Kupendeza sio kuvaa nusu uchi

Kupendeza sio kuvaa nusu uchi

Soja p

Senior Member
Joined
Aug 24, 2017
Posts
190
Reaction score
223
Kila mtu anapenda kuvaa na kupendeza, lakini angalia jinsi unavyo vaa ukiwa mbele za watu kwan jinsi unavyo vaa ndivyo watu watakavyo kufahamu kwa kupitia uvaaji na muonekano wako

Kupendeza sio kuvaa nguo fupi zaidi hadi kuacha sehemu zisizo sitahili kuonekana kila Unapopita au kuvaa nguo inayo kubana zaidi kiasi kwamba inakuonesha maungo yako yote hadi nguo za ndani

Unakuwa u namaanisha nini au unalengo gani kuvaa nguo fupi zaidi hadi kuacha sehemu zingine kuonekana au kuvaa nguo inayo kubana zaidi kiasi kwamba inakuonesha maungo yako yote na kukuchoka jinsi ulivyo hadi ndani?

Unataka wanaume wakutamani? Au ni biashara unatangaza watu waone? Kama si hivyo sasa unataka kumuonesha nani mwili wako? Au unapenda Unapo pita sehem wanaume wote wageuke kukutazama?

Sasa kama umeamua kuvaa ivo mbona Ukifika kwa watu unaanza kulazimisha nguo iwe ndefu unaivuta kana kwamba hukujiona wakati unavaa?

Mbona ukipita kwa watu unaanza kunificha ficha unaogopa jinsi nguo ilivyo kubana hadi unashidwa kutembea?

Watu watakuheshim vip wakati unavaa nusu uchi? Kila unako pita kila mtu anakuona had nguo ya ndani

Vaa mavazi ya heshima kwanin kupendeza sio kutembea nusu uchi huko ni kujidharirisha

Vaa vizuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wanajua kupendeza ni kuvaa nguo nusu akipita watu wanamshangaa ye anajua wamependa nguo zake kumbe wanamshangaa kavaa hovyo,wanajidhalilisha tu. Mtu ukivaa nguo tu ya kukufit vizuri bila kukuacha uchi unapendeza zaidi
 
Inapendeza kuona wakina Dada wakitoa michango yao kuonesha kuwa na wao wenyewe (wakina Dada) hawapendezewi.

Safi sana
 
Back
Top Bottom