Mkunazini ni habari ya Zanzibar Huru.............
 
Sijui serikali inasita nini kuwasikiliza hawa watu!Tumeshachoshwa na kelele zao wangepewa tu nchi yao!Kwanza Bara tutajiongezea mapato kwa makusanyo ya Kodi Kariakoo,Ilala na Tandika toka kwenye maduka ya wawekezaji toka Zanzibar maana tutawahesabu kama raia wa kigeni kama wachina na wahindi na hivyo watatulipa zaidi. Huu Muungano uvunjwe tu sasa tumechoka!!!!
 
Mngekuwa na busara kwana kudai wapemba na waunguja wanaofanya biashara na kujenga kila siku huku bara waje huko visiwani kwao wawekeze na kujenga.Muungano ukivunjika wote watakuwa foreigners na kuishi na kufanya kazi huku bara watatakiwa kuwa na legal permits!
 
Muungano kama koti

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mie nadhani wangekwenda kudai kwenye Mkaburi ya waasisi wa Muungano, sasa hapo Kibanda MAITI wanamdai nani?
Nawapa pole sana hao jamaa zangu
Hapo nakubaliana na maneno ya kamanda mnyika kuwa viongozi lege lege huzaa serikali dhaifu. na tutashuhudia mengi kwa kipindi hiki cha jk. lakini aliapa kuilinda katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania
 
go! Zanzibar go!!!!

kama mnachelewa hivi.!
 
Mie nadhani wangekwenda kudai kwenye Mkaburi ya waasisi wa Muungano, sasa hapo Kibanda MAITI wanamdai nani?
Nawapa pole sana hao jamaa zangu

Umeanzalini kuwashauri watu juu ya Ushirikina ? Since when makaburi yakadaiwa..... Umechanganyikiwa ?

Hata wakisimama katikati ya Bahari na kudai Uhuru wao wewe kinakuuma nini ?

Isiyoowasha hujailambaa.... Waacheni wapumue na nchi yao !
 
Hivi Mzee Moyo yupo hapo Kibanda maiti ? Hahaha hahaha hahhaaaa...

Msalimieni sana my Mentor ! Natamani Zanzibar ipate uhuru wake leo leo isifike hata kesho !
 
Hiyo kodi kariakoo sio issue kwani wazenji wapo bara tu hata uk na sehemu zingine ulimwenguni kua na akili wewe
 
Mie nadhani wangekwenda kudai kwenye Mkaburi ya waasisi wa Muungano, sasa hapo Kibanda MAITI wanamdai nani?
Nawapa pole sana hao jamaa zangu

Wao wamekwenda kudai kibanda maiti na makaburini kuna maiti sasa tofauti iko wapi? Wao ndio wameamua kwenda kibanda maiti basi waache wajinomee
 
Mm sioni sababu ya kuwanyima uhuru wao coz muungano ni makubaliano ya nchi mbili kama upande mmoja hawataki, basi uvunjwe kama kutakuwa na umuhimu watauungana tena kipindi kingine kwa misingi ambayo kila upande utarithia.
 
Back
Top Bottom