Kupotea bila kujijua

Mkuu washkaji walishafariki[emoji30] pole sana
Ila naskia moro kuna maajabu sana
 
Mzee baba tusilishane matango bana... Musoma kwetu pia
Kuwa musoma haimaanishi basi kila kitu kitokacho musoma unakijua!!

Musoma ipi unayozungumzia na Mimi musoma ipi niliyozungumzia?!
Hilo jambo ukimweleza hata Mkono(mbunge)atakweleza mana amewahi kuishi na kuchunga katika maeneo niliyoyataja

Kuwa wa musoma haimaanishi basi kila kitu wakijua ndugu

Wewe kama wa Musoma walau unajua lilipo gereza la Cuba?!
Unayajua maajabu ya mlima Kyahaza?
Unajua walau utaratibu wa kufika lilipo handaki la Mwalimu Nyerere?!

Ukinijibu yote hayo nitaamini nimewalisha matango pori
 
Ushasema pori lina vichaka vinafanana.

Ulijuaje kwamba hapo ulipoitafutia ndiyo hapo hapo ulipoiacha baiskeli na hujachanganya machaka tu katika pori?

Kwa maneno mengine, kama pori lina machaka yanafanana, na wewe mgeni pori hilo, unajuaje kwamba hujaacha baiskeli chaka A, ukapotea na kuitafuta baiskeli chaka B, wakati ipo chaka A, hukuiina chaka B, ukaondoka na miaka mitano baadaye ukarudi chaka A ulipoiacha ikiwa na kutu na haijaguswa na mtu?
 
Thibitisha habari zako, zaidi ya hapo huwezi kuepuka kuambiwa unaleta ngano tu.
Hope haupo Bongo na siku ukitua hapa kwetu(kama niko sahihi)nitafute pm tuzurure kidogo maeneo kadhaa ya vijijini huko,ama twende tu kama watalii Mwitongo Butiama kisha tupate ruhusa ya kuzama humo na tusipotafutwa basi njoo thibitisha hakuna vitu kama hizo!

Kwanza ni tukio linalokukuta wakati usiotarajia na haijalishi ni mzee ama mtoto na jambo hili si jamii flani tu wanalifahamu,ni jamii nyingi sana

Hivyo uthibitisho gani unataka!! Nijirekodi clip wakati napotea au ulimaanisha uthibitisho gani utakao kufikia wewe uamini?!
 
Sio fiction ni tukio LA kweli kabisa na Yale maji tuliyakuta vile vile kwenye dumu ndio kilichonithibitishia ni baiskeli yangu niliyoipoteza mwaka 1997
aisee " mlivamia ',Mji wawatu Maui" shukuru ' haukupotea wew
 
hahaaa eti " nijirecord clip "
 
Kuna mambo mengi hayaeleweki lakini hilo halina maana ni mastaajabu yanayokiuka sheria za kisayansi.

Uthibitisho unaotakiwa ni wowote ulio na uthabiti wa kimantiki na usioweza kuwa na tonw la kuweza kujipinga wenyewe, hata kidhana tu, si lazima uweke video.
 
Hizo ni "Tales" tu ...
 
mkuu nikija kyabakari ntakutafuta
 
Sina hakika kama usithibitisho wowote utauamini kwa sababu tayari umenitajia neno SAYANSI na mlengo wako upo huko
Sayansi jambo ambalo sina uhusiano nalo na sinaga muda wa kufikiria sayansi ya mwanadamu mwenye nyama kama mimi

Hivyo basi nachelea kukwambia kwamba uthibitisho pekee ni wewe kuishi katika ukweli huo namaanisha walau kufika na kuwa miongoni mwa wahanga wa tukio hilo

Tofauti na hapo huwezi kunielewa na utaishia kutaja neno ngano tu kwa kuhusisha mawazo ya kina Shaban Robert
 
hahaaa eti " nijirecord clip "
Yah mana kama hayajakukuta utaishia kuomba uthibitisho na tukio linatokea hata wazo huna na ukieleza watu wa aina yake akikustahi sana atakwambia punguza pombe
 
Jambo la sayansi huna uhusiano nalo wakati unatumia internet?

Unaelewa ulichoandika?

Unaleta habari za "Baniani mbaya, kiatu chake dawa"?
 
Jambo la sayansi huna uhusiano nalo wakati unatumia internet?

Unaelewa ulichoandika?

Unaleta habario za "Baniani mbaya, kiatu chake dawa"?
Kwani SAYANSI ni nini?!
Najua nilichokiandika ndugu wala usidhani sijui niandikacho.
Nina uhusiano na maarifa ya wanadamu ila Sina uhusiano na Sayansi mana siijui
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…