Kusoma UDSM ni dhamana

Kusoma UDSM ni dhamana

Ukweli mtupu,nina rafiki yangu kasoma St John University - Dodoma,ila Fb kaandika Amesoma UDSM,mwingine Makumira - Arusha,ila nae kaandika UDSM.


Hivi unaanzaje kusema umesoma Makumira Mkuu. Binadamu hupenda utukufu ndio maana hata humu wengi ni pangu pakavu lakini wanajitia matawi ya juu
 
Huyo ni mnyakyusa aisee, hawanaga tofauti na wahaya, niliwahi sema bola nisioe kuliko kuoa hili kabila. Mimi ni kabila langu ndio lkn sikutaka nizae pure mnyakyusa ili nipunguze haya makando kando km mnavyoona.


Ningekuwa Mnyakyusa ningejiua muda sana. Sina uhusiano wowote na jamii hiyo. Sina hata aliyewahi kuwa rafiki kutoka jamii tajwa hapo
 
Joka leo mzee baba kati ya siku zote umeandika ugoro kwa mara ya kwanza. Unaweza ukawa na sababu zako, ila kwa kuwa na wewe umesoma UDSM usitake kupitisha kauli hii kuwa sahihi mzee dingi umechemka hapa.

Ni viongozi wangapi wa nchi wenye nyadhifa kubwa ambao wamesoma hapo lakini ni wasomi uchwara tena wachumia matumbo?

Mimi nadhani kwenye mustakabali wa nchi na maendeleo kiujumla kipaumbele hakipaswi kuangalia eti mtu amesoma wapi. Tuangalie huyu mtu anajua nini na anaweza kuleta jipya gani.

UDSM wasomi uchwara kibao tu tumejazana humu mitaani.


Mkuu, huu ugoro ni kimasai lazima upige chafya tuu hakuna namna. Ndio maana nikasema mtu huweza kuwa amesoma Udsm lakini bado ni popoma tuu.

Ninachozungumzia hapa ni ile kasumba ya watanzania waliowengi kuwapa hadhi kubwa wasomi wa Udsm kiasi kwamba mhitimu kutoka chuo hicho akiboronga inakuwa ni fedheha kwake. Ipo tofauti kubwa endapo mhitimu wa Udsm akifanya makosa na asiye mhitimu wa chuo hiko. Mhitimu wa Udsm atalaumiwa zaidi kuliko aliko asiye wa udsm.
 
Kusoma UDSM halafu unakaa miaka 4 huna ajira na wenzako wamesoma SAUT na wameajiriwa mwaka mmoja toka wamalize kipi bora? Ikiwa mlimaliza pamoja?

Kuna mmoja kamaliza hapo alikua sifa kibao kisa UDSM mwaka wa nne sasa yupo nyumbani.


Hahahahah!! Mwambie aje nimpe ajira.
 
Kwenye swala la ajira inategemea ni wapi, nenda viwandani huko ukajionee wahitumu na mainjinia wa Arusha tech aka. ATC, DIT na MUST walivyotawala anga na huwezi waskia wakijitapa kuhusu vyuo walivyotok utawatambua kwa kazi zao.

Kuhusu UDSM nakiheshimu sana hiki chuo maana ni chuo mama hapa nchini ila kinachoniskitisha ni viongozi wengi waliolitumbikiza taifa kwenye dimbwi la rushwa na ufisadi ni wahitimu wa hiki chuo chetu bora sasa sijui kwa upande wa maadili na uzalendo UDSM wamekaaje maana elumu bora bila maadili na uzalendo haiwezi kulikumboa taifa.


Umeongea hoja mkuu. Ila uliona wapi mtu akajisifu kwa udhaifu. Mtu hujisifu endapo anaona zipo sababu za kufanya hivyo.
 
Nilienda kufanya field sehemu fulani walikuwa wananiita 'Yule kijana wa chuo kikuu'. Tulikuwa pale na vijana kutoka vyuo vingine lakini walikuwa wanaitwa kwa majina yao.


Acha mikwala wewe. Hiyo Udsm inakusaidia nini? Teh..teheh
 
Mkuu
Ile Siku Alikuwa Anawaponda Pale Pale Wanaona


Raha ni kuwa anayewaponda naye ni wa-Udsm. Hakuna kichekesho kama mtu kutoka chuo kingine hata akiwa ni boss wako akikufokea wewe uliyetoka Udsm. Hhahahaha
 
Back
Top Bottom