Kuscratch kwa ITV kupitia Star Times

Kuscratch kwa ITV kupitia Star Times

Kwa muda wa zaidi ya wiki mbili kuna maeneo kadhaa hapa nchini pamoja na nyumbani kwangu, ambapo matangazo ya ITV & EATV (Startimes) yamekuwa yanakwama sana na kutoa picha mbaya na tena ni kuanzia saa 11 jioni hadi saa 5 usiku. Sasa ni hivi kwa upande wangu ninapoona matangazo ya ITV hayaonekani vizuri huwa ni bora nikazima TV kuliko kuangalia habari ya TBCCCM.

Nawasilisha wakuu.
KILAKA.

ukweli ni kuwa ITV na EATV ni makampuni yanayoikosoa sana sirikali na ndio maana wanakomolewa na TBC na startime take.
 
Hata kwangu itv ni tatizo kweli taarifa ya habari ya saa 2 usk kutazama ni shida kubwa,startimes haitufai tena WATANZANIA na hao wafanyabiasha wa kichina wafanye biashara waache ujinga unless watapata hasara kwa upumbavu wao

Hapa ninachokiona ni kwamba kampuni ya startimes watajiaribia, watafanya watu waache kutumia ving'amuzi vyao na badala yake waanze kutumia ting,continental,zuku,azam,digitek, dstv.
STARTIMES WANAJIMALIZA.
 
TBC ina hisa za kumwaga STARTIMES kwahiyo haishangazi sana kwa yanayotokea, sema huu ni ushamba na kushindwa kiushindani

TBC wameshindwa kiushindani kwa sababu moja kuu: kuwalinda watawala(CCM), TBC waige kutoka BBC(hii stesheni inaangaliwa hadi njee ya UK) sasa hivi watu wana chaguzi nyingi kwa hiyo kama hautatoa habari nzuri watahama watakwenda stesheni nyingine.
 
mbona startimes wanapitisha maandishi kwenye screen wakiweka wazi tatizo ni nini?? hayo maandishi yanasema 'KUNA MUINGILIANO KWENYE CHANNELS ZA ITV NA EATV NA WAMESHAWAAMBIA TCRA WATATUE HILO TATIZO KWANI LIKO NJE YA UWEZO WAO' sidhani kama kuna hujuma hapo.

Mkuu hujuma hipo, kwa sababu huo muingiliano huna mda maalum ambao ni saa 11 jioni hadi saa 5 usiku. Hii inatokana na nini???
 
mkuu hujuma hipo, kwa sababu huo muingiliano huna mda maalum ambao ni saa 11 jioni hadi saa 5 usiku. Hii inatokana na nini???

haya mkuu...mi sina utaalam wa hayo mambo.
 
Mkuu baada ya kuona Uzi huu Jana ilibidi niangalie taarifa ya habari ya ITV kupitia star times ikawa inakwamakwama ila now asubuhi iko fresh kabisa.
Kwahiyo hayo maingiliano ya mawimbi yanakuwepo jioni na usiku tu

Huku kucheza cheza na kukwama kunakuwepo kuanzia saa 11 jioni hadi saa 5 usiku, hali hii imedumu kwa zaidi ya wiki mbili sasa.
 
kwa muda wa zaidi ya wiki mbili kuna maeneo kadhaa hapa nchini pamoja na nyumbani kwangu, ambapo matangazo ya itv & eatv (startimes) yamekuwa yanakwama sana na kutoa picha mbaya na tena ni kuanzia saa 11 jioni hadi saa 5 usiku. Sasa ni hivi kwa upande wangu ninapoona matangazo ya itv hayaonekani vizuri huwa ni bora nikazima tv kuliko kuangalia habari ya tbc.

Nawasilisha wakuu.
Kilaka.

waache visingizio ushindani umewashinda wanapotea polepole
 
startimes hutumia backbones za tbc kurusha matangazo. wasioitaka tbc hawatumii startimes.
 
KILAKA

Ni kwamba ITV na EATV wanahujumiwa na Startimes au ni wao wanaihujumu Startimes? Kumbuka kwamba, IPP Media waligoma kuweka stations zao kwa Startimes na ilifikia wakati wakaziondoa lakini baada ya kukomaliwa na TCRA, ndipo wakazirudisha! Na si hao tu, hata Star TV nao waliondoa channel kwenye Startimes lakini wakarudisha kwa kulazimishwa! Wote hao, yaani ITV, Star TV na EATV zinapatikana kwa shida sana Startimes... lakini kupitia DSTV, hakuna matatizo!

Hivyo basi, kama kuna hujuma basi hujuma hizi ni kinyume na hivyo unavyosema!
 
Last edited by a moderator:
KILAKA

Ni kwamba ITV na EATV wanahujumiwa na Startimes au ni wao wanaihujumu Startimes? Kumbuka kwamba, IPP Media waligoma kuweka stations zao kwa Startimes na ilifikia wakati wakaziondoa lakini baada ya kukomaliwa na TCRA, ndipo wakazirudisha! Na si hao tu, hata Star TV nao waliondoa channel kwenye Startimes lakini wakarudisha kwa kulazimishwa! Wote hao, yaani ITV, Star TV na EATV zinapatikana kwa shida sana Startimes... lakini kupitia DSTV, hakuna matatizo!

Hivyo basi, kama kuna hujuma basi hujuma hizi ni kinyume na hivyo unavyosema!

Unamaanisha star tv,itv eatv wao ndio wanavuruga matangazo yao???
ili iweje???
 
Last edited by a moderator:
Mkuu hujuma hipo, kwa sababu huo muingiliano huna mda maalum ambao ni saa 11 jioni hadi saa 5 usiku. Hii inatokana na nini???
Ikiwa unahujumiwa na Startimes basi fahamu kwamba hiyo itakuwa ni hujuma pendwa kwa ITV/EATV wenyewe kwa kuwa hawataki kuwapo Startimes... hawa wanaamini njia pekee ya kufanya ving'amuzi vyao vya Digitek kuuzika sokoni ni kuiondoa ITV kutoka Startimes ambako inapatikana bure kwa watazamaji wakati ndio kituo kinachotegemewa zaidi kwa habari!
 
Unamaanisha star tv,itv eatv wao ndio wanavuruga matangazo yao???
ili iweje???
Iweje vipi si nimeshakufafanunulia? Hawa wote, ITV, EATV na Star Tv hawataki channel zao kuwa Startimes na walishawahi kuziondoa sema wakalazimishwa kuzirudisha! Usisahau kwamba, ITV/EATV wana ving'amuzi vyao (Digitek) na Star Tv wana ving'amuzi vyao (Continental). Walitaka kujiondoa Startimes kama njia ya kuwafanya watu wanunue ving'amuzi vyao sema ndo hivyo tena, sheria ikawabana!
 
Iweje vipi si nimeshakufafanunulia? Hawa wote, ITV, EATV na Star Tv hawataki channel zao kuwa Startimes na walishawahi kuziondoa sema wakalazimishwa kuzirudisha! Usisahau kwamba, ITV/EATV wana ving'amuzi vyao (Digitek) na Star Tv wana ving'amuzi vyao (Continental). Walitaka kujiondoa Startimes kama njia ya kuwafanya watu wanunue ving'amuzi vyao sema ndo hivyo tena, sheria ikawabana!

Sijajua kwa nini umeamua kuja kutudanganya, wewe ni mfanyakazi wa startimes???
 
Mkuu ni kweli kabisa. Nimekuwa nikijiuliza maswali yasiyo na majibu. Lakini kama kweli ni hujuma ya Startimes ambao wako chini ya TBC, basi watakuwa wanakata tawi la mti wakiwa wamelikalia.
Mimi nimeshalitupilia mbali hilo decoder lao sasa hivi vipo na Azam.
 
Back
Top Bottom