Kupanda kwa Dollar kunavyoongeza Deni la Taifa

Kupanda kwa Dollar kunavyoongeza Deni la Taifa

Mstahiki Mea

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2018
Posts
5,581
Reaction score
10,111
FB_IMG_1751042256750.jpg

Hivi unafahamu kuongezeka kwa thamanI ya Dolllar ya Marekani kivyovyote kuna athari kubwa katika deni la taifa?

Hili jambo wengi hawalifahamu na hata wakilifahamu wanaona kama halina athari lakini ukweli nikwamba deni linakopwa kwa USD , na malipo yake hufanyika kwa fedha hiyo hiyo .

Sasa tuchukulie deni lilikuwa triliin 50 mwaka 2015 wakati dollar ikiwa 2200 leo ukilipa au kutaja deni hilo litakuwa limeongezeka automatic kwakuwa sasa dollar ni 2665 na kama ukilipa itakuhitaji kulipa Trilion 60, hapo ni bila riba hilo ongezeko limetokana na thamani iliyoongezeka kwa USD.

Jambo hili nimuhimu lisemwe pia
 
Kwa mwaka 2015, kiwango cha kubadilisha fedha kilikuwa takriban:

1 USD ≈ 2,000–2,200 TZS (Tsh)

Sasa tukibadilisha trilioni 50 TZS kuwa dola za Marekani:

50,000,000,000,000 ÷ 2,200 ≈ 22,727,272,727 USD

Hii ni sawa na takriban dola bilioni 22.7 kwa makadirio ya mwaka 2015.
(Kiwango halisi kilitegemea soko, benki na muda husika.)

Kulingana na viwango vya kubadilisha fedha vya hivi karibuni, dola 1 ya Marekani (USD) inalingana na takriban shilingi za Kitanzania (TZS) 2,655.

Kwa hivyo, dola za Marekani 22,727,272,727 zinakuwa sawa na:

22,727,272,727 USD × 2,655 TZS/USD = 60,353,454,090,785 TZS

Hii ni takriban shilingi trilioni 60.35
 
Wenyewe wanakuambia TRA mapato yameongezeka, kiuhalisia hayo madeni ni kama trap na wakopaji na walioweka hiyo system wanajua hakuna kuchomoka, nia kukufanya depended 💯 ili kukumiliki , sad but true
 
Kwa mwaka 2015, kiwango cha kubadilisha fedha kilikuwa takriban:

1 USD ≈ 2,000–2,200 TZS (Tsh)

Sasa tukibadilisha trilioni 50 TZS kuwa dola za Marekani:

50,000,000,000,000 ÷ 2,200 ≈ 22,727,272,727 USD

Hii ni sawa na takriban dola bilioni 22.7 kwa makadirio ya mwaka 2015.
(Kiwango halisi kilitegemea soko, benki na muda husika.)

Kulingana na viwango vya kubadilisha fedha vya hivi karibuni, dola 1 ya Marekani (USD) inalingana na takriban shilingi za Kitanzania (TZS) 2,655.

Kwa hivyo, dola za Marekani 22,727,272,727 zinakuwa sawa na:

22,727,272,727 USD × 2,655 TZS/USD = 60,353,454,090,785 TZS

Hii ni takriban shilingi trilioni 60.35
Ungemalizia hapo iliyoongezeka ni trilioni 10.
Dah, pesa nyingi sana hii..
 
View attachment 3385981
Hivi unafahamu kuongezeka kwa thamanI ya Dolllar ya Marekani kivyovyote kuna athari kubwa katika deni la taifa?

Hili jambo wengi hawalifahamu na hata wakilifahamu wanaona kama halina athari lakini ukweli nikwamba deni linakopwa kwa USD , na malipo yake hufanyika kwa fedha hiyo hiyo .

Sasa tuchukulie deni lilikuwa triliin 50 mwaka 2015 wakati dollar ikiwa 2200 leo ukilipa au kutaja deni hilo litakuwa limeongezeka automatic kwakuwa sasa dollar ni 2665 na kama ukilipa itakuhitaji kulipa Trilion 60, hapo ni bila riba hilo ongezeko limetokana na thamani iliyoongezeka kwa USD.

Jambo hili nimuhimu lisemwe pia
Me nadhani tusipotoshe Umma unapokopa katika Dola nautakapoanza kulipa sio kweli deni linaongezeka in number kama ulivyoainisha bali utatumia pesa mingi kulilipa kwa hayo mabadiliko ya dola lakini mnajichanganya sehemu moja pia mnauambia umma huo huo kua shilingi inaimairika hii inamaanisha dola ulizokua ukizipata na shilingi nyingi niaka kadhaa iliyopita utazipata kwakutumia shilingi chache kwa sasa sasa tulizeni akili mnapoleta taarifa katika umma msije kudhani mna deal na masisiemu tupu ambayo yanakubali kila kitu pasipo kuuliza jipangeni unless mtuambie kuna mfumuko wa bei na mdodororo wa sarafu yetu hivyo vinatuongezea gharama katika ulipaji wa deni ila ukutuambia eneo moja mnafanya vizuri na uchumi kukua above average ya Dunia nikutukosea heshima walipa deni.

No reform No Election
 
Rekebisha hapo, Sio kupanda kwa Dollar, Ni kuporomoka kwa Tsh. zidi ya Dollar, Hii inaleta tafsiri sahihi kua ni tatizo la ndani la sera mbovu za kiuchumi zinafanya shilingi yetu iporomoke.

Anakwepesha ukweli kwa kusema Dollar imepanda ili muone sio makosa ya Serikali yake
 
Rekebisha hapo, Sio kupanda kwa Dollar, Ni kuporomoka kwa Tsh. zidi ya Dollar, Hii inaleta tafsiri sahihi kua ni tatizo la ndani la sera mbovu za kiuchumi zinafanya shilingi yetu iporomoke.

Anakwepesha ukweli kwa kusema Dollar imepanda ili muone sio makosa ya Serikali yake
Nikweli mkuu
 
Kama yale maneno yanatoka kwa kipngozi mkuu 2q Taifa, kweli Tanganzania ina safari ndefu kuondokana kwenye umasikini!
 
Riba mnayoilipa ndio kichaa zaidi kwa deni kubwa namna hilo

Hii ni kausha Moyo sio damu tena
Lakini matamshi ya Trump kusema ana majina kama manne ya kumrithi Jerome Powell kumesababisha $ kushuka

Huku £ leo Baada ya kauli hiyo unabadili kwa $1.37
Wachambuzi na wana Uchumi mnasemaje
 
Riba mnayoilipa ndio kichaa zaidi kwa deni kubwa namna hilo

Hii ni kausha Moyo sio damu tena
Lakini matamshi ya Trump kusema ana majina kama manne ya kumrithi Jerome Powell kumesababisha $ kushuka

Huku £ leo Baada ya kauli hiyo unabadili kwa $1.37
Wachambuzi na wana Uchumi mnasemaje
Kweli mkuu
 
Ninaweza kusema hivi...

Ni kweli kwamba kupanda kwa thamani ya dola kuna athari katika deni la taifa lililokopwa kwa USD, hasa likihesabiwa kwa shilingi. Hata hivyo, ni muhimu kuelewa kwamba thamani ya shilingi dhidi ya dola inaakisi mabadiliko ya jumla ya bei katika uchumi wetu.... mfumuko wa bei...

Kadri shilingi inavyopungua thamani dhidi ya U$D, ndivyo pia bei za bidhaa na huduma hupanda kwa kiasi kama hicho. Hii ina maana kwamba uwezo wa serikali kukusanya mapato kwa shilingi pia hupanda kulingana na hali hiyo.


Kwa mfano, kama soda iliuzwa Tsh 200 mwaka 2005 na sasa ni Tsh 600, hiyo inaonyesha kuwa thamani halisi ya shilingi imebadilika, lakini pia mapato ya serikali kutoka kwenye shughuli kama hizo yameongezeka kwa uwiano ule ule. Hivyo, deni lililokuwa dola milioni 1 mwaka 2015 wakati dola ikiwa Tsh 2200 linaweza kuonekana kuwa ni shilingi bilioni 2.2 wakati huo, na leo linaonekana kuwa Tsh 2.665 bilioni kwa kiwango cha sasa cha dola 2,665 – lakini ni lazima tufahamu kuwa pia uwezo wa kulipa kwa ndani umebadilika kwa uwiano huo huo....


Nahitimisha kwa kusema ni mabadiliko ya thamani ya fedha, si ongezeko halisi la deni....
 
Yule waziri ‘cha-uongo’ sijui atakuja na kamba gani baada ya ‘bi-tozo’ kukiri deni la serikali pekee ni trillion 107.7 na sio deni la nchi kama alivyotaka kutuzuga.
 
Back
Top Bottom