Huu uzi umeshachangiwa sana na sijataka kusoma maoni ya wadau wengine wameandika nini. Nafahamu utakuwa umeshaambiwa ukweli wa kutosha lakini wacha nikomelee msumari juu ya misumari.
Huu ujinga wa kila siku mnakesha kwenye mitandao ya kijamii mkiwatukana na kuwadiscourage viongozi wetu watatu; Mh. Mbowe, Katibu Mkuu Dr. Slaa na Kamanda Heche hautawasaidia chochote zaidi ya kuwazika ninyi wenyewe kisiasa.
Vijana wanamiminika kujiunga na Chadema kwakuwa pamojja na mambo mengine wameridhikka na utendaji kazi wa mwenyekiti wa Bavicha chini ya uenyekiti wa Kamanda Heche. Kila mara tunashuhudia kwenye television, redio, magazeti na mitandao ya kijamii Heche akifanya mikutano maeneo mbalimbali. Ni juzijuzi tu ametoka kufanya mikutano mjini Sumbawanga, tena sasahivi Heche anaungwa mkono sana na watu wa rika zote.
Kamanda Heche amefanya mikutano ya hadhara na ya ndani mikoa kama ya Arusha, Morogoro, Rukwa, Katavi, Dar es salaam, Mara, Mwanza, Shinyanga, Ruvuma, Iringa, Mbeya, Tabora n.k. Sasa mtu unapokurupuka na kuja na allegations za kipuuzi kama hizi eti Heche anakaa ofisini tu ni zaidi ya kuwa na kichwa nazi. Hata viongozi wa ccm wa ngazi ya kitaifa hawawezi kukusanya watu wengi kama anao wakusanya Heche katika mikutano yake.
Kama mlitaka Heche awe anafanya kazi ambayo haina maslahi kwa chama bali kwa maslahi yenu waganga njaa ni haki yenu kumuona mbaya kwakuwa hakuchaguliwa kuwatumika waganga njaa wachache bali kukijenga Chadema hasa kushawishi vijana wa aina zote, wasomi na wasio wasomi kujiunga na Chadema. Leo hii ccm inahangaika kuwarubuni na kuwahonga vijana ili wabadilishe muelekeo na kuiunga mkono, si kutoka vyuo vikuu ama sekondari vijana wanamiminika kuingia Chadema, kama si kazi nzuri ya mwenyekiti wa Bavicha hao vijana wanoingia Chadema kila kukicha wanavutiwa na nani?
Badala ya kukesha mkipika majungu dhidi ya viongozi wetu ni muhimu mjitafutie shughuli halali za kuwainbgizia vipato vya kila siku ili muache kutumiwa na ccm kuwachafua viongozi wetu wakakamavu. Na Mungu mkubwa aliwapa busara wajumbe wa kamati kuu na kuweza jutambua hila mlizokuwa nazo wakati mnagombea uongozi Bavicha na hivyo kuenguliwa, vinginevyo leo hii tungekuwa tunalia na kusaga meno. Watu wa ajabu sana nyie mnaopewa vijisenti vya mlo wa siku mbili tu mnakubali kuwatukana na kuwakashifu viongozi wenu hata hamuoni aibu? hata mkiambiwa muwatukane baba zenu kwakuwa mnapewa hela na chemba bila shaka mtawatukana kwakuwa mmepoteza uwezo wa kufikiria na kuamua, mmeshikwa akili na hao wanaowatuma.