mmmuhumba
JF-Expert Member
- Nov 8, 2017
- 491
- 476
Mkasa wa kwanza
1.Tukiwa wote mapokezi, tulipewa kitabu tuandike majina, lakini mpenzi wangu akakataa, akataka mimi ndiyo niandike tu.
Nami nikakataa, nikiwa na hofu, kwanini yeye hataki kuandika kwani yeye si ndiyo mwanaume wangu na ndiyo kanileta na ndiye atayelala!.
Tumezozana, mwisho eti kakasirika akaamua kuondoka zake, basi nami nikaita boda boda na kurudi kwangu.
Kwani kati ya mwanaume na mwanamke nani anatakiwa awe na jukumu la kuandika jina la chumba?
Na kwanini mtu aogope kuandika jina ikiwa hajadaiwa hata Nida?.
Mkasa wa pili
2. Nikiwa chumbani, mhudumu alileta kitabu cha kusajili wanaolala pale gesti, mwenzangu alikuwa chooni.
Nilikipokea na kuangalia sehemu ya kuandika, najuta sijui kwanini nilisoma majina yasiyonihusu, niliposoma nikakutana na jina la mwanaume wangu niliyekuwa naye, kutizama mpaka namba ya simu ni yake. Kumbe siku mbili nyuma alikuja hapa na kulala, lakini mbona hakuniambia na sio kawaida yake.
Nilimuomba mhudumu aondoke, yaani nilijua kubeba vitu vyangu na kuondoka.
Inamaana ile gesti ndiyo kafanya kama ndio nyumba yake ya upasuaji?.
#imarika na mmmuhumba
#Mikasa ya mapenzi ipo na unaisoma inakupa nafasi ya kujijenga, kama uko na tabia hiyo ujiweke sawa.
1.Tukiwa wote mapokezi, tulipewa kitabu tuandike majina, lakini mpenzi wangu akakataa, akataka mimi ndiyo niandike tu.
Nami nikakataa, nikiwa na hofu, kwanini yeye hataki kuandika kwani yeye si ndiyo mwanaume wangu na ndiyo kanileta na ndiye atayelala!.
Tumezozana, mwisho eti kakasirika akaamua kuondoka zake, basi nami nikaita boda boda na kurudi kwangu.
Kwani kati ya mwanaume na mwanamke nani anatakiwa awe na jukumu la kuandika jina la chumba?
Na kwanini mtu aogope kuandika jina ikiwa hajadaiwa hata Nida?.
Mkasa wa pili
2. Nikiwa chumbani, mhudumu alileta kitabu cha kusajili wanaolala pale gesti, mwenzangu alikuwa chooni.
Nilikipokea na kuangalia sehemu ya kuandika, najuta sijui kwanini nilisoma majina yasiyonihusu, niliposoma nikakutana na jina la mwanaume wangu niliyekuwa naye, kutizama mpaka namba ya simu ni yake. Kumbe siku mbili nyuma alikuja hapa na kulala, lakini mbona hakuniambia na sio kawaida yake.
Nilimuomba mhudumu aondoke, yaani nilijua kubeba vitu vyangu na kuondoka.
Inamaana ile gesti ndiyo kafanya kama ndio nyumba yake ya upasuaji?.
#imarika na mmmuhumba
#Mikasa ya mapenzi ipo na unaisoma inakupa nafasi ya kujijenga, kama uko na tabia hiyo ujiweke sawa.