Ukimpenda mtu, unapomwona tu, moyo unaanza kudunda boom, boom, boom.... Na moyoni utakuwa radhi kumpa CHOCHOTE anachotaka. Nasema chochote maana ndivyo ilivyo-iwe ni nyumba au gari au chochote. Mpenzio asipokupigia simu siku nzima, lazima utataharuki. Na akisafiri unam- miss ile mbaya. Kama wewe ni mwanamke halafu feelings kama hizo hujawahi kuzipata, basi kitaalamu wewe unaitwa 'frigid' (yaani huna hisia bali ni 'baridi' kama friji). Kama wewe ni mwanaume, basi ni wale wanaoitwa 'players' - hatulii, anaonja kila kitu na hachagui. Mtu wa kawaida lazima anafika mahali anapenda kwa dhati. Mara nyingi mtu anayeshindwa kupenda kwa dhati ana jini mahaba linalomsumbua. Atajikuta anaota ndoto za ngono n.k. Duniani hakuna kitu kitamu kama kuwa na mtu anayekupenda na wewe unampenda-hakuna! Hata ukiwa na matrilioni ya dola kama huna mtu anayekupenda kwa dhati (sio kwa sababu ya pesa zako), utajiri wako ni bure. Yaani utamu wa kupendwa acha tu!!!!