Nimelazimika kupiga kura ya maoni kutokana na kwamba nilipobofia kuendelea kusoma michango ya WanaJF juu ya hili suala kompyuta ilikataa kuendelea.
Hata hivyo nilipiga kura kwa Dr Slaa, kwa sababu kwa mujibu wa Katiba ya sasa, Zitto hawezi kuwa mgombea u-Rais kutokana na umri. Hatakuwa na miaka 40 mwaka 2015.
Najua kuna kampeni, hasa miongoni mwa vijana, kupunguza hiyo miaka 40 kufikia 35 kama ilivyo huko Merikani. Lakini Zitto akijiingiza ktk hiyo kampeni waziwazi mbele ya hii Tume ya Warioba, ataonekana ni m'binafsi kiasi cha kutaka kubadilisha Katiba kwa maslahi yake binafsi.!!!!!!!
Hata hivyo, MwanaJF mmoja ameshaorodhesha, kabla yangu, sifa nne stahiki za Mtanzania ambaye anastahili kuwa mteule wa Chama na mimi singetaka kuongeza. Lakini niongeze kwamba hii hoja (ya Zitto au Slaa) ni premature (bado wakati wake). Hakuna kipengele au Ibara ya Katiba ya sasa, au hata ya Katiba tunayoandaa, inaweza kumnyima Raia wa Tz kogombea u-Rais eti kwa sababu ameingia katika chama cha siasa siku za karibuni.