Kura ya Hapana yazidi kupaa CHADEMA , Humphrey Polepole, Prof. Lwaitama na Askofu

mimi nnachokiona n hv,
ccm wanatafta kuja za ndyo, nahc watafanya mchezo mchafu, km huu, Wanavyokwenda kwa wananchi wanatoa ya Warioba, wananchi wanapga ndyooo,
zen kwenye majumuisho watasema katiba ya Chenge + 6 ndyo ilipgiwa ndyo, so itapitishwa hyohyo, hawa watu wanawezafanya hvyo,
My take: WANANCHI KUWENI MAKIN PALE MTAKAPOLETEWA KATIBA PENDEKEZWA NI IP IL UPIGAPO KUJA UJUE UMEPGIA IP,
Nawasilisha:

hivi wananchi gani hao unaowaona wajinga kiasi hicho? Hakika mmeliwa na warioba wenu
 
Katiba hii pendekezwa ni mbaya kwa sababu;-


3. Madaraka ya rais kupunguzwa kama ilivyopendekeza tume ya Warioba imefutwa madhara yake,mashemeji wa mke wa rais, marafiki wa mtoto wa rais , mahawala wa mke wa raisi kabla hajaolewa na rais, waliokataliwa na wanainchi kwenye chaguzi kuu, waliofungwa wakatoka jela kwa msamaha wa rais woteee watapata vyeo kama ukurugenzi, ukuuwa wilaya na mkoa na vyeo vingine. Wanye kustahili na sifa za kutosha watakosa.

.

Hayo mbona yapo chadema sasa hivi? Unataka ushahidi?
 
Hata kama ingekuwa kweli hayo ni ya wana-Chadema, wana uhuru wa kuamua kujiongoza jinsi wanavyotaka na yule anayekubaliana nao anaweza kujiunga nao na yule asiyekubaliana nao halazimiki kujiunga nao !

Hapa tunazungumzia katiba ya taifa la Tanzania, ambalo ni mali yetu sote na hamna option ya kujiunga au kutojiunga !. As long as sisi ni watanzania chochote kinachowekwa kwenye katiba kitatuathiri wote in a positive or negative way !

Tanzania ni zaidi ya CDM, CUF, NCCR, CCM etc.....huwezi kutaka Tanzania ifanye kile kinachofanyika CDM, CUF, CCM etc !. Katiba ya Tanzania inabidi iweke misingi ya kitaifa na iwe mfano ili vyama vilivyopo na vitakavyokuja viige kwenye hizo values za kitaifa !.

Hayo mbona yupo chadema sasa hivi? Unataka ushahidi?
 
'''''''''''''''''''''
nasema hapana ina maana gani , kwani hutaki hata haki ya kuishi , kuabudu , kusoma , kuishi , kuenzi muungano , kuilinda tanzania kwa gharama yoyote , demokrasia , haki za binadamu kwa ujumla ,n.k. Naomba unieleweshe ili ikae vizuri . Na , tusaidie vipi ambavyo ni hapana kwenye katiba iliyopendekezwa ili tusije tukabatizwa hapana kw kila kitu tuakaonekana ni wehu kitaani .please nieleweshe.

samaki akioza mmoja katika kapu,analeta uvundo hata kwa wengine,ndiyo maana inasemwa hivi samaki mmoja akioza wote wameoza.kula ya hapana ni sahihi kabisa kwa vifungu vyote ni sahihi kabisa.
 
ebaeban , ulizotoa ni hoja sawa lakini nachotakakujua na kuelewa kwa wewe ulitaka madaraka ya Rais yaweje. Na hata yakiwa kama unavyotaka harafu haki ya kuishi na kuulinda muungano wa Tanzania ambayo ndiyo tunu yetu kwa karne ya sasa vikaondolewa , unaona itakuweje kwa vizazi vijazo. Au tupinge katiba iliyopendekezwa ili tuipate Tanganyika yetu ambayo kwa mtu aliyezaliwa kuanzia miaka ya 1967 haelewi ilitokana na nini na kwanini iliitwa Tanganyika , na isiitwe MBEYA au DAR ES SALAAM .Naomba nieleweshwe ili tuwe pamoja , am sorry .Nachoomba ni ushauri tu .:hail:


Pana mambo ya msingi ambayo hayawezi kuondolewa katika katiba kama haki ya kuishi/kuabudu na mengine ya msingi.Hivi ni kwa nini unaamini kwamba ikija hiyo Serikali tatu na ukaipata Tanganyika basi unaondolewa moja kwa moja haki yako ya kuishi?.Kwa nini na wewe unaamini Serikali tatu itavunja Muungano wetu.Hebu na wewe utujibu hayo maswali sababu nna wasi wasi usiokuwa na shaka umezikariri zile fikra za Raisi Kikwete alipofungua lililokuwa Bunge la katiba ambapo alisema Serikali tatu jeshi litapindua nchi.Tafadhali tujibie hayo maswali kwanza.
 
'''''''''''''''''''''
nasema hapana ina maana gani , kwani hutaki hata haki ya kuishi , kuabudu , kusoma , kuishi , kuenzi muungano , kuilinda Tanzania kwa gharama yoyote , Demokrasia , haki za binadamu kwa ujumla ,n.k. Naomba unieleweshe ili ikae vizuri . Na , tusaidie vipi ambavyo ni hapana kwenye katiba iliyopendekezwa ili tusije tukabatizwa hapana kw kila kitu tuakaonekana ni wehu kitaani .Please nieleweshe.

Wakati wa jk nyerere kulikuwa na upigaji wa ndio na hapana, waliokuwa wanapiga hapana ina maana hawakujua kuwa kuna mambo mazuri alisha yafanya?
 
Kura ya hapana imezidi kupata wafuasi na vyama vya siasa baada ya CHADEMA kutangaza wazi kuunga mkono kura ya HAPANA na ufunguzi kufanyika tarehe 14 kwa kongamano.

Kongamano litaoongozwa na viongozi wa CHADEMA , Profesa Lwaitama na mjumbe wa kamati ya kukusanya maoni Humphrey polepole.

Na hii imefanya watu waliojitoa waziwazi kuunga kura ya hapana kuongezeka baada ya askofu wa jimbo la rulenge askofu niwe mgizi kutangaza waziwazi.

Mtihani mkubwa bado hupo kwa baadhi ya vyama vilivyokaa kimya . Cuf na nccr katika umoja UKAWA.

Ambavyo havijasema lolote kama watashiriki au la

UKAWA kwa umoja wetu tunasema HAPANA hakuna mjadala wala Ukimya wa CUF wala NCCR, wote walishasema hapana.
 
Hata kama ingekuwa kweli hayo ni ya wana-Chadema, wana uhuru wa kuamua kujiongoza jinsi wanavyotaka na yule anayekubaliana nao anaweza kujiunga nao na yule asiyekubaliana nao halazimiki kujiunga nao !

Hapa tunazungumzia katiba ya taifa la Tanzania, ambalo ni mali yetu sote na hamna option ya kujiunga au kutojiunga !. As long as sisi ni watanzania chochote kinachowekwa kwenye katiba kitatuathiri wote in a positive or negative way !

Tanzania ni zaidi ya CDM, CUF, NCCR, CCM etc.....huwezi kutaka Tanzania ifanye kile kinachofanyika CDM, CUF, CCM etc !. Katiba ya Tanzania inabidi iweke misingi ya kitaifa na iwe mfano ili vyama vilivyopo na vitakavyokuja viige kwenye hizo values za kitaifa !.

Mkuu umetumia akili nyingi sana kumjibu huyu FAIZAFOXY asielipendea mema taifa hili
 
'''''''''''''''''''''
nasema hapana ina maana gani , kwani hutaki hata haki ya kuishi , kuabudu , kusoma , kuishi , kuenzi muungano , kuilinda Tanzania kwa gharama yoyote , Demokrasia , haki za binadamu kwa ujumla ,n.k. Naomba unieleweshe ili ikae vizuri . Na , tusaidie vipi ambavyo ni hapana kwenye katiba iliyopendekezwa ili tusije tukabatizwa hapana kw kila kitu tuakaonekana ni wehu kitaani .Please nieleweshe.

Ndugu huyu bwana kusema hapana hajakosea kwa sababu katika kura za katiba hakuna kupigia kifungu kwa kifungu kura hupigwa kwa ndio au hapana kwa katiba yote
 
Katiba hii pendekezwa ni mbaya kwa sababu;-

1. Tanzania upande wa Zanzibar kazi yao ni kutoa makamo wa rais , urais wenyewe Ngo`ooooo.

2. Maadili ya viongozi yaliyopendekezwa na tume ya kukusanya maoni yamefutwa, madhara yake mtumishi wa umma atataka kupata kiti tu na meza kwenye ofisi za umma hata asipopewa mshahara ndani ya mwaka mmoja tu wa ajira atakuwa amajenga nyumba , amenunua gari , amafanya harusi kubwa hadi kuchinja ngamia.

3. Madaraka ya rais kupunguzwa kama ilivyopendekeza tume ya Warioba imefutwa madhara yake,mashemeji wa mke wa rais, marafiki wa mtoto wa rais , mahawala wa mke wa raisi kabla hajaolewa na rais, waliokataliwa na wanainchi kwenye chaguzi kuu, waliofungwa wakatoka jela kwa msamaha wa rais woteee watapata vyeo kama ukurugenzi, ukuuwa wilaya na mkoa na vyeo vingine. Wanye kustahili na sifa za kutosha watakosa.

4. Ubunge au udiwani wawe na Elimu ingalao kidato cha nne imefutwa madhara yake, hii italeta madhara makubwa sana sana kwenye halimashuri kwa sababu wasimamizi ambao ni madiwani watazidiwa sana ki-elimu na watendaji wa halimashauri ambao ni mkurugenzi na wakuu wake wa idara. Fedha za kodi hukusanywa na TRA na zote hupelekwa hazina,kule hazina fedha hizo hurudishwa kwenye halmashauri ambako kuna watu kwa ajili ya kutekelezwa miradi mbali mbali ya maendeleo. Sasa kwa kuwa wasimamizi (madiwani) ambao wengi wao ni darasa la saba watashindwa kuzisimamia fedha hizo kutokana na umbumbu wao, watendaji(mkurugenzi na mkuu wake wa idara) watatumia mwanya huo watawaibia fedha zote mwisho wa siku miradi haitakamilika. Mfano hai halmashauri ya wilaya ya Mtwara chini ya mbunge Hawa Ghasia ina madiwani mambumbu tupu. Idara ya afya tulikula fedha zote za Semina za ukimwi, tulitengeneza semina hewa kwa maana waliohuzudhuria walikuwa ni hewa, attendance registar ilikuwa ni hewa, payment vocha tuliandika majina hewa na tukatia sahihi zao hao watu hewa na tukuchukua mshiko wote shs 60,000,000/= madiwani husika walitia sahihi zao kwenye ripoti tuliyowapelekea HAWAKUJUA CHOCHOTE MASKINI. Huu ni mfano wa halmashauri moja tu na zingine ni hivyo hivyo lakini kama madiwani wangekua na elimu ya kutosha kwa maana wangafanya monitoring kule site wangeangalia majina na kuwafuata wahusika lazima tungekamatwa.

5. 50 kwa 50 katika vyombo vya maamuzi wanawake na wanaume hii ina madhara makubwa sana kwa sababu muumba mwenyewe aliliona hili akaweka viwango na kila mtu anajua mungu alimpa mamlaka nani, hata hivyo hilo la 50 kwa 50 likitekelezwa kwenye majeshi, inchi itatekwa, Majambaji yatakuwa kila siku yanakimbia, Takukuru hawawezi kuwakamata wanaopokea hela za moto maana mala zote watuhumiwa watawashinda nguvu watakimbia na hela za moto zitapotea serikali itakula hasara.

Hii ni mifano michache tu ya ubovu wa katiba pendekezwa ya wabunge wa CCM,ILE YA WARIOBA ILIKUWA BOMBA WATU KAMA AKINA RAGE wasingepata uongozi tena ndani ya katiba ya tume ya Warioba.

Wale waliokuwa wanaitwa UKAWA walifanya makosa makubwa sana kususia wangebaki mule mule ila wakomae na rasimu ya WARIOBA, waliwaachia nyani shamba la mahindi.

Ikija KATIBA hiyo wanainchi tuikatae kabisa.

Mchango wako ni poa sana ila tu hapo uliposhindwa kufahamu au kukubali kuwa UKAWA walikuwa sahihi kuondoka na kususia. Hawa wajumbe walitoka baada ya kuona kuwa walikuwa hawana tena hata chembe ya kusikilizwa. Badala ya mijadala yenye busara na uelewa vilikuwa ni vijembe tupu na zaidi uliona uvunjifu wa kanuni ulianza na Raisi na uliendelea hadi dakika ya mwisho. Ulijionea mwenyewe katika kura za maoni. Nadhani umeshapata habari kuwa hata ambao hawakushiriki kwenye kura ya mwisho wameorodheshwa kama vile walishiriki.
Kwa ajili hiyo walikuwa sahihi kupisha jambo hilo maana lingesababisha wao baadaye wazuliwe kesi za kukosa ustaarabu kwa kuleta fujo kumbe ni ubabe wa Sita ambao ulikuwa unatumiwa kama chombo cha kupitisha mambo yasiyopendekezwa na wananchi.
Ukiangalia kwa makini sana utaona kuwa ni wazi CCM hawakutaka kuwepo kwa Katiba mpya, tangu mwazoni, maana hili ni jambo wanaharakati wamelidai muda mrefu sana likawa linafanyiwa ubabe huo huo. Hata waziri wa katiba naye alionyesha muelekeo wao huo, ila walipoona hana nguvu ya kuwakabili wanaharakati wakambadilisha haraka ili watafute wababe zaidi kuhakikisha hatupati katiba mpya.
Lakini kizuri ni kuwa picha yote sasa iko wazi, mwananchi asiyeiona au kujifanya kipofu ni uhuni wake tu anaendekeza au anacho kinachomfaidisha katika mfumo wa sasa ambao kila mmoja wetu anafahamu kuwa hauna tofauti na mfumo wa kiimla. Na hautuhakikishii maendeleo ya haraka. Wakati wenzetu wanakwenda kasi ya kilometa 100 kwa saa sisi tutabakia na mwendo ule ule wa kilometa 2 kwa saa na kila nusu saa tunachoka na kukaa chini tukihema halafu tuendelee tena mwakani, tutamkuta nani akitusubiri wa TZ?
Naomba tubadilike sasa.
 
Back
Top Bottom